Na kwa ukubwa wa transfer hizi, je haikuhitajika approval ya BOT, au hapo utaratibu ukoje? Na je, wenzetu hawaombwi supporting document ya hizo transfer?
Huna sababu za kumuomba supporting documents kwa sababu huyu ni mteja wako na ulishamtambua siku unamfungulia akaunti. Unaweza kutaka supporting document if and only if, hayo ndiyo masharti ambayo aliyaweka yeye mwenyewe wakati anafungua akaunti! Baadhi ya taasisi zinapofungua akaunti, zinasema(written) in advance kwamba withdrawal above certain limiti lazima kuwe na hiki au kile (including people to authorize/approve).
Transaction pekee ambayo nafahamu lazima iwe na supporting document ni Government Cheques. Kabla government cheque haijalipwa, lazima kuwe na checklist iliyosainiwa na signatories wa akaunti husika otherwise, cheque hairuhusiwi kulipwa. Kisheria, hii checklist inatakiwa kufika bank kabla mteja hajafika lakini kwenye mambo ya business as usual, usishangae ukaona mteja mwenyewe anakuja na cheki na upande mmoja kabeba checklist. Only stupid person can effect such payment ingawaje zinafanyika sana hususani kwa cheki za halmashauri!!!
Kama nilivyosema awali, sehemu kubwa ambayo Stanbic wanawajibika ni hiyo inward transaction ya $ 22 million na sio hizo outward. Hiyo $ 22 million Stanbic ilikuwa ni lazima wajiridhishe kwamba ni genuine transactions...!
Hata hivyo, kuna post moja niliandika kwamba, unapomtambua mteja wako kwa mara ya kwanza, fanya jitihada za kufahamu ni kwanini anafungua akaunti... don't ask him/her a direct question kwamba kwanini anafungua akaunti! Hivyo basi, ukija kwangu na mathalani unataka kufungua personal account; naweza kukufungulia huku ukiwa na introduction letter peke yake provided nimejiridhisha na hiyo barua coz' sheria ya BOT ya Know Your Customer inasema "A customer should provide introduction letter OR ID card! Hata hivyo, ingawaje unafungua personal account, nikishagundua kwamba unataka ku-deposit cheque au kuna money transfer unaitarajia... hapo piga ua nabadilisha hiyo sheria mwenyewe na badala ya kuwa Introduction OR ID Card, itakuwa Introduction Letter
AND ID card from mamlaka inayotambulika na hapo nitakuwa makini mara mbili ya ile ya awali! WHY? Ni kawaida sana kuona mtu aitwae Juma anakuja kufungua akaunti kwa jina la John kwavile ana cheki ya wizi yenye jina la John! Kwahiyo hapo lazima ujiridhishe kwa 100% kwamba huyu aliye mbele yangu ni John na huwezi kujiridhisha kwa barua peke yake!!
Sasa basi, ukija kwenye hiyo akaunti ya PAC...inaonesha wazi kwamba ilifunguliwa kwa ajili ya ku-facilitate hiyo inward transaction ya $22 million. Ukiangalia vizuri hiyo statement, utagundua hiyo $ 22 million ni transaction ya kwanza! Kwa kutumia kigezo hicho, Stanbic walitakiwa si tu kufahamu source ya hiyo $ 22 million bali ni kwanini baada ya muda zinaanza outwards transaction kutokea kwenye hiyo amount! Sisemi kwamba kuna dhambi hapo bali walitakuwa kuwa suspcious hasa kwa kuzingatia ni nani beneficiaries wa hizo outward transactions. Kama zilikuwa zinaenda kwa business entities, no offense coz' PAP ni wafanyabishara kwahiyo kwao ingekuwa ni rahisi kusema wanalipa suppliers wao! Lakini kama zilikuwa zinaenda kwa watu binafsi, nadhani walitakiwa kuwasiliana na TAKUKURU na ku-raise their suspicions.
Kama walihitaji approval ya BOT... kama hiyo sheria ipo sijui but if you ask me, naweza kusema hiyo sheria hakuna! Kwa akaunt za biashara kufanyika transactions kubwa ni jambo la kawaida.
Pamoja na yote hayo... hiyo statement hapo juu tunachoona ni only one page lakini ukisoma juu ya neno TAX INVOICE... juu kabisa ya kulia mwa statement, unakuta neno Page 1 of 7. Hizo page 6 zilizobaki sijui zimeishiwa wapi!!!