hayati samwel sitta

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Apr 4, 2017
392
946
Buriani SAMUEL JOHN SITTA (Disemba 12, 1942 - Novemba 7, 2016)

Taarifa rasmi ni kuwa Mzee wetu, Spika wa Bunge wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu Samuel John Sitta amefariki dunia akiwa kwenye matibabu nchini Ujerumani. Taarifa zaidi zitatolewa baadaye.

Watanzania Mashuhuri tunaipa pole Familia ya mzee Sitta, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, watu wa jimbo la Urambo Mashariki mkoani Tabora pamoja na Watanzania wote kwa Ujumla.

Pichani ni mzee Samuel John Sitta akiwa pamoja na Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye chini yake mzee Sitta alihudumu kwa nafasi mbalimbali za Uwaziri.

Kwa Picha na Maelezo Juu ya Kumbukumbu mbalimbali za Historia ya Tanzania, Like Ukurasa wa Watanzania Mashuhuri Ili kujifunza Zaidi. Unaweza Kutag Watu Wengi zaidi na Kushare Habari hii Ili kupanua wigo wa Ukurasa kuwafikia Watu Wengi zaidi.

"Watanzania Mashuhuri: Mashujaa wa Jamii, ni Kielelezo cha Jamii Husika".
14906974_1279267295451634_1931658340818395640_n.jpg
 
Naipa pole familia yake kwa sababu ni utamaduni wetu waafrika kupeana pole tunapopata misiba.

Napenda kuwa mkweli.. SIMUONI SAMWEL SITTA KAMA SHUJAA WA TAIFA.

Kitendo cha kupoka maoni ya wananchi ktk rasimu ya katiba mpya, na udanganyifu mkubwa aliousimamia ktk kukamilisha mchakato ule ndani ya bunge maalum la katiba, kwa hakika ni usaliti mkubwa dhidi ya UMMA.

Sioni namna yoyote ya kumtambua Samwel Sitta kama shujaa wa Taifa.
 
Back
Top Bottom