Midazolam
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 806
- 1,337
Moja kwa Moja kwenye mada.mimi ni mkristo na muumini mzuri tu katika maisha yangu.
Nimekuwa na hii hali na imekuwa inajirudia sana ninapokuwa msafi wa rohoni na huwa ninapoomba sana.
Nimekuwa nikienda kununua kitu dukani basi nitatoa ela na kununua bidhaa,ila Cha ajabu nitarudishiwa ela nyingi au juu zaidi,
Mfano juzi nilienda kunyoa nywele saluni nikatoa elfu kumi nikampa kinyozi nikamwambia kata elfu nne yako ,kinyozi akanirudishia elfu kumi na mbili nikamwambia aisee mbona umenirudishia kibao,nikachukua elfu sita nikamrudishia Ile ela yake iliyozidi
Jioni nikaenda dukani kunununua maji Huwa nachukua kwa dazani kwa ajili ya kuweka ndani,akaniambia jumla unatakiwa kulipa kumi na mbili na mia mbili nikampa elfu 20,Cha ajabu amenirudishia tena kama elfu kumi na nane.nikamwambia dada umenizidishia ela,akashukuru sana ,kwenye hiyo duka ni kama mara mbili ,akasema aisee kaka una roho nzuri mdogo wangu pia aliwahi kukuzidishia ela ila kwa uaminifu wako ulimrudishia nikamwambia sitaki kula ela ambayo si jasho langu.
Huku kazini siku iliyofuata nikaenda kununua chakula Cha elfu tatu maeneo ya hapa hapa kazini,yule kaka naye akajichanganya akanirudishia tena ela iliyozidi nilimpa elfu Tano akanirudishia elfu nane ,kwa kweli hii sikurudisha Mungu anisamehee,
Swali nafanya vizuri kurudisha hizi ela au makosa ? Wajuzi wa haya mambo nisaidieni nijue.
Nb hii hali hata nikipanda daladala nimekuwa na bahati ya kutoombwa ela na konda ,atanipita tu kama hanioni vile ila Kuna mda nafsi inanisuta nachukua ela na kulipa.
Nimekuwa na hii hali na imekuwa inajirudia sana ninapokuwa msafi wa rohoni na huwa ninapoomba sana.
Nimekuwa nikienda kununua kitu dukani basi nitatoa ela na kununua bidhaa,ila Cha ajabu nitarudishiwa ela nyingi au juu zaidi,
Mfano juzi nilienda kunyoa nywele saluni nikatoa elfu kumi nikampa kinyozi nikamwambia kata elfu nne yako ,kinyozi akanirudishia elfu kumi na mbili nikamwambia aisee mbona umenirudishia kibao,nikachukua elfu sita nikamrudishia Ile ela yake iliyozidi
Jioni nikaenda dukani kunununua maji Huwa nachukua kwa dazani kwa ajili ya kuweka ndani,akaniambia jumla unatakiwa kulipa kumi na mbili na mia mbili nikampa elfu 20,Cha ajabu amenirudishia tena kama elfu kumi na nane.nikamwambia dada umenizidishia ela,akashukuru sana ,kwenye hiyo duka ni kama mara mbili ,akasema aisee kaka una roho nzuri mdogo wangu pia aliwahi kukuzidishia ela ila kwa uaminifu wako ulimrudishia nikamwambia sitaki kula ela ambayo si jasho langu.
Huku kazini siku iliyofuata nikaenda kununua chakula Cha elfu tatu maeneo ya hapa hapa kazini,yule kaka naye akajichanganya akanirudishia tena ela iliyozidi nilimpa elfu Tano akanirudishia elfu nane ,kwa kweli hii sikurudisha Mungu anisamehee,
Swali nafanya vizuri kurudisha hizi ela au makosa ? Wajuzi wa haya mambo nisaidieni nijue.
Nb hii hali hata nikipanda daladala nimekuwa na bahati ya kutoombwa ela na konda ,atanipita tu kama hanioni vile ila Kuna mda nafsi inanisuta nachukua ela na kulipa.