Dkt. Gwajima D
Minister
- Nov 28, 2015
- 1,706
- 8,657
Wasaalam wanajukwaa.
Kuelekea Siku ya Wajane Duniani tarehe 23 Juni 2024, fahamu machache tafadhali 👇🇹🇿
HISTORIA; Siku ya Wajane Duniani huadhimishwa tarehe 23 Juni kila mwaka ambapo, iliasisiwa na Bw. Lord Loomba aliyeanzisha Taasisi ya Loomba mwaka 2005 baada ya baba yake kufariki tarehe 23 Juni mwaka 1954.
UMUHIMU WA SIKU HII: Wajane ni kundi kubwa ambalo, hukabiliwa na changamoto nyingi baada ya kufiwa na wenza wao ikiwemo, wengine kuachwa katika umaskini, kunyimwa haki zao za mirathi kama ardhi, haki za kuwalea watoto na kudhulumiwa mali nyinginezo walizochuma kwa pamoja na wenza wao. Aidha, wajane wengine hufukuzwa nyumbani mwao, hutengwa na kunyanyaswa na ndugu wa mume pamoja na jamii na wengine hulazimishwa kuolewa na ndugu wa marehemu pasipo ridhaa yao huku wengine wakikosa huduma ya utetezi pale wanapotafuta haki zao.
Maadhimisho ya siku ya wajane nchini Tanzania hulenga pia, kukuza hamasa, mshikamano na uelewa ndani ya jamii ili kuacha ukiukwaji wa haki za binadamu kwa wajane. Aidha, maadhimisho haya hutoa fursa ya pamoja kwenye kutambua changamoto za wajane na namna ya kukabiliana nazo. Katika maadhimisho haya, wajane pia hutengeneza kwa upya mtandao unaowapa nafasi ya kupata taarifa mbalimbali zinazohusu fursa za kiuchumi, kijamii na uongozi kwa maendeleo na ustawi. Halikadhalika, siku hii ni muhimu katika kuongeza uhamasishaji wa kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu kwa wajane.
KAULIMBIU 2024. “Imarisha Mifumo ya upatikanaji wa Nishati: Kukuza Uchumi wa Wajane na Familia”.
MAADHIMISHO YANAFANYIKA WAPI? Kila mkoa na wilaya zake kuadhimisha.
_________________
ZIADA YA TAARIFA 👇
Duniani inakadiriwa Wajane ni takriban millioni 258 na kati ya hao, Wajane 115 millioni wanadhulumiwa, wanafanyiwa ukatili, wanakabiliwa na umaskini na kutengwa na jamii.
Tanzania, idadi ya wajane ni 1,396,262 sawa na asilimia 4.5 ya wanawake wote nchini, kwa sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.
Kaulimbiu ya Mwaka huu hapo juu, inaendana na agenda ya Kitaifa inayosisitiza matumizi ya Nishati Safi na Salama ya Kupikia ambapo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Kinara wa Upatikanaji wa Nishati hii Duniani kwa lengo la kupunguza mzigo wa kazi za malezi (unpaid care work) (zisizo na malipo) kwa Wanawake wakiwemo Wajane.
Aidha, Mwongozo wa Benki ya Dunia kuhusu Nishati safi na salama ya kupikia wa mwaka 2020 unasisitiza matumizi ya Nishati Safi na Salama ya kupikia.
Faida za juhudi zote hizi kuwa, hazilengi tu kupunguza mzigo wa kazi kwa wanawake wakiwemo wajane bali pia, kuwapa nafasi ya kujihusisha na shughuli za uzalishaji mali na hivyo kuingiza kipato katika ngazi ya jamii na Taifa na kupunguza uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kiafya.
MWISHO.
Kuelekea Siku ya Wajane Duniani tarehe 23 Juni 2024, fahamu machache tafadhali 👇🇹🇿
HISTORIA; Siku ya Wajane Duniani huadhimishwa tarehe 23 Juni kila mwaka ambapo, iliasisiwa na Bw. Lord Loomba aliyeanzisha Taasisi ya Loomba mwaka 2005 baada ya baba yake kufariki tarehe 23 Juni mwaka 1954.
UMUHIMU WA SIKU HII: Wajane ni kundi kubwa ambalo, hukabiliwa na changamoto nyingi baada ya kufiwa na wenza wao ikiwemo, wengine kuachwa katika umaskini, kunyimwa haki zao za mirathi kama ardhi, haki za kuwalea watoto na kudhulumiwa mali nyinginezo walizochuma kwa pamoja na wenza wao. Aidha, wajane wengine hufukuzwa nyumbani mwao, hutengwa na kunyanyaswa na ndugu wa mume pamoja na jamii na wengine hulazimishwa kuolewa na ndugu wa marehemu pasipo ridhaa yao huku wengine wakikosa huduma ya utetezi pale wanapotafuta haki zao.
Maadhimisho ya siku ya wajane nchini Tanzania hulenga pia, kukuza hamasa, mshikamano na uelewa ndani ya jamii ili kuacha ukiukwaji wa haki za binadamu kwa wajane. Aidha, maadhimisho haya hutoa fursa ya pamoja kwenye kutambua changamoto za wajane na namna ya kukabiliana nazo. Katika maadhimisho haya, wajane pia hutengeneza kwa upya mtandao unaowapa nafasi ya kupata taarifa mbalimbali zinazohusu fursa za kiuchumi, kijamii na uongozi kwa maendeleo na ustawi. Halikadhalika, siku hii ni muhimu katika kuongeza uhamasishaji wa kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu kwa wajane.
KAULIMBIU 2024. “Imarisha Mifumo ya upatikanaji wa Nishati: Kukuza Uchumi wa Wajane na Familia”.
MAADHIMISHO YANAFANYIKA WAPI? Kila mkoa na wilaya zake kuadhimisha.
_________________
ZIADA YA TAARIFA 👇
Duniani inakadiriwa Wajane ni takriban millioni 258 na kati ya hao, Wajane 115 millioni wanadhulumiwa, wanafanyiwa ukatili, wanakabiliwa na umaskini na kutengwa na jamii.
Tanzania, idadi ya wajane ni 1,396,262 sawa na asilimia 4.5 ya wanawake wote nchini, kwa sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.
Kaulimbiu ya Mwaka huu hapo juu, inaendana na agenda ya Kitaifa inayosisitiza matumizi ya Nishati Safi na Salama ya Kupikia ambapo, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Kinara wa Upatikanaji wa Nishati hii Duniani kwa lengo la kupunguza mzigo wa kazi za malezi (unpaid care work) (zisizo na malipo) kwa Wanawake wakiwemo Wajane.
Aidha, Mwongozo wa Benki ya Dunia kuhusu Nishati safi na salama ya kupikia wa mwaka 2020 unasisitiza matumizi ya Nishati Safi na Salama ya kupikia.
Faida za juhudi zote hizi kuwa, hazilengi tu kupunguza mzigo wa kazi kwa wanawake wakiwemo wajane bali pia, kuwapa nafasi ya kujihusisha na shughuli za uzalishaji mali na hivyo kuingiza kipato katika ngazi ya jamii na Taifa na kupunguza uharibifu wa mazingira pamoja na athari za kiafya.
MWISHO.