BABA JUICE
JF-Expert Member
- Sep 5, 2010
- 426
- 52
Kuna ndugu yangu kaibiwa kaenda polisi(osterbay) kufungua file wamemtoza shillingi elfu 30 ya kufungulia file police watatu kumkamata mualifu akatoa elfu 60, na akalipia na tax shilingi elfu 25 na eti pingu hazikai kituoni hadi kwenye kotazi zao, garama yote ni shilingi 115,000/= nikajiuliza hawa polisi hawana mishaara au mishahara yao ni midogo sana....na bado wamemfanya ndugu yangu huyu mradi wanampigia simu wanaomba pesa za kumfuatilia huyo mwizi kwani hadi muda huu naandika habari hii mwizi mwenyewe hajakamatwa.....kwakweli sielewi kazi za polisi na garama zao kwani mi najua polisi ni huduma.....hata file la kesi mahakamani hufungui kwa elfu 30. Nielimisheni wanajamii....TUJENGE PAMOJA.