Habari za jioni mabibi kwa mabwana,
Bila kupoteza wakati, hebu Leo tutembelee mkoa wa iringa.
Kwa ufupi,
Jina iringa linatokana na neno lilinga, (which means fort) au boma kwa kiswahili.
Mkoa wa iringa una wilaya nne, ambazo ni Iringa manispaa, Iringa vijijini, Kilolo na Mufindi,
Katika elimu, mkoa wa iringa una shule nyingi za sekondari (ni nyingi kuzitaja) na vyuo vikuu vitatu,
Ambavyo ni
Chuo kikuu cha mkwawa
Chuo kikuu cha iringa
Chuo kikuu cha Ruaha
Pamoja na taasisi nyingine za elimu ya juu zikiwemo chuo cha ustawi wa jamii na chuo cha mafunzo ya Ualimu cha kleruu.
Shughuli za maendeleo,
Shughuli za maendeleo katika mkoa wa iringa ni kilimo, ufugaji, usindikaji na biashara,.
Kilimo ndio inayochukua nafasi kubwa, hasa katika mazao ya nafaka, mbao, mazao ya biashara kama chai, mazao ya mbogamboga n.k
Bado kuna fursa nyingi hasa katika kilimo cha misitu ya mbao katika wilaya za kilolo na Mufindi, ambazo hali ya hewa inafaa sana kwa makuzi ya misitu ya mbao. (Fursa hii vijana watz changamkieni),
Mpaka sasa mkoa wa iringa una TV station moja (IMTV) na fm Radio Stations 7
Ambazo ni
Trap Gang Radio
Ebony FM
Country FM
Nuru FM
Kibla ten FM
Furaha FM
Overcomers FM
Hivi karibuni iringa imekuwa ni manispaa ya kuvutia sana kuanzia huduma za jamii (umeme, maji, afya na elimu), miundombinu, mazingira na ujenzi wa mji unaokuwa kwa kasi ,
hali hii pia imechochewa na kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami inayounganisha Dodoma na iringa,
Ambapo kwa sasa kanda ya ziwa na kaskazini zimeunganishwa na nyanda za huu kusini na kupelekea kufunguka fursa zaidi za kibiashara.
Kwa sasa iringa ni HUB.
Pamoja na mengine mengi,
Nihitimishe kwa kupongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na pia Hongera sana ndugu zangu wana iringa, ongezeni juhudi,
Asanteni sana.
Sio kweli mkuu, ni vile tu limekaa vinywani mwa watu but once u ask anyone to justify, hakuna anaeweza, lakini pia hilo limekaa kiutani zaidi na Mimi binafsi sioni tatizo katika hilo..hujamaliza kuipamba vizuri vipi watu wake hehe pipo kwa ujumla,naomba kuuliza hivi ni kweli rate ya kujinyonga huko ni kubwa au ni story
Nashukuru mkuu barbosa, yapo mengi ya kujivunia kuhusu iringa, binafsi nikizeeka nitarudi iringa,Napenda Iringa, ndiyo mji mzuri na niupendao kuliko yote Tanzania, umesahau jiwe la Gangilonga nilishapanda mara nyingi tu hadi juu!
Long live Iringa, my home of Choice, Nitarudi Iringa Mungu akipenda!
Nashukuru mkuu barbosa, yapo mengi ya kujivunia kuhusu iringa, binafsi nikizeeka nitarudi iringa,
To me This is the best town in Tz.
Picha zangu haziko vizuri ila kama unazo tuletee, ni faraja sana kuona picha za mji wa iringa.
Hahaha, ukishakula na kuchimba dawa pale kitonga chini, gari ikianza kupanda ule mlima dereva huzima AC unakuwa huru kufungua kioo.Kilichofurahisha zaidi kuhusu Iringa ni ukiwa unatoka Dar au hata Moro ukianza Milima ya Kitonga na kufika juu unaona watu wanaanza kupekuwa Masweta, mara ya kwanza nilivyokwenda Iringa nilishangaa sana, lile badiliko la hali ya hewa kwa maana unaona kabisa Dar, Moro joto la kufa mtu lkn ukifika kileleni tu Kitonga unaanza kutafuta sweta!
Mleta uzi hajakuelewa mtafsirieBhee Mwagito...Wiwonga nyoni...imatawa ga vanu na imikoa gaitamilwa na ierufi ngomiiii
iringa Iringa
kleruu Kleruu
mkwawa Mkwawa
kilolo. Kilolo
Wivu kontenaMkuu naomba sifau au mapungufu ya wanawake wa kihehe maana naona 98% nahisi nitakuja kuoa mhehe
Mkuu mm ni mnyalu na sijui hii dhana inatokana na nini... Kama ingekuwa na uhalisia kila siku tungekuwa tunasikia watu hadi 10 wanajinyonga kwa siku! Lkn hakuna!hujamaliza kuipamba vizuri vipi watu wake hehe pipo kwa ujumla,naomba kuuliza hivi ni kweli rate ya kujinyonga huko ni kubwa au ni story
Ni wavumilivu sana.... Hutajuta kuwa na mke mnyalu.... Japo mm nataka nioe mchagaMkuu naomba sifau au mapungufu ya wanawake wa kihehe maana naona 98% nahisi nitakuja kuoa mhehe