Hekaya za bahlul 1

KABAVAKO

JF-Expert Member
Apr 5, 2011
229
32
Nimekuandalieni mfululizo wa makala ziitwazo Hekaya za Bahlul. Makala hizi zina ukweli ndani yake ndani ya Historia ya Mashariki ya kati. Tutaanza kwa kukupa maana ya Bahlul na Historia yake.
Bahlul ni kumaanisha kwa ujumla wa kucheka, uwema na pendeza.


Majibu haya yanaweza kuwa mafunzo kwa watu wa kila aina hadi katika zama zetu na mbeleni.

Watu wengi waliweza kutokezea kwa jina hilo, lakini mashuhuri ni lile la Bahlul aliyekuwapo katika zama za Harun al-Rashid. Bahlul alikuwa ni mmoja wa wanafunzi bora wa Imam Jaafer as-Sadiq a.s. na vile vile alikuwa mpenzi wa Ahli-Bayt a.s. ya Mtume s.a.w.w.

Vile vile inasemekana kuwa Bahlul alikuwa na undugu wa Harun Rashid kwa upande wa mama yake na riwaya nyingine imesemwa kuwa alikuwa jamaa wa karibu wa Harun.
Qadhi Nurallah Shushtary anasema katika kitabu chake Majalis al-Muuminin Bahlul alikuwa ni mtu mwenye akili mno ambaye kwa sababu fulani fulani alijigeuza mwendawazimu.

Bahlul alizaliwa Kufa na jina lake la asili lilikuwa Wahab bin Umru. Kwa mujibu wa riwaya moja, Harun Rashid alimwona Imam Musa bin Jaafer a.s. kama tishio kubwa kwa kubakia utawala wake. Hivyo alijishughulisha katika mbinu za kutaka kumwua. Na aliweza kutafuta hila moja ya kumwua. Hivyo alimzulia dai la kuasi na hivyo aliwataka hukumu wacha Mungu ya kumwua Imam, ambamo Bahlul pia alikuwamo. Wote walitoa fatwa ya kuuawa kwa Imam a.s. lakini Bahlul aliipinga. Bahlul alimwendea Imam a.s. na kumjulisha yale yaliyokuwa yakitokea, na alimwambia Imam a.s. ampatie ushauri na njia za kuyakabili hayo. Imam a.s. alimwambia kuwa ajigeuze na awe mwenda wazimu.

Hii ndiyo sababu ya yeye kuwa mwenda wazimu kwa matakwa ya Imam a.s. na hivyo aliweza kuepukana na adhabu na maangamizi ya Harun Rashid, aliyekuwa Khalifa wakati huo. Na hivyo bila ya woga wowote akijifanya mwenda wazimu, aliweza kukabili, kumsuta hata Khalifa na mawaziri wake na papo hapo aliwatetea wanyonge na wale wote waliokuwa wamedhulumiwa. Pamoja na hali yake hiyo, watu walimpenda kwa mioyo yao, hadi leo hekaya zake zinasimuliwa katika vikao na kujifunza mengi kutokana hayo.

Kwa mujibu wa riwaya ya pili - ambayo inasadikiwa zaidi. Masahaba na wapenzi wa Imam a.s. walikuwa wametingwa na udhalimu wa Khalifa na watawala wake. Hivyo wote walimwomba Imam a.s. uongozi kuhusu swala hilo. Imam a.s. aliwajibu kila mmoja kwa herufi moja tu. "Jim" kwa hivyo walielewa kuwa hapakuwapo na haja ya kuulizia ziada.

Kila mmoja alielewa hilo herufi tofauti tofauti. Mmoja alielewa "Jila Watan" yaani kutoka nyumbani, mwingine alielewa 'Jabl yaani 'Mlimani' na Bahlul alielewa kuwa ikimaanisha 'Junuun' Yaani "Uenda wazimu" na hivyo alijigeuza hivyo na kwa hayo, wote waliweza kunusurika na janga hilo la kuteketezwa na udhalimu wa Khalifa.

Bahlul alikuwa akiishi maisha ya starehe na bora kabisa lakini baada ya ishara hiyo ya Imam a.s. aligeuzia uso dunia na kuziacha starehe zote hivyo akaishi maisha ya utawa na akawa na mavazi yaliyokuwa yamechakaa. Yeye alipendelea kuishi uwanjani kuliko majumba ya Wafalme, vile vile aliishi kwa kipande kikavu cha mkate kuliko kutegemea misaada ya hisani ya Khalifa kwani alikuwa akijiona yu bora kuliko Khalifa Harun Rashid, mawaziri wake na Baraza lake zima.

Bahlul kwa hakika, alikuwa mcha Mungu na mpenzi wake, mwenye akili sawa na Aslim kamili. Yeye alikuwa ni mtu mwenye akili sana na fahamu zaidi na mwenye kutoa majibu ya papo hapo na mtatuzi wa masuala katika zama zake. Jina lake halikuwa mashuhuri tu miongoni mwa watu wenye akili tu bali kwa amri ya Imam a.s. alijifanya mwenda wazimu na hivyo aliweza kuelezea Din na Sharia na kuelezea uhakika na ukweli wa Ahli Bayt a.s.

Katika zama hizo hapakuwapo na njia nyingine ila yeye kujifanya mwenda wazimu amasivyo Harun Rashid angalimwua. Kama vile Harun Rashid alisikiliza uthibitisho wa Uimam Musa ibn Jaafer a.s. kutoka mwanafunzi mmoja wa Imam Jaafer as-Sadiq a.s. Hisham bin Hikam, na akamwambia Waziri wake Yahya ibn Khalid Barki: "Ewe Yahya! Maneno ya mtu huyu, Hisham, kwangu mimi ni sawa na tishio la mapanga laki moja, lakini jambo la kushangaza ni kule kubainika kwake hai wakati mimi natawala!"
Harun alibuni kila aina ya mbinu za kutaka kumwua Hisham. Na alipopata habari hizo, alitorokea Kufa ambako aliishi nyumbani (mafichoni) mwa rafiki yake, na katika kipindi kifupi alifariki.
 
Back
Top Bottom