Hee! 'Kitimoto' na Mapepo ni Damdam?

Hee! 'Kitimoto' na Mapepo ni Damdam?

dalalitz

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2013
Posts
3,476
Reaction score
2,086
Awali ya yote ifahamike kuwa Mie sijabobea kwenye elimu ya Biblia.
Hata hivyo,
Ni muumini mzuri wa kuhitaji kuongeza taarifa na maarifa pale inaponiruhusu.

Ni kwa mukhtadha huo basi leo nikiwa napitia luninga tofauti tofauti nikakutana na kituo cha Channel Ten kikirusha filam ya Maisha na miujiza ya Bwn. Yesu.

Moja wapo ya tukio lililonifikirisha na ambalo ningeomba kwa yoyote mwenye ufahamu wa kutosha kunidadavulia mantiki,sababu/funzo au lengo la sehemu moja wapo inayoonekana katika filam hii, Tukio ambalo Sina Shaka litakuwa linao ufafanuzi kutoka kwa waliobobea.

Nalo ni pale ambapo Bwana Yesu,
Akiwa ametangulizana na wanafunzi wake katika harakati za kusambaza Neno;
Anafika sehemu (Ugenini),
Ikiwa taarifa juu yake zikiwa zimekwishafika,
Na akichukuliwa kama si mtu mwema,
Anatokea bwana mmoja akiwa na dhamira ya kuwadhuru Yesu na wenzake,
Lakini Yesu anajipeleka mbele ya huyu bwana, kimiujiza huyu bwana anaishiwa nguvu ghafla.
Lakini hapo hapo inaelezwa kuwa;
Yule bwana
(Aliekusudia kudhuru) alijawa na pepo wabaya na hivyo Bwana Yesu kwa uwezo aliokuwa nao aliweza kuwatoa wale Mapepo na kisha kuyatupa kwa Nguruwe (Kitimoto) ambao walikuwepo sehemu hiyo na wanaonekana 'Kitimoto' hao wakitawanyika (Na Mapepo yao, eti)

Huku Yule bwana akidai sasa kuona ukweli na akiapa kujiunga na harakati za Yesu za kusambaza Neno.

Nimefuatilia hadi mwisho wa filam hiyo sijaona mahali 'Kitimoto' hao tena Wala wakitolewa (kuopolewa) dhidi
Ya yale Mapepo.

Sasa najiuliza;

Kitimoto ni Mapepo?
Au

Si Mapepo lakini wanamapepo?

Na je,
Anaekula-je?

Ufafanuzi kwa ajuae tafadhali.
 
Kitimoto si mapepo eti tu sababu mapepo yaliwaingia.mbona wanadamu wana mapepo mengi tu je na binadamu ni mapepo ?
Ilikuwa tu ni sehemu salama mapepo kukaa bila kubuguziwa yangeweza kwenda baharini au kwa watu.
 
Wewe acha kuzuzuka na movie nguruwe wa miaka karibia 2000 iloyopita adi leo wapo dunia kweli? Wale waliopewa mapepo ni wakipindi kile lakini hawa wasasa hawana hayo unayoyaita mapepo.
 
Wewe acha kuzuzuka na movie nguruwe wa miaka karibia 2000 iloyopita adi leo wapo dunia kweli? Wale waliopewa mapepo ni wakipindi kile lakini hawa wasasa hawana hayo unayoyaita mapepo.
Teheeee!
Kweli,
Aliependa, Chongo huita Kengeza.
 
Teheeee!
Kweli,
Aliependa, Chongo huita Kengeza.
Ule usemi wa samaki mmoja akioza ni wote wameoza hiyo hatu apply kwenye nguruwe. Waliotupiwa mapepo na yesu ni wale wakipindi kile cha yesu, lakini hawa tunaofuga mitaani hawana na hawajawai kuwa na hayo mapepo.
 
Ule usemi wa samaki mmoja akioza ni wote wameoza hiyo hatu apply kwenye nguruwe. Waliotupiwa mapepo na yesu ni wale wakipindi kile cha yesu, lakini hawa tunaofuga mitaani hawana na hawajawai kuwa na hayo mapepo.
Mkuu,
Sikuonei donge kama umejihakikishia kuwa ni halali kwako jimwaemwae kwa Raha zako.
 
Hapa nilipo nimefuga nguruwe 3 waislam wakipita hapa hukunja nyuso zao na kuondoka, zaidi hawa wadudu hufukuza majini, hakuna cha jini makata au sharif majini. Ila hata hao wavaa kanzu wanampenda sana huyu mdudu ila kwa kujificha.
 
Labda ujaelewa ni kwamba aliyaamulu mapepo wayaingie nguruwe lakini nguruwe wakaona ujinga kuingiliwa na mapepo ni heri kujitupa baharini tufe . Hivyo nguruwe wakajitupa baharini na kufa.. mapepo walipoona wamekosa makazi waliyoamuliwa wakaona waweke makazi tu baharini ndio maana hadi leo hii mapepo makazi yao ni baharini...
Kitendo kile kiliwachosha mapepo na kuwachukulia nguruwe ni kama wendawazimu kujiua hivyo hadi leo mapepo hayataki masihara na nguruwe kabisa..
 
Kitimoto si mapepo eti tu sababu mapepo yaliwaingia.mbona wanadamu wana mapepo mengi tu je na binadamu ni mapepo ?
Ilikuwa tu ni sehemu salama mapepo kukaa bila kubuguziwa yangeweza kwenda baharini au kwa watu.
Ndio kusema upo uhusiano wa karibu kati ya 'Kitimoto' na Mapepo hadi sasa?
Kama haupo uhusiano je,
Ni nani aliyaopoa mapepo hayo,wapi na kwa uthibitisho upi?
Tujiridhishe.
 
Awali ya yote ifahamike kuwa Mie sijabobea kwenye elimu ya Biblia.
Hata hivyo,
Ni muumini mzuri wa kuhitaji kuongeza taarifa na maarifa pale inaponiruhusu.

Ni kwa mukhtadha huo basi leo nikiwa napitia luninga tofauti tofauti nikakutana na kituo cha Channel Ten kikirusha filam ya Maisha na miujiza ya Bwn. Yesu.

Moja wapo ya tukio lililonifikirisha na ambalo ningeomba kwa yoyote mwenye ufahamu wa kutosha kunidadavulia mantiki,sababu/funzo au lengo la sehemu moja wapo inayoonekana katika filam hii, Tukio ambalo Sina Shaka litakuwa linao ufafanuzi kutoka kwa waliobobea.

Nalo ni pale ambapo Bwana Yesu,
Akiwa ametangulizana na wanafunzi wake katika harakati za kusambaza Neno;
Anafika sehemu (Ugenini),
Ikiwa taarifa juu yake zikiwa zimekwishafika,
Na akichukuliwa kama si mtu mwema,
Anatokea bwana mmoja akiwa na dhamira ya kuwadhuru Yesu na wenzake,
Lakini Yesu anajipeleka mbele ya huyu bwana, kimiujiza huyu bwana anaishiwa nguvu ghafla.
Lakini hapo hapo inaelezwa kuwa;
Yule bwana
(Aliekusudia kudhuru) alijawa na pepo wabaya na hivyo Bwana Yesu kwa uwezo aliokuwa nao aliweza kuwatoa wale Mapepo na kisha kuyatupa kwa Nguruwe (Kitimoto) ambao walikuwepo sehemu hiyo na wanaonekana 'Kitimoto' hao wakitawanyika (Na Mapepo yao, eti)

Huku Yule bwana akidai sasa kuona ukweli na akiapa kujiunga na harakati za Yesu za kusambaza Neno.

Nimefuatilia hadi mwisho wa filam hiyo sijaona mahali 'Kitimoto' hao tena Wala wakitolewa (kuopolewa) dhidi
Ya yale Mapepo.

Sasa najiuliza;

Kitimoto ni Mapepo?
Au

Si Mapepo lakini wanamapepo?

Na je,
Anaekula-je?

Ufafanuzi kwa ajuae tafadhali.
kila siku unakunywa maji, na majini ni viumbe roho, vichafu hatari, vinaishi kwene maji na kwa kutokuwa na jina waliviita majini kwa kuwa vinaishi humo hapa napo unapasemeaje?
 
Acha kufananisha kitimoto na ujinga

Sijafananisha.
Nimehoji UHUSIANO (wakaribu sana) kati ya 'Kitimoto' na Mapepo ambao unao ushahidi wa kimaandishi pasi na chembe ya Shaka.

Unadhani ningekurupuka Hali ya hewa ingekuwa shwari hapa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom