Henry Matata: Dr. Slaa mwongo no. 1 duniani

CDM nao wawe wanaangalia aina ya watu wa kuwasimamisha kama wagombea wakati wa chaguzi. vichwa vingine already vina ukichaa. huyo matata sishangai kwa utumbo anaotapika maana hata ktk taarifa ya habari ya ITV alishawahi kuoneshwa akipigana ngumi huko mwanza!
 
Makene nimekupata Slaa ni tishio no. 1 pale magogoni ndo maana ccm hawalali. Na sijui hawa ssm wanataka kukaa madarakani hadi lini mimi nasema ssm wakiingia tena ikulu basi tz kama nchi itakuwa ikisikika kwenye ramani tuu itatoweka ghafla.
 
Last edited by a moderator:
Matataaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! Ama kweli nyani haoni k****** le.
Matata huyu mimi ninaye mfahamu tangu miaka ya tisaini!.
Matata huyu ambaye anaishi pale Kirumba mbungani!.
Matata huyu ambaye alimwibia dada yake vifaa vya muziki na kuvifanya vyake kisha akamtishia kwa kumuua!
Matata huyu ambaye miaka hiyo ya tisaini alikuwa akiongoza kikosi cha kusafirisha bia kwa magendo toka kenya na uganda kwa magendo huku akiua wavuvi hapo ziwa vICTORIA!
Matata huyu ambaye amejenga pagala ambalo halijulikani kama ni Guest! Nyumba ya kuishi! Club! Bar! Hall! au ukumbi wa cinema!
Matata huyu ambaye ni kibaka mzoefu!
Matata huyu ambaye amejenga katika eneo la wazi!
Matata huyu ambaye ukiingia kwenye ukumbi wake na mwanamke mzuri anakuandalia majambazi wa kukupola!
Matata huyu ambaye alikuwa akiwakaba wateja wake chooni wale walionekana kuwa na pesa!
Jamani labda ni Matata mwingine ambaye mlimpa udiwani baada ya mimi kuondoka katika jiji hilo miaka kadhaa! Lakini kama ndio huyo ninaye mfahamu tangu miaka hiyo tukilewa pamoja, huyo ni kibaka namba moja.

TAHADHARI: umefika wakati sasa ambapo chama kinatakiwa kuwa macho katika uteuzi wa viongozi, bora kukosa kiongozi kuliko kuwa na mtu kama MATATA.

HAYA NI MACHACHE NINAYOYAJUA KWA HUYU BWANA, KAMA ANAKANUSHA AJE HAPA..................
 
Meya wa manispaa ya Ilemela jijini Mwanza amekiri kuwa anamiliki jeshi ambalo analitumia kupambana mara inapohitajika kufanya hivyo.

Akiongea na kituo cha Redio Kwa Neema fm jijini hapa meya huyo amesema kuwa "ndugu mtangazaji,niko fiti nina majeshi yangu".CHADEMA nimewashinda mara nyingi,niliwapiga kwenye kikao cha kwanza walipokataa kuteua jina langu kugombea umeya kikao kikavurugika (Ni kweli alituma watu na kuvuruga mkutano)."Nimewashinda ktk umeya."Mimi ni diwani wa mahakama,kama isingekuwa mahakama mimi nisingekuwa meya."

Aliendelea kusema yuko fiti kwa kila kitu hata ngumi.Alipohojiwa na mtangazaji kuwa kama atakuwa tayari kukutana diwani Abubakari Kapela hapo studio,meya huyo alisema kuwa hawezi kuongea na mpumbavu kama Kapela,isipokuwa labda wapambanishwe nae kwa ngumi ili tuone nani mshindi.

Aidha meya huyo ilifikia hatua kumwomba mtangazaji ampe ruhusa kumtukana mchangiaji mmoja kwenye simu ambapo alikataliwa kwani alikuwa amepanic kutokana na simu zote zilizopigwa watu walikuwa wakimpönda hakupata hata mmoja aliemsapoti.Ilifikia hatua ya yeye Matata kumlazimisha mtangazaji awazimie simu wachangiaji.

Haya ni machache ukitaka kusikia matusi mengi aliyotoa na pia kuahidi mbele ya Mwigulu kuwa 2015 atagombea kupitia CCM,fuatilia marudio ya kipindi hicho.
 

Sina budi nikubaliane nawe kwa hili.

CHADEMA wanatakiwa waondokane na siasa za matukio ambazo wanazitumia pia katika kuwapata viongozi wao.

Ni cha kushangaza sana pale mtu anapoongea sentensi mbili au tatu kwenye hadhara na watu wakimshangilia basi kesho unakuta ameishapewa uongozi au anakuwa mteule wa kata, jimbo kuwa mgombea wao, na kwa vile katika maeneo mengi CCM inakuwa imechokwa, basi hata uwezekano wa kuchaguliwa pia unakuwa ni mkubwa bila kujari kama ni makapi ( empty substance)

Matatizo yaliyopo kwa sasa ndani ya CHADEMA ni matokeo ya kuokoteza watu barabarani na kuwapa uongozi bila hata ya kuwapitisha kwenye tanuru la moto(scan). Kwa maana nyingine, CHADEMA is reaping what they sow.

Kwa wale tunaoangalia kwa mbali, marumbano yanayoondelea hapa jf kati ya hawa wanaojiita viongozi wa CHADEMA (BAVICHA) inatoa picha kama ni viongozi wa aina gani pia tutegemee kwa kipindi kijacho kama hawa ndiyo viongozi wa vijana ndani ya chama.
 
Mwongo namba 1 duniani? loh

Yaani kwa maneno mepesi ni kuwa ukichukua waongo wote duniani mchumba wa josephine anaongoza kwa uongo.

hili neno kubwa sana! mtake radhi slaa.

Inaonekana Josephine alikupiku
 
Huyu diwani si yule aliyepokea mil 20 kutoka kwa CCM na kukiri mbele ya kamati kuu ya CHADEMA?

Hafai,huwa anamshambulia sana Dr kwenye media
.
Hiyo ndio sababu! Tatizo lenu cdm mnapenda kusikua mazuri ya DK slaa tu, hamtaki mabaya yake.
 
Chama changu kimeingia kirusi kibaya. Watu wanafanya kazi ya kubomoa chama badala ya kukijenga. Wengine wanathubutu kwa dhati kabisa kufanya kazi za CCM...
njaa ndo ilivo mwanajamvi!
 
Hao kwa jina jengine ni wanachama kumbi kumbi
 
Hivi ni Matata yule ambaye miaka ya 80 alikuwa anateka watu na kuwaweka ktk meli zake zilizokuwa zinafanya biashara ya magendo kati ya Mwanza , Uganda na Kisumu na kuwatumbukiza majini?. Ambaye pia anamiliki hoteli fulani hapo Mwanza. Nakumbuka kijana wa Chief Fundikira aliwahi kuwa mhanga ugaidi wa bwana huyu.
Kama ndiye yeye na CCM wanamuona wa maana na kumtumia, basi Mungu atawaangushia laana kubwa itakayopelekea anguko kubwa siku za usoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…