SuperImpressor
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 1,505
- 649
Hii kwa M-Pesa MasterCard Nitaiita LoopHole
Kama mnavyojua kampuni ya Vodacom wametuletea huduma nzuri ya kutuwezesha kufanya manunuzi mtandaoni kupitia huduma yao ya M-Pesa Virtual Card ambayo inapatika kupitia USSD *150*00# ambayo ni menu ya Vodacom M-Pesa. Tukumbuke kwamba taarifa za kadi hii zinatakiwa kuwa siri ya mtumiaji tu ili kuiepusha kadi yake kutumiwa na mtu mwingine kufanya miamala. Lakini sasa cha kushangaza ni kwamba hii M-Pesa Mastercard ambayo ni msaada kwetu, iko “UCHI” (NAKED) kwa sababu unapoingia katika menu ya M-Pesa, 4 Lipa kwa M-Pesa, 6 M-Pesa Mastercard, 2 Taarifa za Kadi, utatumiwa taarifa zako za kadi hadi ile CVV bila hata kuombwa namba za siri na hiyo itampa nafasi mtu mbaya kuona taarifa za kadi.
Swali langu ni kwamba hawa jamaa hawajaona kuwa huo ni mwanya unaoweza kumsababishia mteja wao hasara?
Kama mnavyojua kampuni ya Vodacom wametuletea huduma nzuri ya kutuwezesha kufanya manunuzi mtandaoni kupitia huduma yao ya M-Pesa Virtual Card ambayo inapatika kupitia USSD *150*00# ambayo ni menu ya Vodacom M-Pesa. Tukumbuke kwamba taarifa za kadi hii zinatakiwa kuwa siri ya mtumiaji tu ili kuiepusha kadi yake kutumiwa na mtu mwingine kufanya miamala. Lakini sasa cha kushangaza ni kwamba hii M-Pesa Mastercard ambayo ni msaada kwetu, iko “UCHI” (NAKED) kwa sababu unapoingia katika menu ya M-Pesa, 4 Lipa kwa M-Pesa, 6 M-Pesa Mastercard, 2 Taarifa za Kadi, utatumiwa taarifa zako za kadi hadi ile CVV bila hata kuombwa namba za siri na hiyo itampa nafasi mtu mbaya kuona taarifa za kadi.
Swali langu ni kwamba hawa jamaa hawajaona kuwa huo ni mwanya unaoweza kumsababishia mteja wao hasara?