Hii ndiyo sheria ya Wapangaji wote kulipa 10% ya Kodi ya nyumba TRA

lord atkin

Senior Member
Sep 30, 2018
197
683
Mwanzoni ilikuwa Wapangaji wa nyumba na ofisi Kwa ajili ya biashara tu (commercial/business) ndiyo waliokuwa wakitakiwa kulipa withholding tax ya asilimia kumi (10%) TRA. Kifungu Cha 82(2)(a) Cha The Income tax Act RE 2019 kiliweka wazi kuwa mtu asilipishwe withholding tax ya pango la jengo au nyumba kama halitumii Kwa biashara. Hivyo Wapangaji wa fremu za maduka, maofisi na biashara zinginezo tu ndiyo waliotakiwa kulipa Kodi ya withholding tax ya 10% TRA.

Bunge letu tukufu kupitia sheria ya fedha ya 2022, (The Finance Act, 2022) Kwa busara zake liliifanyia marekebisho sheria ya Kodi yaani The Income Tax Act R.E 2019 na kufuta kifungu Cha 82(2)(a) kilichokuwa kimetoa maelekezo kuwa wanaopaswa kulipa Kodi ya withholding tax ya 10% ya pango ni wale tu wanaopanga nyumba Kwa madhumuni ya biashara.

Kufuatia marekebisho haya ya sheria Sasa ni Kila mpangaji hata wale wanaopanga nyumba Kwa ajili ya makazi binafsi (residences) wanatakiwa kulipa asilimia 10 ya Kodi ya nyumba ya Kila mwezi TRA kama withholding tax na utaratibu uliotolewa na TRA ni kwamba wanapaswa kulipa wapangaji na kuwapelekea risiti wenye nyumba kuwa asilimia 10 imekwisha lipwa TRA.

Marekebisho haya ya sheria yameanza kufanya kazi July 2022 pamoja na bajeti ya Serikali. Hivyo ni wajibu wetu kama wananchi kuiunga mkono Serikali yetu sikivu Kwa kuchangia mapato na kutii sheria bila shuruti.

Alamsiki

View attachment tz-act-2022-1-publication-document.pdf
Soma kifungu kilichobadilishwa hapa chini

Screenshot_20220825-195352_1.jpg


Kabla ya madiliko hapa chini

Screenshot_20220825-194109_1.jpg
 
Hehehehe mimi siwezi kumlaumu Mwigulu, yupo pale kutekeleza anachoagizwa ili kutetea ugali wake maana akileta ujuaji kibarua kinaondoka ( mfano ni Job & mtumishi aliyefukuzwa juzi)

Ni upumbavu na kutotaka kukubaliana na uhalisia pale mtu anapoamua kusema kuwa SHH anahujumiwa na mawaziri, unless akubali kwanza kuwa SHH ni punguani ndipo hoja yake italete mashiko, kwakua mamlaka yote juu ya hao mawaziri anayo.

Tozo zote hizi kinachotafutwa ni hela ya safari zake, maana kiuhalisia angesema ategemee pato lilelile isingewezekana.
 
Mwanzoni ilikuwa Wapangaji wa nyumba na ofisi Kwa ajili ya biashara tu (commercial/business) ndiyo waliokuwa wakitakiwa kulipa withholding tax ya asilimia kumi (10%) TRA. Kifungu Cha 82(2)(a) Cha The Income tax Act RE 2019 kiliweka wazi kuwa mtu asilipishwe withholding tax ya pango la jengo au nyumba kama halitumii Kwa biashara. Hivyo Wapangaji wa fremu za maduka, maofisi na biashara zinginezo tu ndiyo waliotakiwa kulipa Kodi ya withholding tax ya 10% TRA.

Bunge letu tukufu kupitia sheria ya fedha ya 2022, (The Finance Act, 2022) Kwa busara zake liliifanyia marekebisho sheria ya Kodi yaani The Income Tax Act R.E 2019 na kufuta kifungu Cha 82(2)(a) kilichokuwa kimetoa maelekezo kuwa wanaopaswa kulipa Kodi ya withholding tax ya 10% ya pango ni wale tu wanaopanga nyumba Kwa madhumuni ya biashara.

Kufuatia marekebisho haya ya sheria Sasa ni Kila mpangaji hata wale wanaopanga nyumba Kwa ajili ya makazi binafsi (residences) wanatakiwa kulipa asilimia 10 ya Kodi ya nyumba ya Kila mwezi TRA kama withholding tax na utaratibu uliotolewa na TRA ni kwamba wanapaswa kulipa wapangaji na kuwapelekea risiti wenye nyumba kuwa asilimia 10 imekwisha lipwa TRA.

Marekebisho haya ya sheria yameanza kufanya kazi July 2022 pamoja na bajeti ya Serikali. Hivyo ni wajibu wetu kama wananchi kuiunga mkono Serikali yetu sikivu Kwa kuchangia mapato na kutii sheria bila shuruti.

Alamsiki

View attachment 2334773
Soma kifungu kilichobadilishwa hapa chini

View attachment 2334774

Kabla ya madiliko hapa chini

View attachment 2334776
Kumekucha !!
 
Back
Top Bottom