KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Hayo maneno manee ya kwanza katika kichwa cha mada hii sio mageni kwetu, na wala sitopenda kuyaandikia kwa kirefu juu yake.
Haya manne niliyoongeza mimi, hata kama yanafanana na yale ya mwanzo, yanatofauti yake.
Kama ni kweli hii nchi "ilichezewa sana"; tulipoyasikia hayo maneno tulielewa nini?
Ni kweli hii nchi ilichezewa sana, na nani? Kuhusu nini? Nini kilifanyika tuache kuchezewa?
Hiyo ilikuwa ni wakati huo.
Sasa tena tunauliza: Hii nchi itachezewa sana?
Kwa nini tukubali kuchezewa tena, wakati tulishasema, tuliwahi kuchezewa!
Kama hatukubali kuchezewa tena, tumejiandaa vipi ili tusichezewe tena?
Au hatuamini kuwa kama nchi tuliwahi kuchezewa; ilikuwa ni uongo tu wa mtu mmoja hata kama alikuwa ni kiongozi?
Tunayo hakika gani kwamba kiongozi wa sasa anajua anayofanya, na kwamba atahakikisha nchi hii haichezewi tena?
Na tukibaini kwamba tunachezewa tena, tunazo njia za kujinasua na kuchezewa huko?
Haya manne niliyoongeza mimi, hata kama yanafanana na yale ya mwanzo, yanatofauti yake.
Kama ni kweli hii nchi "ilichezewa sana"; tulipoyasikia hayo maneno tulielewa nini?
Ni kweli hii nchi ilichezewa sana, na nani? Kuhusu nini? Nini kilifanyika tuache kuchezewa?
Hiyo ilikuwa ni wakati huo.
Sasa tena tunauliza: Hii nchi itachezewa sana?
Kwa nini tukubali kuchezewa tena, wakati tulishasema, tuliwahi kuchezewa!
Kama hatukubali kuchezewa tena, tumejiandaa vipi ili tusichezewe tena?
Au hatuamini kuwa kama nchi tuliwahi kuchezewa; ilikuwa ni uongo tu wa mtu mmoja hata kama alikuwa ni kiongozi?
Tunayo hakika gani kwamba kiongozi wa sasa anajua anayofanya, na kwamba atahakikisha nchi hii haichezewi tena?
Na tukibaini kwamba tunachezewa tena, tunazo njia za kujinasua na kuchezewa huko?