Nimekaa Mbeya miezi miwili sasa, ila nimenyoosha mikono. Mbeya ni likijiji likubwa, picha linaanza kila mtu kajaa vumbi kuanzia usoni hadi miguuni. Huwezi kutembea Mbeya kwa raha, bajaji zina fujo, highway hakuna sheria zinafuatwa, vumbi kama lote. Utapata mtu kapendeza town, ila chini ana soksi, jinsi vumbi linakera!
Ukija kwenye biashara, hawa watu hawana habari na customer service, utachoka wewe mteja....wahehe wanasema 'sindimgaya sida'...vifungashio vyao utalia. Yaani wanafanyia biashara kimaskini, imagine mfuko ulioisha diapers, mama muuza matunda anakupa ndo uwekee matunda. Usiponunua mfuko wako, utalishwa uchafu ufurahi.
Mbeya panasifika Kwa vyakula vingi, ila nimechoka mwili na roho kwasababu menu zao ni ugali na wali kila siku, hapo utawekewa na chainizi, maharage na nyama(nilitafuta mtori, nikaambiwa huku ukipika mtori hakuna wa kununua, ndizi za kupikwa pia siyo kitu utakikuta sana sehemu za vyakula). Au uende sehemu za kitimoto, manake huku mdudu amejaa kila Kona au ule chips na zile nyama choma zao. Kupata matunda yaliyokatwa ni shidaaaaa, nasema ni shida. Ukitaka kula varieties lazima jasho likutoke. Nikaja kuelewa kwanini wakazi wengi wa hili likijiji wanamaumbo ambayo huwezi jua kiuno Kiko wapi, matumbo yao yamejaa wanga hatari, swala la balance diet kwao ni ndoto. Ukionwa unakula matunda laZima uulizwe kama wafanya diet au. Wako na ushamba fulani hivi wakazi wa huku, kwanini Mbeya ni Jiji? Aibu naona mimi.
Mbeya katikati ya mji Ile mitaa ya Mwanjelwa Kuna watu wanapika chips kwa kutumia kuni, basi Moshi unasambaa maduka ya jirani hadi siyo poa, na Watanzania tunajua kuvumiliana, basi majirani wanavumilia. Sehemu imejaa Moshi, unakaaje hata ule chakula? Na kwamba hakuna kiongozi anayeona hiyo shida? Katikati ya mji kabisa?
Hapo sijagusia miundombinu, mipango ya mitaa, majengo yao, ni fujo TU. Halafu vijana wengi wa rika fulani hawaogi, wote wananuka harufu hiyo hiyo....wanaogopa maji hatari. Wakija kupata huduma ofisini unatamani umwambie Kaa kwanza pembeni nitakuhudumia ukiwa umekaa ili Ile harufu yake isijae kwenye dirisha lako.
Kuna mtaa street lights zinawaka kwa sensor, Kuna muda sensor zinafanya kazi, Kuna muda hazifanyi. Usiku wa Giza kabisa taa inawaka sekunde mbili inajizima. Kweli aliyefunga hizi taa ni mzima kabisa?
Baada ya kusema haya, na kwa mpangilio mbovu, niseme TU, Watanzania tunasafari ndefu ya kuishi kwa ustaarabu kwenye miji yetu. Uchafu kila sehemu, noise pollution ndo usiseme, hard waste zimetapakaa kila sehemu. Hatuoni shida?
Am out.
Ukija kwenye biashara, hawa watu hawana habari na customer service, utachoka wewe mteja....wahehe wanasema 'sindimgaya sida'...vifungashio vyao utalia. Yaani wanafanyia biashara kimaskini, imagine mfuko ulioisha diapers, mama muuza matunda anakupa ndo uwekee matunda. Usiponunua mfuko wako, utalishwa uchafu ufurahi.
Mbeya panasifika Kwa vyakula vingi, ila nimechoka mwili na roho kwasababu menu zao ni ugali na wali kila siku, hapo utawekewa na chainizi, maharage na nyama(nilitafuta mtori, nikaambiwa huku ukipika mtori hakuna wa kununua, ndizi za kupikwa pia siyo kitu utakikuta sana sehemu za vyakula). Au uende sehemu za kitimoto, manake huku mdudu amejaa kila Kona au ule chips na zile nyama choma zao. Kupata matunda yaliyokatwa ni shidaaaaa, nasema ni shida. Ukitaka kula varieties lazima jasho likutoke. Nikaja kuelewa kwanini wakazi wengi wa hili likijiji wanamaumbo ambayo huwezi jua kiuno Kiko wapi, matumbo yao yamejaa wanga hatari, swala la balance diet kwao ni ndoto. Ukionwa unakula matunda laZima uulizwe kama wafanya diet au. Wako na ushamba fulani hivi wakazi wa huku, kwanini Mbeya ni Jiji? Aibu naona mimi.
Mbeya katikati ya mji Ile mitaa ya Mwanjelwa Kuna watu wanapika chips kwa kutumia kuni, basi Moshi unasambaa maduka ya jirani hadi siyo poa, na Watanzania tunajua kuvumiliana, basi majirani wanavumilia. Sehemu imejaa Moshi, unakaaje hata ule chakula? Na kwamba hakuna kiongozi anayeona hiyo shida? Katikati ya mji kabisa?
Hapo sijagusia miundombinu, mipango ya mitaa, majengo yao, ni fujo TU. Halafu vijana wengi wa rika fulani hawaogi, wote wananuka harufu hiyo hiyo....wanaogopa maji hatari. Wakija kupata huduma ofisini unatamani umwambie Kaa kwanza pembeni nitakuhudumia ukiwa umekaa ili Ile harufu yake isijae kwenye dirisha lako.
Kuna mtaa street lights zinawaka kwa sensor, Kuna muda sensor zinafanya kazi, Kuna muda hazifanyi. Usiku wa Giza kabisa taa inawaka sekunde mbili inajizima. Kweli aliyefunga hizi taa ni mzima kabisa?
Baada ya kusema haya, na kwa mpangilio mbovu, niseme TU, Watanzania tunasafari ndefu ya kuishi kwa ustaarabu kwenye miji yetu. Uchafu kila sehemu, noise pollution ndo usiseme, hard waste zimetapakaa kila sehemu. Hatuoni shida?
Am out.