Baraza la Famasi Tanzania
Member
- Mar 27, 2025
- 33
- 45
Heri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Udhibiti na Usajili wa Dawa upo chini ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba na kwa dawa za asili zinazajiliwa na Baraza la Tiba Asili chini ya Wizara ya Afya ambalo lina wawakilishi kila Mkoa na Wilaya wanaofanya kazi chini ya Ofisi za Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya.Hongera BLFT kwa kuwa wanachama humu jukwaani
Leo tukiazimisha siku ya wafanyakazi Tanzania na duniani je mnamaoni gani na mpango gani juu ya Watanzania wanaobuni na kugundua dawa mbali mbali za asili zinazotibu maradhi mengi
Lini mtaanza kuwatambua na kuwasajili?
Mmejipangaje kuhusu kuanzisha kozi za mimea tiba kwenye mitaala ya famasi ili kuchochea ugunduzi wa dawa mpya kwa vijana wasomi na ukuaji wa sekta ya dawa?
Je mmejikita kwenye utoaji wa dawa, utunzaji na usajili pekee?
Kwanini mmefuta kozi za ADDO ?
Nawasilisha nitashukuru kwa moyo wa dhati na unyenyekevu mkubwa endapo nitapata ufafanuzi
Ni mimi OMOYOGWANE member wa hapa jukwaani Mtanzania mkulima
Ahsante
Ahsanteni piaUdhibiti na Usajili wa Dawa upo chini ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba na kwa dawa za asili zinazajiliwa na Baraza la Tiba Asili chini ya Wizara ya Afya ambalo lina wawakilishi kila Mkoa na Wilaya wanaofanya kazi chini ya Ofisi za Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya.
Pia Taasisi ya Tiba Asili - Muhimbili (Institute of Traditional Medicine) wanatoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa watu wanaojihusisha na Tiba Asili. Unaweza kuwatembelea Upanga Muhimbili au kupitia tovuti yao.
Ahsante
TM