Hii miradi inayotekelezwa kwa maagizo kutoka juu bila bajeti kupitia bungeni, ipo siku itamfunga mtu jela

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Believe me or not, huu utaratibu mpya wa kuanzisha miradi mikubwa na ya mapesa mengi bila kupitia taratibu zilizozoeleka kwa sababu mtu katiba inatoa mwanya huo, kimsingi mambo kama haya hua na mapungufu makubwa sana. Ukianza kufuatilia utakuta matumizi ya pesa zinazotengwa hayaendani na miradi.

Walioanzisha mabunge walikua na maana zao, hii ndio kila mara bajeti nyingi zinapojadiliwa huzuka mabishano makubwa sana baina ya wabunge kukiwa na maana ya kuwepo kwa mapungufu makubwa ndani ya bajeti hizo.Sasa kama mradi unatekelezwa kwa bajeti zilizotengwa kwa maagizo hali itakuaje?

Sasa bunge linapokwepwa na miradi mikubwa inatekelezwa pasipo kulihusisha tufahamu kua lazima kuwepo na mapungufu makubwa tuu, tukumbuke usemi usemao kua "Mali bila daftari hutumika bila habari". Tu nafikiri kufanya hili ni kulisaidia taifa kumbe ni kujitengenezea mazingira ya kulitia hasara. Huwezi kufanya mradi unaochukua muda mrefu kukamilika au usiohitajika kwa haraka kama kitu cha Emergency, hiki kitu si cha kawaida. Hivi ununuzi wa bombardier ni Emergency? Kwenye majanga hata sheria inaruhusu pesa kutolewa kwa emergency ingawa nako kuna taratibu zake.

Nasema ipo siku hawa wanayoyafanya haya watakutwa na hatia za matumizi mabaya ya ofisi au ufisadi. Tunayafurahia haya kwa vile uwezo wetu wa kuhoji huenda unatia mashaka lakini utafika muda haya mambo yatamlaza mtu jela bila kujali umri alionao kwa sababu sheria na vifungu vyake viko wazi. Kutekeleza mambo nje na taratibu za kisheria kwa sababu tu sasa ni zama zingine, ipo siku zama zingine zitafuta sheria katika kufuatilia kama zamazingine nazo zilifuata sheria.
 
Labda wanajiona wana akili kuliko wabunge wote na hasa wa ccm ambao ndiyo wengi
 
Orodhesha hapa mirad iliyoanzishwa bila itaratib halaf utuletee na bajet ya wizara husika yuangalie ili tuhukum kwa haki,,unaweza kua sahihi ila binafs kama mrad una tija siwez ona ajab kuanzishwa
 
Believe me or not, huu utaratibu mpya wa kuanzisha miradi mikubwa na ya mapesa mengi bila kupitia taratibu zilizozoeleka kwa sababu mtu katiba inatoa mwanya huo, kimsingi mambo kama haya hua na mapungufu makubwa sana. Ukianza kufuatilia utakuta matumizi ya pesa zinazotengwa hayaendani na miradi.

Walioanzisha mabunge walikua na maana zao, hii ndio kila mara bajeti nyingi zinapojadiliwa huzuka mabishano makubwa sana baina ya wabunge kukiwa na maana ya kuwepo kwa mapungufu makubwa ndani ya bajeti hizo.Sasa kama mradi unatekelezwa kwa bajeti zilizotengwa kwa maagizo hali itakuaje?

Sasa bunge linapokwepwa na miradi mikubwa inatekelezwa pasipo kulihusisha tufahamu kua lazima kuwepo na mapungufu makubwa tuu, tukumbuke usemi usemao kua "Mali bila daftari hutumika bila habari". Tu nafikiri kufanya hili ni kulisaidia taifa kumbe ni kujitengenezea mazingira ya kulitia hasara. Huwezi kufanya mradi unaochukua muda mrefu kukamilika au usiohitajika kwa haraka kama kitu cha Emergency, hiki kitu si cha kawaida. Hivi ununuzi wa bombardier ni Emergency? Kwenye majanga hata sheria inaruhusu pesa kutolewa kwa emergency ingawa nako kuna taratibu zake.

Nasema ipo siku hawa wanayoyafanya haya watakutwa na hatia za matumizi mabaya ya ofisi au ufisadi. Tunayafurahia haya kwa vile uwezo wetu wa kuhoji huenda unatia mashaka lakini utafika muda haya mambo yatamlaza mtu jela bila kujali umri alionao kwa sababu sheria na vifungu vyake viko wazi. Kutekeleza mambo nje na taratibu za kisheria kwa sababu tu sasa ni zama zingine, ipo siku zama zingine zitafuta sheria katika kufuatilia kama zamazingine nazo zilifuata sheria.
Lazima afungwe na achapwe fimbo za kutosha kwenye makalio yake....imagine mtu anachukua hela za serikali Bil.140 kukomboa ndege kwa hasara aliyoisababisha mwenyewe kwa ujinga wake!
 
Orodhesha hapa mirad iliyoanzishwa bila itaratib halaf utuletee na bajet ya wizara husika yuangalie ili tuhukum kwa haki,,unaweza kua sahihi ila binafs kama mrad una tija siwez ona ajab kuanzishwa
Akiorodhesha nitag mkuu tafadhari.
 
Kwaiyo haina tija kwa taifa? Na orodhesha miradi imepangiwa na pesa azikufika na kwa kiasi gani kwa kila mradi tafadhari.
mkuu.. Ulisema uorodheshewe sasa umeongeza maswali tena? Kwani wewe unaishi nje ya nchi, hapa mtaani kwangu kuna mradi mkubwa tu wa maji lakini umefia katikati, kuna mradi mkubwa wa uzalishaji umeme kwa kutumia upepo nao umefia njiani! Haya yote hayajafanyika ni kwa sababu tumepeleka hela kwenye visivyo na tija kama bomberdie, usiniumize kichwa!
 
Lazima afungwe na achapwe fimbo za kutosha kwenye makalio yake....imagine mtu anachukua hela za serikali Bil.140 kukomboa ndege kwa hasara aliyoisababisha mwenyewe kwa ujinga wake!
Una Risiti ya hizo bilioni 140?
 
Back
Top Bottom