Lighton
JF-Expert Member
- Aug 5, 2019
- 881
- 1,636
Hakuna kitu ambacho huwa kinaniumiza sana kama hiki. Yaani huwa naumia sana, moyo wangu huwa na huruma sana ninapoona kuna mtu anaumia moyo kwaajili yangu na kwa namna yoyote huwa najitahidi kuwa sehemu ya furaha kwa wale wanipendao.
Lakini nina madhaifu yangu pia. Sina moyo uliopondeka, siwezi kuvumilia kuona mwanamke ananipenda but at the same time anampenda zaidi mwanaume mwingine yaan bora hata asingenipenda na asinipende ndo atazidi kuniumiza.
Inafikia hatua nafikiria kuishi kihuni tu, yaan nafikiri ningekuwa nafurahi tu kupitia maumivu ya wengine. Ile ile tu yaani hata kwa wanaonipenda ni kupiga tu na kutembea. Nafikir nikiishi maisha haya nitakuwa na furaha sana.
Nina msichana ambaye upendo wake kwangu ulinifanya niamini she was the one forever, i believed that she was my Eternal. Anasema ananipenda, alinipenda na atazidi kunipenda lakini Kuna mtu ambaye anampenda zaidi yangu na ni mwanaume wa maisha yake, wamecherish vingi sana.
Haya ni maneno ambayo yameshasemwa na karibia wanawake wawili ambao nimewah kukutana nao kwenye maisha yangu ya mahusiano ambao wamewahi kunionyesha upendo ambao ulinifanya nijione ni wa pekee lakini kilichokuja kutokea baadae ni maumivu makubwa.
Nawaza na najuta kuwa mwema, kuwa na upendo wa dhati kwa mwanamke anayetumia wakati wake wa shida kujiliwaza kwangu.
Haya ni maumivu yenye mafunzo makubwa sana kwenye maisha yangu ya mahusiano. Najua mimi ni binadamu nimeumbwa kusahau, lakini sitaweka kipaombele mawazo ya kuwa dhaifu kama binadamu...... Yataniumiza sana.
Haya ndiyo yanayonikuta sasa.
Nawasilisha kwa huzuni sana
Lakini nina madhaifu yangu pia. Sina moyo uliopondeka, siwezi kuvumilia kuona mwanamke ananipenda but at the same time anampenda zaidi mwanaume mwingine yaan bora hata asingenipenda na asinipende ndo atazidi kuniumiza.
Inafikia hatua nafikiria kuishi kihuni tu, yaan nafikiri ningekuwa nafurahi tu kupitia maumivu ya wengine. Ile ile tu yaani hata kwa wanaonipenda ni kupiga tu na kutembea. Nafikir nikiishi maisha haya nitakuwa na furaha sana.
Nina msichana ambaye upendo wake kwangu ulinifanya niamini she was the one forever, i believed that she was my Eternal. Anasema ananipenda, alinipenda na atazidi kunipenda lakini Kuna mtu ambaye anampenda zaidi yangu na ni mwanaume wa maisha yake, wamecherish vingi sana.
Haya ni maneno ambayo yameshasemwa na karibia wanawake wawili ambao nimewah kukutana nao kwenye maisha yangu ya mahusiano ambao wamewahi kunionyesha upendo ambao ulinifanya nijione ni wa pekee lakini kilichokuja kutokea baadae ni maumivu makubwa.
Nawaza na najuta kuwa mwema, kuwa na upendo wa dhati kwa mwanamke anayetumia wakati wake wa shida kujiliwaza kwangu.
Haya ni maumivu yenye mafunzo makubwa sana kwenye maisha yangu ya mahusiano. Najua mimi ni binadamu nimeumbwa kusahau, lakini sitaweka kipaombele mawazo ya kuwa dhaifu kama binadamu...... Yataniumiza sana.
Haya ndiyo yanayonikuta sasa.
Nawasilisha kwa huzuni sana