HESLB acheni uonevu

HESLB acheni uonevu

Enzymes

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2013
Posts
4,332
Reaction score
3,018
Hii Board ya Mikopo nchini ina kasoro nyingi sana;

1. Ina toza watu riba ambazo hazikuwa kwenye mkataba wa makubaliano (fomu) miaka ya 2009 hadi 1994.
Huu ni wizi!

2. Riba zenyewe ni 5% each day the amount remains outstanding! Hiyo ni retention fee tu. Tena kuna interest ya 5% tena! Huu ni wizi mtupu. Mlimkopesha kashindwa kupata 7m za kujisomesha, wazazi wake hawana hata nyumba. Huyu mtu kwa lugha nyingine ni maskini.
Afu nyie mnakuja na deni la 18M from 7M. Hata CRDB ni mabepari lakini hawako hivyo! Kwa style hii tukutane Mahakamani tu. Liwalo na liwe (Pinda, 2014).

3. Katika sheria za kodi, kipa umbele ni madeni ya TRA. Sasa nyie mna nidai 18M na marafiki zangu nao wana nidai ndogo tu 2M. Inakuweje nyie mnipe siku 30 wakati nina madeni mengi? Mlinipa muda wa ku adjust matumizi na malipo yangu? Je kama nina mkopo CRDB na wanakata 700,000? Na nyie nijisalimishe mkate 300,000 nile majani eti eeh??? TRA wakate 400,000++; NSSF wakate 200,000+++

Mtoe muda wa kuadjust. Muanze January.

4. Kwanza board hii haina data. Majina yaliyotolewa yanajumisha hata ambao tiyari washalipa na wanao lipa!

5. Tunataka ufafanuzi wa hizi riba zenu. Tunakomoana au? Au enzi za JK mlipiga hela sasa mnatafuta sehemu ya kuzibia mashimo?

6. Zamani tulikuwa tuna andamana sisi kuomba mtulipe. Kama hamtaki iwe zamu yenu kuandamana tuwalipe. Tengenezeni mazingira rafiki ya mikopo kulipika kwa urahisi na kwa unafuu. Isiwe kama kukomoana!
Mf. Ondoeni riba, pili makato ya 15% ni ya kipuuzi (wengi wa Wabunge waliopitisha sheria hii hawadaiwi mikopo). Wabunge hawa huwalipia watoto wao bila ya mikopo.

PAYE- 30%
NSSF-10%
HESLB-15%
NHIF-3% TOTAL 58% Hii kazi nawafanyia nyie au?

Subsidies kwenye elimu ni mhimu. Msitake kufanya biashara na wanafunzi tena watoto wa maskini kwa kuwatoza Riba!! Mkubali tu kuondoa riba iwe kama ruzuku ktk Elimu. Hawaliokopeshwa na Maskini!

7. Hivi mna data za Interval ya kupata ajira Tz? Mmetengeneza mazingira ya ajira Tz? Mf. Mtu alihitimu 2009 lakini kazi kapata 2013, iweje riba mmutoze tokea 2011?

Hii nchi watu wengi hufikiria kinyume nyume, ndio maana haiendelei kamwe! Wateule wengi ni wabovu!

Mwambieni Rais Magufuli alivyo semehe wafanyabiashara faini za TRA pia awasamehe watoto wa maskini riba za Elimu.
 
Magereza yajiandae kujaa kwani wasio na uwezo wa kulipa ni wengi. Mfano Mimi tangu nimalize chuo 2007 nipo kitaa naunga unga, hapo jela nje nje na nimesha jiandaa na jela kwani kulipa sina uwezo wala kipato cha uhakika.
 
Magereza yajiandae kujaa kwani wasio na uwezo wa kulipa ni wengi. Mfano Mimi tangu nimalize chuo 2007 nipo kitaa naunga unga, hapo jela nje nje na nimesha jiandaa na jela kwani kulipa sina uwezo wala kipato cha uhakika.
Siyo ww tu mkuu. Watu wapo wengi sana.
Ugumu zaidi umefanywa na hiyo riba
 
Kifupi sielewi tunakwenda wapi? Education is very expensive commodity without cost sharing between government and students or parents its difficult to achieve the goal naona Tanzania ya viwanda ikififia kabisa! Mungu okoa wasomi wa Tanzania!!! Naanza kuwaza yawezekana mkuu hana mpango wa kuendelea kuongoza that's why kila kitu upside down au kuna watu wanamkakati wa kutaka kumuangusha wachumi na policy maker mko wapi?
 
Kifupi sielewi tunakwenda wapi? Education is very expensive commodity without cost sharing between government and students or parents its difficult to achieve the goal naona Tanzania ya viwanda ikififia kabisa! Mungu okoa wasomi wa Tanzania!!! Naanza kuwaza yawezekana mkuu hana mpango wa kuendelea kuongoza that's why kila kitu upside down au kuna watu wanamkakati wa kutaka kumuangusha wachumi na policy maker mko wapi?
Offcourse, and I hope wengi wao hata wataalamu wana muogopa!!

Hivyo yy ndie huwashauri na siyo wataalamu kumshauri Rais.
Ukipingana nae utaonekana Jipu.
Hivi ili watoto waende choo ni lazima wasema kila kitu YES!!
 
Back
Top Bottom