Nyoka wa kijani hangati kutokana na maumbile ya meno yake, hana meno kwa mbele, meno yake yameanzia katikati ya taya, hivyo kungata mpaka umkanyage na ahangaike kutoka
Nyoka wa kijani hawanaga madhara,unaweza lala nae ktandani,tuliwah ishi mahala walkuwa weng sana lakin hawakuwah kuleta madhara mwanzo tuliwauwa sana kwa sku tulkuwa tunaua watatu mpaka watano,jamaa mmoja akatueleza kuwa waacheni tu hawana shida mpaka Leo Mimi kama nyoka hayupo ndani hata kama ni wale weusi siwezi kumuua ni dhambi pale hajafanya kosa lolote why umuue
Wakuu hapa naona umeseleleka na mazoea.
Ni kweli Kuna nyoka wa kijani wasio na madhara (Green Grass Snakes, Green Rough Scale snakes na Green Snakes) Hawa unaweza hata kucheza nao lakini don't take a chance Kama huwezi kuwatambua nyoka kwa muonekano wao na sio rangi yao peke yake.
Kuna nyoka wa kijani wenye madhara Kama Boomslang na Green Mamba Hawa usijaribu kunyoosha mkono uwashike na uzuri au ubaya wao mbinu yao ni moja "Wait and see" kifupi patience ni silaha yao.
Green Mamba akikung'ata huna hata saa ya kuishi Kama utakosa msaada, sumu yake huathiri mfumo wa fahamu na moyo. Na kwa faida ya watu wa pwani Green Mamba wanapatikana Sana pwani ,Tanga, Dar es Salaam, Morogoro mtwara na Lindi.
Boomslang ni mpole na watu huzani hana madhara lakini katika nyoka wa kijani mwenye sumu Kali na yeye yumo akikuuma unaweza pitisha masaa bila kuona madhara na hapa wengi wamekufa pasipo kujua kwasababu ya kupuuzia. Sumu yake huathiri mfumo mzima wa damu.
Ukimsogelea Green Mamba Kama yupo Chini husimama hii ni ishara ya mapambano na Kama akiamua kukufukuza hufiki mbali.
Ukimsogelea Boomslang hutengeneza umbo "S" tayari kuattack yeye Hana tabia ya kufukuza. All in all kama huwezi kuwatambua chukua tahadhari, binafsi naweza kuwatambua but I never take a chance to belittle them.
Chizi Maarifa
Nyoka ni ngumu kupambana nao lakini unaweza ukachukua hatua chache wasifanye makazi yako kuwa makazi yao.
👉Mosi hakikisha ujenzi wa nyumba yako umezuia penyo kwa nyoka kuingia ndani ya nyumba hapa namaanisha milango na madirisha yawe well fitted
👉Hakikisha chemba za maji machafu zimefunikwa na mifuniko sawasawa bila kuacha nafasi
👉Fukuza au ondoa upatikanaji wa chakula Cha nyoka Kama vyura, mijusi,konokono,vinyonga,panya etc
👉Ondoa maficho ya nyoka Kama mashimo, nyufa, na pia nyoka hupenda kukaa kwenye sehemu zenye giza vivuli vizito na zenye unyevu
👉Fuga mifugo inayokula nyoka Kama Turkey (Bata mzinga) Nguruwe (Samahani Kama nimekukwaza kiimani) na Guinea Hens (Hawa nadhani ni Kanga)
👉Kuna harufu nyoka huwa hawapendi na moja ya harufu wasiyoipenda ni Moshi was Moto Kama mapira so you can smoke them out hili hufanyi kwa siku moja yawezakua wiki nzima Moshi haukati
👉Panda mimea inayofukuza nyoka Kama Michaichai kuanzia getini
👉 Landscaping, fyeka majani na epuka vichaka nyumbani
👉Chunguza fence yako kwa ndani na kwa nje Kama Kuna mashimo na nyufa ziba.
Mengine ni expensive Kama kuspray mafuta ya karafuu na mdalasini kwa wakati moja.
Salaam.