Haya ndiyo yanayojiri nchini Iran

Haya ndiyo yanayojiri nchini Iran

Huwa nasikitika sana nikiona watoto wadogo wamefunikwa vichwa gubigubi katika hili jiji la Dar es Salaam. Sio haki na haikubaliki kabisa, ni mateso sana kwa mambo ambayo hata hawayaelewi.
#IRAN KILICHO NYUMA YA MAANDAMANO DHIDI YA HIJABU NCHINI IRAN.

Mnano tarehe 16 mwezi wa 9 mwaka 2022 kilitokea kifo cha bint Mahsa Amin

Amefariki akiwa katika kituo cha polis mjiji Tehran na akiwa mikononi mwa polisi wa maadili wa Iran

Kosa la bint huyu ni kutovaa hijabu katika maisha jumla( mitaani,sokoni ofisini, nk)

Kama uislamu unavyoamrisha kwa binti wa kiislamu aliyefikia Baleghe avae hivyo

Jambo hili limesababisha kuripuka kwa maandamano nchini Iran na kuibuka kelele kutoka nchi za Magharibi
zikishirikiana na mavuvuzela yao (vyombo vya habari na vyama vya haki za binadamu) kulaani na kupinga vikali tukio hili

Je kuna nini nyuma ya pazia?

Tutatupia jicho katika nukta kadhaa juu ya qadhia hii

1 Nchi za magharibi.
hawa ndio chanzo cha matatizo ulimwenguni kwa kuandaa matatizo kusudi na kujifanya kutoa utatuzi.

Hawa ndio wapishi wa machafuko yote duniani kisha hujifanya kuwahi kwa mbele na kujifanya kuja na utatuzi

hivyo hawana ila unafiki tu, na pia huchagua matatizo ya kupigia kelele na mengine hukaa kimya cha mfu

Tumeshuhudia tukio kama hili hili la hijabu nchini India

mabinti wa kiislamu kupigwa na kuzuiliwa kuingia darasani na wakilazimishwa kuvua hijabu

Hawa wote walikaa kimya,

Hatukusikia kelele za haki za binadamu, uhuru binafsi, na elimu kwa mwanamke, vyote hivi havikusikika

2, #HAKI_ZABINADAM, Hawa hawana ila unafiki tu,

wao wanasubiri maagizo toka kwa mabwana wao tu, ndio hupiga kelele.

wana weza kupiga kelele juu ya kuchinjwa mende mwezi mzima lakini wakakaa kimywa juu ya kuchinjwa binadamu 5000 mbele ya macho yao.

Hawa ni mavuvuzela tu wanapaza sauti za mabwana wao na sio kutetea haki za wanadamu.

bint mwenye umri chini ya miaka kumi na nane akilazimishwa na wazazi wake kuolewa watapiga kelele mwaka mzima kwamba amepokonywa haki yake.

Lakini binti huyo huyo akitaka yeye mwenyewe kwa ridhaa yake kuolewa lakini wazazi wakamzuia hawafungui mabakuli yao kwamba kanyimwa uhuru wake na maamuzi ya mwili wake

waislamu wangapi wamekamatwa na kupotea duniani?
wao kimya cha mfu,

3 SERIKALI YA IRAN

Je ni kweli serikali hii inashida na uislamu? Hivyo inaumwa na hijabu vazi la kiislamu?

Ni sheria ngapi za kiislamu Iran haitaki hata kuzisikia?

Imekamata waislam wangapi na kuwa uwa wanao taka kweli sheria za kiislamu?

Sheria za Iran za uchumi, siasa, jamii, utawala, nk zote sio za kiislamu bali ni za kibepari

Katiba ya Iran haielewiki msingi wake ni upi

Imetambua kukusanya mambo yenye kugongana kiitikadi.

1 uislamu.
2 democrassia.
3 umajusi.

Yote hayo yamo ndani ya katiba ya Iran yametambuliwa

Hivyo haikuwa ajabu kwa serikali ya Iran kuitambua rasmi siku tukufu ya ya kimajusi ya kuabudu moto NAIRUZ na kuipa hishma kwakutoa likizo kwa watumishi wa serikali ili wakasherehekee ibada ya kuabudu moto

Iran ili saidiana na Amerka kuuwa waislamu Afghanstan mwaka 2001

Ilishirikiana na Urus kuuwa waislamu Adhribjan mwaka 1994 na na pia 2021 na Armeniya

Ina chinja waislamu Yemen ikilitumia genge lake la kigaidi Huthy

Imetelekeza Aqsa ikinajisiwa na mayahudi miaka zaidi ya 40.

eti hufanya maandamano tu dhidi ya mayahudi yanayo ishia kujipongeza kwa sufuria za pilau jioni ya siku ya Qudus day

Nchi hii ni Sawa na Saudia.

zimetengenezwa na wamagharibi kuvunja uislamu

ila zikaambiwa wachukue sheria mbili tatu za kuwalazia waislamu

na hasa sheria zenye kuwahusu wanawake zaidi

Hivyo wakatilia mkazo hijabu, na vikwazo vingi na kadhaa kwa wanawake

Lengo nikutoa picha ya hadaa kwamba ni nchi zenye kufuata uislamu

Lakini kwa wamagharibi kwao ni mtego watakao utumia kupenyezia fikra zao za uhuru

na kupiga kelele za ukandamizaji ili ifunguke milango yote ya uchafu wa kimagharib

hivyo wamagharib wakawaachia watawala wa Saud na Iran kushikilia sheria ya hijabu kwa ukali na mabavu ili muda muafaka ukifika watumie kama cheche ya kuripua na kuhitimisha kuingiza uchafu wao woote

Na Saudia si mbali, na mripuko huo utakuwa mbaya zaidi kuliko ya Iran.
wao watatembea uchi kabisa kama walivyo zaliwa kwani Kuna fukuto kubwa sana la chini kwa chini linasimamiwa na mwana mflame mwenyewe wa Saudi na masheikh wanao jaribu kuligusa wanakamatwa na kupotezwa mimbari zimebakia kwa wale masheikh wanao jiliza wakimuona mtu amenyoa ndevu

4 WAANDAMANAJI

Si kweli kwamba wana andamana kwa sababu ya kupinga kuuliwa tu kwa binti huyu

Bali hawa waandamanaji hawaungani katika sababu za kuandamana.

wamo makundi kadhaa na sababu kadhaa

A.chuki dhidi ya serikali ya Iran hivyo wana chukua fursa hii kutoa duku duku lao

B .ugumu wa maisha

C. Vikundi vya kipagani vya kupinga uislamu.

ambayo vimekuwa vikifanya kazi kwa siri na kwa miaka mingi sana, vikijikusanya na kujijenga,

vikitumia maneno ya kuhadaa watu kama haki za binadamu, kupinga mfumo dume, ukatili wa kijinsia, haki za mashoga, nk

Na mapagani hawa wanafanya kazi hii Saud na Arabuni kote kwa ujumla.

Kazi hii wana ifanya kwa juhudi kubwa sana, wakimiminiwa mamilioni na nchi za kimagharibi.

na serikali za Iran Saud nk zina jua na hazichukui hatua zozote kama ilivyo Afrika.

makundi haya ni mengi na kwasasa yanaanza kujitokeza kidogo kidogo bila haya wa soni wakitaka uchafu wote wa kimagharibi uhalalishwe.

Hivyo wandamanaji Iran si chuki tu dhidi ya mauaji bali ni chuki dhidi ya uislamu na alama zote za kiislamu ikiwemo hijabu adhana nk

Kwani hijabu na adhana mathalani, ni alama kubwa sana katika jamii husika kwamba hapa uislamu upo au haupo.

Hivyo maandamano ya Iran sio ya kupinga dhulma aliyo fanyiwa binti huyu bali ni ya kupambana na ishara za dini na kuingiza umafharibi

Saud na Iran hazikuwa andaa wanawake wa kiislam kuvaa hijabu kifikra na ki ikhlasi,

bali kwa nguvu ya sheria na ukali wa askari maalumu.


Hili ni tatizo kubwa sana kwani ni bomu ambalo muda wowote lina ripuka

Waandamanaji wanachoma hijabu, je sheria ya hijabu ni ya Allah au ya serikali ya Iran?
Ni kweli hata hili hawalijui?

Ikiwa hawalijui, ni dhahiri walivishwa kwa nguvu na sio kifikra na khiyari ya kufahamu kwamba dini ime amrisha

Na ikiwa wanajua basi chuki si dhidi ya mauaji bali ni dhidi ya uislamu

Hili ni sawa na uvaaji wa hijabu shuleni Tanzania.

mabinti wanavaa vitambaavya kichwani kwa muda wa miaka 7 mpaka 13 akitoka shule tu au kwenda chuo kikuu mitaani hijabu hazionekani na vyuoni zinapotea au kupungua licha ya kwamba ni hijabu ambazo hazijakidhi vigezo

Na hali hii ipo mpaka kwenye shule zinazojiita za kiislamu.

watoto wanavaa hijabu kama amri za kishule na uniform tu na shule hizi zimemeshindwa kuwavisha watoto Hawa hijabu kama dini na anri ya Allah

na ndio sababu hatuoni athari ya shule hizi katika hijabu mitaani si kwambii madili mengine

5 MASHEIKH
ilitarajiwa wale masheikh wakuhimiza ndevu na kupinga khitma na maulidi,au wale wa kupenda maulid vipenzi vya mtume(عشاق النبي) au wale wenye kujiliza kwa mapenzi ya nyumba ya mtume, na wale wenye kutoa nasaha laini laini za kutamanishana pepo kwa mambo madogo madogo tungewaona wakitoa kauli zao na misimamo yao kama waislamu na wakitupilia mbali misimamo ya madhihab zao

Ajabu wapo kimya cha mfu juu ya haya

Na walio zungumza walizungumza kwa taasubi zao za kimadhihab tu na si msimamo safi wa kiislamu kwa kuangazia pande zote kwa upana

By Sheikh Ramadhani Moshi
 
Nakubalina na wew Sheria za dini inabidi watu wazifwate Kifkra zaidi kuliko kulazimishana pia tunasahau kua Kuna Technology utamkazata mtu asizini lakini akiwa chumbani kwake atawasha simu ataangalia watu wakizini unachokua umemsaidia nin,haya utawambia watu mtaani wasivae nusu uchu mtu akikaa ndani anawasha simu anaangalia vizuri wanawake kibao wapo uchi Sasa unakua umefanya kitu gani
 
Wametumia sana dini kuwalaghai wajinga. Sasa welevu wameongezeka na hawatakubali tena kuburuzwa
Mwili wa mtu mwingine, mavazi anajinunulia yeye mwenyewe. Bado pia namna ya kuvaa na kuishi umpangie, huu ni upuuzi.
 
Ww km ni shekhe basi kazi ipo maana umejaza chuki tu ndo maana watu wanajilipua kwa upuuzi km haya mtu auliwe na askari wenu maandamano myafanye nyinyi lawama mnampa jirani hizi si ni akili za mende
 
Waislamu wote wamekaririshwa adui wao wakwanza ni Westerners nadhani hii fikra duni itawasumbua sana.

Shida ipo kwao na mafundisho yao ya dini..dini/imani hailazimishwi ni hiyari ya mtu na mola wake.

Vazi la hijabu au sheria yoyote ile hasa za kidini sio kulazimishana ni hiyari baada ya mtu kuwa na uelewa sio kumtungia sheria kandamini kulazimisha.

Dunia imebadilika sana..usipo kubali kubadilika mabadiliko yatakubadilisha.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Upuuzi sana yaani
Mwanamke amebanwa saana kwenye dini ya kiislamu.

Wengi wao hata ndoa za kiislamu wanazichukia. Mwanamme ana amri ya kuwa na wake wanne ila mwanamke kuwa na wanaume zaidi ya mmoja ni kosa.

Kwenye mavazi umtenge, ibada umbague, mazishi umbague n.k
 
Back
Top Bottom