Healing is a process sio tukio la siku moja

Healing is a process sio tukio la siku moja

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,077
Reaction score
1,444
Healing

Juzi nilikuwa Nyamagana, ndani ya ukumbi wa Tanzanite, tukizungumza kuhusu healing.

Nikasisitiza jambo moja muhimu sana:
Mtu inaweza kupita miaka 10… na bado hajapona.
Kwa sababu healing si tukio la siku moja, ni process.
Na zaidi ya yote, ni suala la utayari wa ndani.

Ndipo jamaa mmoja akasimama akasema:
“Mi nishaheal kabisa, niliachana na mke wangu miaka 6 iliyopita.”

Nikamuuliza
“Mkeo anaitwa nani?”

Akasema: Annastazia Johnson.

Nikamtazama, nikamwambia kwa upole lakini kwa uhakika:
“Mkeo sasa yuko kwenye ndoa mpya, ana mapacha wawili, ana furaha sana…
Na ukweli ni kwamba hata hakumbuki kama aliwahi kuolewa kabla.
Mtoto wako pia sasa anatumia ubini wa mume wake wa sasa.
Na wiki ijayo wanaenda vacation Uturuki.”

Ukimya ukatawala sekunde chache.

Nikamalizia:
“Kabla hawajaoana, nilikuwa mshauri wao wa ndoa… ndiyo maana nilipolisikia hilo jina, nikamfahamu.”

Ghafla… yule jamaa akalipuka:

“Yule ana mambo mengi hawezi kuolewa! Hakuna mtu angeoa ile takataka!”

Matusi yakaanza kumwagika… hasira, chuki, maumivu—vyote vikaanikwa wazi.

Nikamtazama tu nikamwambia:

“Unaona sasa… bado hujaheal.”

Ukikimbia healing, haimaanishi umepona.
Ina maana umeahirisha maumivu.

Na siku moja… yatakurudia kwa nguvu mara mbili.

Healing si kujisahaulisha.
Healing ni kukubali.

Kukubali kuwa umeumizwa.
Kukubali kuwa imekwisha.
Kukubali kuwa huwezi kubadilisha kilichopita.

Kwa sababu:

👉 Maumivu ukikubali, yanakufundisha.
👉 Maumivu ukiyakubali, yanapungua.
👉 Maumivu ukiyakataa… yanakutawala.

Ukishaumia na ukakubali, utaumia mara moja au mbili tu.
Lakini ukiyakataa maumivu… utaendelea kuumia tena na tena.

Usijidanganye umeheal kwa sababu umepita muda mrefu.

👉 Bado unachukia?
👉 Bado una hasira?
👉 Bado unalipuka ukikumbushwa?

Kama jibu ni ndiyo…

Bado una safari ya kufanya.

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
Mwanza
 
Kuachana kunaruhusiwa mkuu.., huwezi kukaa na abusive partner, toxic…sababu tu unataka uonekane uko ndoani….

Huyo rafiki yako ame react kutokana na experience yake na Huyo mwanamke sio kwamba amemiss uwepo wake au anampenda still. Ume interpret vibaya
 
Kwanini tuheal? Maana kilicho sababisha kuumia kiendelee kuumiza wengine? Hatuwezi kuheal kamwe. Ukishasema nataka kuheal Bado ndani yako kutakuwa na masononeko yasemayo " ila yule mjinga hakupata revenge" so Mimi naona ni tit for tat. Hakuna maswala ya kuheal hapa. Mtu akizingua lazima alipe in one way or another
 
Kwanini tuheal? Maana kilicho sababisha kuumia kiendelee kuumiza wengine? Hatuwezi kuheal kamwe. Ukishasema nataka kuheal Bado ndani yako kutakuwa na masononeko yasemayo " ila yule mjinga hakupata revenge" so Mimi naona ni tit for tat. Hakuna maswala ya kuheal hapa. Mtu akizingua lazima alipe in one way or another
Tit for tat ni revenge , ni kama unywe sumu halaf utegemee afe bro ni day light dreaming. Ukianza ku accept that when good things start coming back
 
Tit for tat ni revenge , ni kama unywe sumu halaf utegemee afe bro ni day light dreaming. Ukianza ku accept that when good things start coming back
Haunywi sumu! Unahakikisha aliyekuumiza anapata alichokotaka. In every action there's equal and opposite reaction.
 
Ubongo wa binadamu ulivyo, hakunaga cha ku heal.

Ubongo unatunza kumbukumbu vibaya mno.

Hata ukae miaka 50, Ukikutana na mtu uliyemchukia sana, Ubongo utarudisha kumbukumbu haraka sana. Na chuki itarudi on the spot.

Hakunaga ku heal.

Ubongo hautambui hicho.

Ubongo una react kwa namna ile, ulivyo react tukio hilo kwa mara ya kwanza.

Ndio maana ukishang'atwa na nyoka 🐍 hata jani 🌱likikugusa tu, Ubongo unarudisha kumbukumbu za ulivyong'atwa na nyoka.
 
Katika maisha

1. Ili uwe na historia ya maisha ya furaha lazima utengeneze historia ya maumivu

2. Hakuna adui wa asili, wote mlikuwa marafiki na baadae mkawa maadui, kwa hyo katika mahusiano kufurahia na baadaye kuumia tena ukaja kuwa na furaha ni jambo la kawaida ijapo la mchakato.

3. Maumivu ya kuachana na mtu mlie zaa naye huwa si marahisi maana ni vigumu sana kusahau (maumivu huwa yameahirishwa)
-kuna mtu waliachana na mke wake, wakaja kurudiana baada ya miaka minane

4. Kujifariji kuwa humkumbuki mkeo mliechana naye lakn una historia naye kichwani mwako hyo ni mbay kuliko kansa, maana unakuwa katika utumwa wa maumivu usioisha.

5. Tujitahidi sana kuepuka kutengeneza maumivu katika maisha kama hatuwezi kuyaishi.
 
Ubongo wa binadamu ulivyo, hakunaga cha ku heal.

Ubongo unatunza kumbukumbu vibaya mno.

Hata ukae miaka 50, Ukikutana na mtu uliyemchukia sana, Ubongo utarudisha kumbukumbu haraka sana. Na chuki itarudi on the spot.

Hakunaga ku heal.

Ubongo hautambui hicho.

Ubongo una react kwa namna ile, ulivyo react tukio hilo kwa mara ya kwanza.

Ndio maana ukishang'atwa na nyoka 🐍 hata jani 🌱likikugusa tu, Ubongo unarudisha kumbukumbu za ulivyong'atwa na nyoka.
Kumbukumbu hazipotei lakini chuki na maumivu hupungua mkuu!
 
Kumbukumbu hazipotei lakini chuki na maumivu hupungua mkuu!
Hupungua ndio lakini ubongo hauwezi ku heal tena kuhusu tukio au mtu huyo.

Ubongo utaweka tahadhari sana kuhusu mtu au tukio hilo.

Huwezi ku heal completely.
 
Hupungua ndio lakini ubongo hauwezi ku heal tena kuhusu tukio au mtu huyo.

Ubongo utaweka tahadhari sana kuhusu mtu au tukio hilo.

Huwezi ku heal completely.
Lakini haina madhara kwa wakati huo kuliko hapo awali!
 
Kuhusu issue ya ku heal naona inatokana na tukio husika kuna vitu havifuti ng'oo utasahau kwa mda fulani tu ila ukiona kitu tukio linalofanana na kichookuumiza lazima tu mood iwe off
 
Physically hakuna tena madhara.

Mentally kuna madhara ya daima na tahadhari kali dhidi ya tukio hilo au mtu huyo.

Yani ukikumbuka tu, Ubongo unarudisha kumbukumbu ile hapohapo.
Haijalishi ni muda gani umepita??
 
Back
Top Bottom