Haya yanayosemwa kuhusu Hospitali ya Mloganzila ni kweli?

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,352
Habari za wakati huu.
Niende kwenye mada moja kwa moja.

Jana nikiwa katika kijiwe flani hapa jijini kwa Makonda nilisikia watu wazima wakitoa malalamiko makubwa ambayo kiukweli yalinitisha.

Hoja zao zilihusu hospitali ya Mloganzila (ile branch ya Muhimbili National Hospital) iliyoko Kibamba, wale wazee walikua wakisikitika kuhusu ubora wa huduma za pale na gharama za matibabu kuwa ghari sana.

Wanasema ukipelekwa pale unaumwa uwezekano wa kupona unakua mdogo sana, ukinusurika kufa basi utakua unadaiwa mamilioni ya fedha, waliendelea kusema kwamba madaktari wa pale wengi ni wanafunzi (internship) hawana care kubwa wala uzoefu mkubwa hali inayopelekea cases nyingi kushindikana na wagonjwa kufa.

Hayo yalikua na mazungumzo ya wale wazee, nilisikiliza mazungumzo yao bila kuchangia wala kuonesha kama nawasikiliza stori zao lakini nilikua nafatilia kwa makini sana kutokana na unyeti wa suala lenyewe.

Mimi sijawahi kufika hospitali ya Mloganzila naishia kuona kibao chake pale barabarani tu, mliowahi kwenda kupata huduma au mlipeleka ndugu zenu hebu wekeni ukweli tusiojua tujue maana sisi sote ni wagonjwa watarajiwa.
 
Mwaka jana mwezi wa 10 Mama Mkwe wangu kafariki hapo Mloganzila baada ya kupata transfer toka Muhimbili. Alivyofika hapo hakuna matibabu ya maana yoyote aliyopata zaidi ya story za vipimo. Usemalo mkuu linaukweli mkubwa ndani yake.
 
Kumbuka tu pale ni hospitali ya rufaa na ukifika pale maana yake tatizo lako limeshindikana kote Hao ndiyo Madaktari bingwa hivyo wanapigania kukuokoa ukifariki ukiwa hapo ni sawa na askari aliyeokolewa uwanja wa vita akiwa na serious injuries akafariki ukiwa kwenye chopa unapelekwa hospitali.
 
Kumbuka tu pale ni hospitali ya rufaa na ukifika pale maana yake tatizo lako limeshindikana kote Hao ndiyo Madaktari bingwa hivyo wanapigania kukuokoa ukifariki ukiwa hapo ni sawa na askari aliyeokolewa uwanja wa vita akiwa na serious injuries akafariki ukiwa kwenye chopa unapelekwa hospitali.
Kwahiyo wanafunzi wanakuwa huru kujifunza kwenye mwili wa mgonjwa maana hakuna matumaini ya kupona.
 
Hii kitu nilipata wasiwasi toka wakati ule wa mwanzo badala ya kuifanya kuwa na hadhi zaidi ya hapo ilipo ila wamechaguliwa madaktari kutoka vitengo.
 
Jiulize viongozi wakubwa na matajiri wangapi wamefanyiwa referal ama kufia hapo? Kama wapo wanahesabika.
Kina Spika wanaenda India kwa mabilioni ya gharama na ndio maana mpaka leo wana kiburi cha kubwabwaja ovyo wakijiona miungu watu.
Kama wangepelekwa hapo leo tungekuwa tunaanza na neno 'Marehemu' kabla ya majina yao. Hivyo kwa kifupi uliyosikia ni kweli huduma hapo ni duni kama ilivyo kwingineko ndani ya nchi yetu tukufu.
 
Ukweli kuhusu mloganzira gharama za matibabu zipo juu mno kutokana na huduma wanazotoa ni ghari sana kuhusu vifo ni kweli vipo kwa kuwa wao hupokea wagonjwa walio kuwa na hari mbaya kiasi cha ndugu kukata tamaa madaktari mabingwa wapo pale ni zaidi ya wanao kuwepo mhimbili
 
Hata mimi nilikuwepo pale miezi michache iliyopita kwa lengo la kumuona mgonjwa. Kwenye gharama siwezi kusemea maana mgonjwa wangu ana bima ya afya. Kuhusu madaktari, nadhani kuna ka ukweli fulani ka uwepo wa madaktari wengi vijana ila ni vigumu kuwahukumu kama ni madaktari wanafunzi au hawana sifa stahili maana nimewaona wakitekeleza majukumu yao kama kawaida.
 
Habari za wakati huu.
Niende kwenye mada moja kwa moja.
Jana nikiwa katika kijiwe flani hapa jijini kwa Makonda nilisikia watu wazima wakitoa malalamiko makubwa ambayo kiukweli yalinitisha.
Hoja zao zilihusu hospitali ya Mloganzila (ile branch ya Muhimbili National Hospital) iliyoko Kibamba, wale wazee walikua wakisikitika kuhusu ubora wa huduma za pale na gharama za matibabu kuwa ghari sana.
Wanasema ukipelekwa pale unaumwa uwezekano wa kupona unakua mdogo sana, ukinusurika kufa basi utakua unadaiwa mamilioni ya fedha, waliendelea kusema kwamba madaktari wa pale wengi ni wanafunzi (internship) hawana care kubwa wala uzoefu mkubwa hali inayopelekea cases nyingi kushindikana na wagonjwa kufa.
Hayo yalikua na mazungumzo ya wale wazee, nilisikiliza mazungumzo yao bila kuchangia wala kuonesha kama nawasikiliza stori zao lakini nilikua nafatilia kwa makini sana kutokana na unyeti wa suala lenyewe.
Mimi sijawahi kufika hospitali ya Mloganzila naishia kuona kibao chake pale barabarani tu, mliowahi kwenda kupata huduma au mlipeleka ndugu zenu hebu wekeni ukweli tusiojua tujue maana sisi sote ni wagonjwa watarajiwa.
Habari kubwa ya hapo ni akinamama wanaojifungua huwa hawaruhusiwi kutoka mpaka walipe deni! Nalo wazazi wanalalamika kuwa ni kubwa mnomno.
 
JK Alijitahidi kutuletea Hospitali yenye Majengo mazuri lakini huduma zake ni mbovu hazielezeki.. Dokta anapita asubuhi kwa asubuhi.... Simshauri mtu yoyote kwenda hiyo Hospitali... Madokta wenyewe Wanafunzi...wapo Kwenye Field... Ni Changamoto...
 
kwa kweli jengo la hospitali hiyo ni zuri sana.... ila kama mgonjwa wako anahamishiwa pale toka hospitali nyingine haswa siku za mwisho wa wiki kwa kweli muombe Mungu tu.
 
Kwahiyo wanafunzi wanakuwa huru kujifunza kwenye mwili wa mgonjwa maana hakuna matumaini ya kupona.
Acheni kuamini maneno ya kusikia. Kwanza intern doctor au intern nurse hufanya kazi under supervision. Hawezi mfanyia mgonjwa kila kitu peke yake. Halafu intern si mwanafunzi bali kahitimu masomo na yuko mafunzoni kwa mujibu wa sheria. Mbona Muhimbili ndo yenye interns wengi kuliko hospitali yoyote Tz hamuisemi mmekomalia Mlongazila? Mnataka interns wajifunzie wapi? Mgonjwa akifa akiwa na specialist hamna shida ila akifia mikononi mwa intern intern kaua!!
Hebu waacheni vijana wetu wafanye kazi
 
Back
Top Bottom