Hili swala la adhabu watu wa haki za binadamu wameingilia na kulipigia kelele sana, Imefika mahali hawataki watoto waende shule na fagio na makopo ya kumwagia maji maua.
Swali la kujiuliza, Je nani atafanya usafi mazingira ya shule? Mtoto atajuaje umuhimu wa kufanya usafi wa kwake binafsi na mazingira kwa ujumla? Unakuta jumatatu na alhamis mtoto shati chafu utadhani hatoki nyumbani.\
Shule yenyewe inakuwa Tandale shule ya msingi au Shule ya msingi Mtongani, Hiyo Ada mzazi matatizo, mchango wa mlinzi wa shule mbinde kuchangia.
Sembuse Kuweka kampuni ya ufagizi shuleni kama shule za Watakatifu.
Wanahakati wa haki za binadamu sijui wanatupeleka wapi katika hili?