Hayati Nyerere aliwajengea Watanzania uoga?

Hayati Nyerere aliwajengea Watanzania uoga?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,646
Reaction score
10,861
Maelezo yake kwenye clip hapo chini, dakika ya tisa na kumi, yanaonesha kuwa anahisi kuwa alichangia kuwafanya Watanzania kuwa waoga.

Anasema kuwa haikuwa nia yake kulijenga Taifa la watu waoga sana!

Hiyo inamaanisha nini?

1. Alikusudia kulijenga Taifa la watu waoga kiasi gani?

2. Ni kweli Watanzania ni waoga sana?

3. Taifa linanufaikaje linapokuwa na raia waoga sana?

4. Kati ya raia waoga kiasi na waoga sana ni wepi wenye manufaa kwa Taifa?

5. Hayati Nyerere alikuwa sahihi kutaka kulijenga Taifa la watu waoga kiasi na si watu waoga sana?
 

Attachments

  • MWAL__NYERERE_-_RAIS_USIWE_MPOLE_SANA_USIENDEKEZE_WALA_KUPUUZA_MAMBO_YA_DINI(144p).mp4
    25.1 MB
Maelezo yake kwenye clip hapo chini, dakika ya tisa na kumi, yanaonesha kuwa anahisi kuwa alichangia kuwafanya Watanzania kuwa waoga.

Anasema kuwa haikuwa nia yake kulijenga Taifa la watu waoga sana!

Hiyo inamaanisha nini?

1. Alikusudia kulijenga Taifa la watu waoga kiasi gani?

2. Ni kweli Watanzania ni waoga sana?

3. Taifa linanufaikaje linapokuwa na raia waoga sana?

4. Kati ya raia waoga kiasi na waoga sana ni wepi wenye manufaa kwa Taifa?

5. Hayati Nyerere alikuwa sahihi kutaka kulijenga Taifa la watu waoga kiasi na si watu waoga sana?
Tuna elimu mbovu isio wapa raia kujiamini.
 
Umeamua kuungana na hayati Kenyatta kumponda hayati Nyerere?

Inasemekana ni yeye ndiye aliyeianzisha hiyo kauli, kuwa Nyerere alikuwa akiongoza maiti.
Na alikuwa sahihi sana kupitiliza tizama leo hii miaka 60 baada ya uhuru wanyonge wanazidi kunyongwa na maisha
 
Umeamua kuungana na hayati Kenyatta kumponda hayati Nyerere?

Inasemekana ni yeye ndiye aliyeianzisha hiyo kauli, kuwa Nyerere alikuwa akiongoza maiti.
Mybe kenyatta was a bit harsh na kauli zake. But yes he was right, si kumponda ila ni truth. Huu uwoga ndio mpaka leo watawala wanautumia kuwadidimiza wabongo
 
Watanzania sio waoga kama mnavyodhani na ndio maana kesi za raia kwa raia kufanyiziana hazikosekani. Siku katiba ikiheshimiwa na watawala wakaacha kutumia askari kuwanyamazisha raia kwa silaha za moto ndio utaelewa. Bongo hakuna freedom of speech! Watawala wamejigeuza Miungu watu.

Jiulize tu hivi mtu muoga au dhaifu anaweza mkata mapanga mwenziwe? Anaweza kumuua mwenzie kikatili? Watu wangekuwa waoga kesi za kuumizana zisingekuwepo mahakamani.
 
Mybe kenyatta was a bit harsh na kauli zake. But yes he was right, si kumponda ila ni truth. Huu uwoga ndio mpaka leo watawala wanautumia kuwadidimiza wabongo
Halafu huu uoga ukabatizwa jina amani. Unakuta watu anaishi maisha magumu huku viongozi wakichezea kodi zao na hawana la kuwafanya, kisha viongozi wanasifia hayo majoga kwa kuyapaka mafuta kwa mgongo wa chupa kuwa sisi watanzania ni watu wa amani, na tusiichezee amani yetu maana tutajuta tukiipoteza!
 
Watu wanaona kabisa huu muungano sio sawa, ila wanasemea kichinichini Lissu yupo sahihi. Badala ya kupaza sauti kumuunga mkono
Mkuu ni baadhi ya mambo ya kisheria yawekwe sawa tu lakini Zanzibar litabaki kuwa koloni letu mpaka bahari ya hindi ikauke
 
Maelezo yake kwenye clip hapo chini, dakika ya tisa na kumi, yanaonesha kuwa anahisi kuwa alichangia kuwafanya Watanzania kuwa waoga.

Anasema kuwa haikuwa nia yake kulijenga Taifa la watu waoga sana!

Hiyo inamaanisha nini?

1. Alikusudia kulijenga Taifa la watu waoga kiasi gani?

2. Ni kweli Watanzania ni waoga sana?

3. Taifa linanufaikaje linapokuwa na raia waoga sana?

4. Kati ya raia waoga kiasi na waoga sana ni wepi wenye manufaa kwa Taifa?

5. Hayati Nyerere alikuwa sahihi kutaka kulijenga Taifa la watu waoga kiasi na si watu waoga sana?
Ni kweli alikandamiza kiuchumi na kielimu makabila yaliyokuwa juu kabla ya uhuru na kuyanyanganya ushawishi ndo madhara tunayoyaona Leo ya uchawa na uoga uliopotiliza
 
Halafu huu uoga ukabatizwa jina amani. Unakuta watu anaishi maisha magumu huku viongozi wakichezea kodi zao na hawana la kuwafanya, kisha viongozi wanasifia hayo majoga kwa kuyapaka mafuta kwa mgongo wa chupa kuwa sisi watanzania ni watu wa amani, na tusiichezee amani yetu maana tutajuta tukiipoteza!
Uku wakitoa mifano ya nchi zenye machafuko ya kisiasa kama Somali,Congo (DRC),Sudan nk

Nyumbu wanatetemeka kwa hofu uku haki zao zikikandamizwa.
 
Back
Top Bottom