HESLB jipangeni mapema, mwaka huu hatutaki visingizio

HESLB jipangeni mapema, mwaka huu hatutaki visingizio

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
14,192
Reaction score
19,118
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na TCU, majina ya wanafunzi watakaokuwa wamedahiliwa katika vyuo vikuu mbalimbali yatatoka rasmi tarehe 2/10/2017. Lakini vyuo vitafunguliwa tarehe 30/10/2017.

Hivyo bodi ya mikopo watakuwa na mwezi mzima wa kufanya zoezi la kuchakata upangaji wa mikopo kwa waombaji wa mikopo hiyo. Kitu ambacho hatutaki kusikia ni kuona mpaka vyuo vinafunguliwa na mikopo kwa waliopata kuwa bado haijawa tayari.

Tunataka mwanafunzi atakapofungua chuo, pesa zake za mkopo ziwe tayari zipo na akitoa akaunti yake tayari aweze kuingiziwa pesa zake. Wahusika wote washughulike sasa. Kama ni wizara ya fedha au hazina, basi waanze kujipanga sasa, siyo wasubiri kusukumwa na maandamano ya wanafunzi pale UDSM.

Hilo tumelichoka. Ambaye atakuwa amekosa mkopo, basi ajue mapema aamue kusuka au kunyoa mapema. Siyo kumwacha mtu amesharipoti chuoni na kisha kuambiwa hajapata mkopo. Au mtu anaambiwa amepata mkopo lakini anakaa zaidi ya mwezi mzima akiwa hajaingiziwa pesa zake kwenye akaunti. Tumetoa ilani mapema!
 
First year mnajifanya wajuaji kweli!!
Kama umekaa tu home unasubiri Kula Kulala Kwa Mama hutafuti hela ya kuanzia maisha chuo subiri uone!!

Unatishia hela yenyewe ya mkopo??
Niaje we chali angu??
 
First year mnajifanya wajuaji kweli!!
Kama umekaa tu home unasubiri Kula Kulala Kwa Mama hutafuti hela ya kuanzia maisha chuo subiri uone!!

Unatishia hela yenyewe ya mkopo??
Niaje we chali angu??
We kama hauko concerned wqachie wenyewe.
 
We kama hauko concerned wqachie wenyewe.
Hapa unaelekezwa tu hata kama hutaki!!
Hakuna chuo utafungua leo upeleke account number kesho uingiziwe mzigo!!
Zimekuwa njugu hizo!!
Kuna taratibu ambazo huwa zinachukua muda kidogo.....
 
Hapa unaelekezwa tu hata kama hutaki!!
Hakuna chuo utafungua leo upeleke account number kesho uingiziwe mzigo!!
Zimekuwa njugu hizo!!
Kuna taratibu ambazo huwa zinachukua muda kidogo.....
Selection itatoka tarehe mbili octoba. Vyuo vinafunguliwa tarehe thelathini oktoba. Kuna mwezi mzima wa kufanya mchakato wote ukamilike kabla ya vyuo kufunguliwa. Hivyo visingizio havikubaliki. Vyuo vinapofunguliwa hela iwe tayari kabisa, ubaki mchakato wa wanafunzi kusaini na kuingiziwa pesa. Hilo zoezi la kusaini na kuingiziwa pesa haliwezi kuchukua hata wiki moja. Visingizio vyote mwisho Chalinze!
 
kwangu naona angalau mpaka oktoba 15 bodi ingekuwa imeshatoa orodha ya wanufaika wa bodi ya mkopo waliopata. kitendo cha mwanafunzi kwenda chuoni bila kujua kama amepata mkopo au lah sio sawa.
 
Hapa unaelekezwa tu hata kama hutaki!!
Hakuna chuo utafungua leo upeleke account number kesho uingiziwe mzigo!!
Zimekuwa njugu hizo!!
Kuna taratibu ambazo huwa zinachukua muda kidogo.....
Mwambie huyo chariiiiiiii
 
Selection itatoka tarehe mbili octoba. Vyuo vinafunguliwa tarehe thelathini oktoba. Kuna mwezi mzima wa kufanya mchakato wote ukamilike kabla ya vyuo kufunguliwa. Hivyo visingizio havikubaliki. Vyuo vinapofunguliwa hela iwe tayari kabisa, ubaki mchakato wa wanafunzi kusaini na kuingiziwa pesa. Hilo zoezi la kusaini na kuingiziwa pesa haliwezi kuchukua hata wiki moja. Visingizio vyote mwisho Chalinze!
Mdogo wangu naona unaongea vitu huvijui au kama unavijua basi kwa maksudi unajitoa fahamu!
Unajua first huwa mnafika hamna hata account ya bank?
Au unafikiri ukifika ukatoa account namna yako basi wewe peke yako unaingiziwa pesa?
Uingiziwe pesa hata orientation hujamaliza!!!
Wacha ujuha we Dogo eboooo!
 
Back
Top Bottom