Hii ndiyo hali halisi ya Brake Point Posta na Nexus Victoria

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,285
9,922
Na miaka miwili toka nianza shughuli zangu mikoani hivyo na muda kidogo sijafika maeneo ya Posta, leo nilipanga niende Posta lengo ni kwenda kununua bidhaa , kuna msela wangu mikaa 5 sasa imepita, alikuwa ananiuzia shati, Jeans, Na Makoti ya suti makali ya mtumba kali.

Nasikitika msela wangu sikuweza baada ya kumulizia kwa jamaa niliwakuta kwenye kijiwe hicho walinitonya kuwa jamaa aliamua kuacha biashara baada ya hali ya biashara kuwa ngumu.

Basi niliamua kuungisha jamaa ingawa hakuwa na shati kali kivile, nikaendelee na shopping zangu ilifika muda wa Lunch nilasema ngoja nikapate Lunch pale Brake point ilikuwa mida ya saa 8:30, Dah hali nilioikuta pale nikahisi pamefungwa nini? Nilikuta wateja wasiozidi 8 kwakweli nilishangaa sana, basi nikaagiza msosi wangu nikagonga nikaondoka nikiwa na mawazo sana.

Nikaondoka zangu kufika maeneo ya victoria nikapigiwa simu kuna docs muhimuanahitaji docs ya haraka natakiwa niitume basi nikapata wazo ningie pale makumbusho stand nikaiscan then niitume. Nilipomaliza kuituma nikaenda pale Nexus àngalau kupata bia mbili tatu then niondoke hali niliikuta pale kweli nilifadhaika sana hakuna wateja kabisa.

Jamani hali ni mbaya sana

Angalia picha

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…