ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,681
Isaac JK
Asante sana kwa ushauri wako wenye nia njema ya kujenga na kuimarisha harakati za mapambano ya ukombozi wa pili wa Mtanzania kutoka kwenye makucha ya mkoloni 'mjomba, shangazi, kaka, dada, rafiki, bibi, babu, mama, baba', walioko kwenye mwamvuli wa CCM!
Mtu akipitia andiko lako kwa umakini atabaini kuwa vitu ulivyoviandika viko very vague. Haijulikani hasa unataka kusema au kushauri nini. Mathalani vitu vyooooooooote ulivyoorodhesha hujasema vinawaangusha namna gani CHADEMA na namna gani ushauri wako ufanyiwe kazi. Lakini si mbaya, tutakujibu kwa mantiki hiyo hiyo iliyoeleweka kwenye ujumbe.
Lakini pia labda ni tabia yetu Watz kutopenda kutafuta taarifa kwanza kabla ya kusema, masuala ya media za CHADEMA, mfano tv, redio na gazeti, yameshajibiwa hapa mara kadhaa. Kuna masuala na hatua kadhaa za kupitia. Imeshaelezwa hapa, siku moja hadi nikaenda mbali nikasema watu wengine wanashangaza wanataka tuje tujadili mpango kazi na mkakati wa wa chama kwenye vyombo vya habari, kwa faida ya nani?
Takwimu sahihi za wanachama zimekuwaje? Malipo kwa watendaji wake yamekuwaje? Vitendea kazi kama magari, pikipiki, vipeperushi, vimekuwaje? Vitega uchumi vingine, vimekuwaje? Very vague, utaishia kupata majibu vague vile vile.
Chama cha mpito! Sikuwahi kufikiria mwanaCHADEMA makini anaweza hata kuwaza eti chama hiki ambacho kimeweza kuiweka kwenye kona CCM na serikali yake, kikiendesha harakati za ukombozi wa kifikra kwa miaka zaidi ya 20 mfululizo, kinaweza kuwa chama cha mpito.
Chama cha namna hiyo kinaweza kuwa CHADEMA kweli? Vyama vya mpito vingi tu tunavyoviona kwa matendo na maneno, bungeni, na nje kwenye mikutano ya hadhara na press conference, vikifanya kazi ya CCM...
Pasi na shaka, viongozi wa CHADEMA pamoja na wanachama wake makini, wanaotambua wajibu wao, wameendelea kukijenga chama hiki kwa ajili ya vizazi vilivyopita, vilivyopo na vijavyo, ndiyo maana daima kimejikita katika sera makini, mikakati endelevu na oganaizesheni thabiti, kuibua dhana za mabadiliko mapya ya kimfumo na kiutawala kwa ajili ya kuzungumzia maendeleo ya zaidi ya miaka 50 hadi 100 ijayo.
Nikushukuru tena Isaac.
Sehemu kubwa ya masuala ambayo umejaribu kushauri hapa, ama yako katika hatua mbalimbali za utekelezaji, mengine ni sehemu ya misingi ya uanzishwaji wa CHADEMA, hivyo imekuwa ni sehemu ya majukumu ya kila siku katika kuwatumikia Watanzania, zinaweza kuwa zinabadilishwa modus of operandi, kwa nia ya kuboresha, lakini lengo, dhamira na nia ikabaki pale pale.
Kitu kikubwa sana cha msingi, saidia kuwatia shime wanachama wenzako (kama nawe ni mwanachama) kushiriki katika mpango wa sasa wa kukiweka chama mikononi mwa wanachama. Masuala mengine mengi tu uliyoshauri hapa si lazima yafanywe kuanzia makao makuu, ungeweza hata kusaidia yafanayike katika ngazi ya msingi au tawi. Hivyo Isaac kama hujajiandikisha, nenda ukafanye hivyo kwenye msingi wako na ulipie kadi yako.
Bila shaka huko pia utapata fursa ya kushiriki vikao na kupata jukwaa murua la kupenyeza mawazo yako na kupata fursa ya kufuatilia na kusukuma utekelezaji wake.
Karibu.
Makene
0752 691569/ 0688595831
These guys are not serious.
Chama kina zaidi ya miaka 20 (ISHIRINI) tangu kianzishwe lakini swla muhimu kama kujipatia ofisi bado liko kwenye "hatua mablimbali za utekelezaji".
Hiki ndio chama kinachowalaghai wananchi kuwa kina uwezo wa kubadilisha hali ya maisha ya watanzania kwa miaka mitano, wakati chenyewe zaidi ya miaka 20 kimeshindwa hata kupata ofisi ya kujihifadhi.
Wajinga ndio waliwao...