TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Hakika hiki ndicho chama cha mapinduzi ninachokifahamu. Kipo kila sehemu na viongozi wake wanawajibika..kuanzia kwenye Chama Chanyewe mpaka kwa jumuiya zake. Jana tumepata taarifa juu ya muendelezo wa ziara za Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi katika mikoa ya Lindi na Mtwara ambapo kutokana na ziara hiyo Katibu wa Chadema wa Wilaya ya Tandahimba alijiunga na CCM.
Leo viongozi wa Chama, katibu wa Uenezi ndg Nape yupo Nyamagana mwanza kumpokea aliyekuwa kiongozi wa Chadema na Rais wa Chuo kikuu cha SAUT Ndg Dova Mcheshi.
Wakati hayo yakiendelea Naibu Katibu Mkuu bara ndugu Mwigulu nchemba yeye yupo katika mkutano wa Hadhara katika Mji wa Morogoro.
Lakini pia viongozi wa jumuiya ya Vijana hawako nyuma kwani Makamu Mwenyekiti wa UVCCM ndg Mboni Mhita alikuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika jiji la Arusha na Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi wa jumuiya hiyo Ndg Makonda Paul yupo Mkoani Geita akihutubia umma wa watanzania kuwaeleza wananchi hatua iliyofikiwa na CCM katika kuisimamia Serikali katika utekelezaji wa Ilani yake.
Kama hiyo haitoshi nae Mbunge wa Chalinze Ndugu Ridhwan Kikwete yupo Mkoani Morogoro akizungumza na wanavyuo wa mkoa huo.
Hii ndio CCM, najua ikifika 2015 watasema kuna makontena ya kura yameingizwa kutokea Rwanda. Hawa jamaa sometimes hawako serious kabisa..kuna ombwe kubwa la uongozi katika vyama vya upinzani hapa nchini.
Leo viongozi wa Chama, katibu wa Uenezi ndg Nape yupo Nyamagana mwanza kumpokea aliyekuwa kiongozi wa Chadema na Rais wa Chuo kikuu cha SAUT Ndg Dova Mcheshi.
Wakati hayo yakiendelea Naibu Katibu Mkuu bara ndugu Mwigulu nchemba yeye yupo katika mkutano wa Hadhara katika Mji wa Morogoro.
Lakini pia viongozi wa jumuiya ya Vijana hawako nyuma kwani Makamu Mwenyekiti wa UVCCM ndg Mboni Mhita alikuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika jiji la Arusha na Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi wa jumuiya hiyo Ndg Makonda Paul yupo Mkoani Geita akihutubia umma wa watanzania kuwaeleza wananchi hatua iliyofikiwa na CCM katika kuisimamia Serikali katika utekelezaji wa Ilani yake.
Kama hiyo haitoshi nae Mbunge wa Chalinze Ndugu Ridhwan Kikwete yupo Mkoani Morogoro akizungumza na wanavyuo wa mkoa huo.
Hii ndio CCM, najua ikifika 2015 watasema kuna makontena ya kura yameingizwa kutokea Rwanda. Hawa jamaa sometimes hawako serious kabisa..kuna ombwe kubwa la uongozi katika vyama vya upinzani hapa nchini.