mwehu ndama
JF-Expert Member
- Nov 12, 2019
- 543
- 1,837
Nisikilizwe Nina hoja!
Baada ya hivi karibuni kutangaza kufanya maamuzi magumu tena ya kishujaa ya kumkufukuza mke wangu hapa nyumbani na kumrudisha kwao, kutokana kuninyima uhuru wa kuishangilia Yanga sc na kuwatetea kina pacome na Guede mitandaoni, nimekuwa nikipokea jumbe za matusi na kejeli DM.
Ila niweke wazi kuwa msimamo wangu hautobadilika ni heri niishi kwa punyeto huku nikiishangilia Yanga sc kwa uhuru. Sitaki ushauri, tena mnikome, na mkichonga sana kumbukeni na hapa ipo!
Ratiba yangu ya sasa ya kila siku baada ya kumfukuza mke wangu ili niishangilie Yanga sc ni kama ifuatavyo.
Saa 1-4 asubuhi: naamka naingia mitandao yote ya kijamii kuisifia Yanga na kupambana na comment zote mbovu dhidi ya Yanga.
Saa 4-7 mchana: natuma meseji za kuomba msaada wa hela ya kula kwa wanayanga wenzangu, nikikosa natembea kwa mguu mpaka makao mkuu yetu pale jangwani kupata supu na chapati za bure.
Saa 7-10 jioni: natembelea vijiwe vyote vya kahawa maeneo ya kariakoo na katika kila kijiwe naanzisha mada ya Pacome vs chama kisha namtetea Pacome kwa nguvu zote mpaka nieleweke, na itakapolazimu makonde kurushwa niko tayari
Saa 10-2 usiku : naanza kumsifia eng. Hersi Said na Gsm, hii itamuhusu kila atakaye niongelesha ndani ya haya masaa, kila baada ya salamu ntahakikisha nachomekea mada ya Yanga sc na kuanza kumsifia engineer.
Saa 2-4 usiku : Natazama marudio ya mechi ya Yanga sc 5 vs 1 Mbumbumbu fc, nikimaliza nalala.
Baada ya hivi karibuni kutangaza kufanya maamuzi magumu tena ya kishujaa ya kumkufukuza mke wangu hapa nyumbani na kumrudisha kwao, kutokana kuninyima uhuru wa kuishangilia Yanga sc na kuwatetea kina pacome na Guede mitandaoni, nimekuwa nikipokea jumbe za matusi na kejeli DM.
Ila niweke wazi kuwa msimamo wangu hautobadilika ni heri niishi kwa punyeto huku nikiishangilia Yanga sc kwa uhuru. Sitaki ushauri, tena mnikome, na mkichonga sana kumbukeni na hapa ipo!
Ratiba yangu ya sasa ya kila siku baada ya kumfukuza mke wangu ili niishangilie Yanga sc ni kama ifuatavyo.
Saa 1-4 asubuhi: naamka naingia mitandao yote ya kijamii kuisifia Yanga na kupambana na comment zote mbovu dhidi ya Yanga.
Saa 4-7 mchana: natuma meseji za kuomba msaada wa hela ya kula kwa wanayanga wenzangu, nikikosa natembea kwa mguu mpaka makao mkuu yetu pale jangwani kupata supu na chapati za bure.
Saa 7-10 jioni: natembelea vijiwe vyote vya kahawa maeneo ya kariakoo na katika kila kijiwe naanzisha mada ya Pacome vs chama kisha namtetea Pacome kwa nguvu zote mpaka nieleweke, na itakapolazimu makonde kurushwa niko tayari
Saa 10-2 usiku : naanza kumsifia eng. Hersi Said na Gsm, hii itamuhusu kila atakaye niongelesha ndani ya haya masaa, kila baada ya salamu ntahakikisha nachomekea mada ya Yanga sc na kuanza kumsifia engineer.
Saa 2-4 usiku : Natazama marudio ya mechi ya Yanga sc 5 vs 1 Mbumbumbu fc, nikimaliza nalala.