Hawajaenda!.......

Hawajaenda!.......

Ngokongosha

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2011
Posts
3,400
Reaction score
7,610
_ Kwani si huko ukerewe ndiko walikopata Mbunge, mbona viongozi wa kitaifa wa chadema hawajaenda, wamebaki kubwabwaja kwenye mitandao na vyombo the habari, Je wameshindwa kupeleka mwakilishi?.

Aaah nimekumbuka huu msiba haukuwa na umuhimu sana ukilinganisha na wa mama yake Sugu. Au labda waliokufa wengi ni CCM?, Ati wamejuaje kwamba ni wa CCM?

Hapana, nimeambiwa msiba huu hauna Kiki ndio maana hawajaenda.
Aahhggg!!! Wangeenda Tu wakasema ajali imesababishwa na magufuli tungewaelewa Tu, mbona kule Kwa mama yake Sugu walisema magufuli ndio chanzo wa kifo cha mama Yule tukawaelewa!

Aaah nimekumbuka, kivuko kimezama Kwa hiyo hakuna usafiri wa kuwafikisha kule, lakini je wengine wamewezaje kwenda?.

Poleni ukerewe, poleni ukara na bugolora,,.... Ila hawajaja pamoja na kwamba mliwapa Mbunge.
Sijui labda watakuja msiba ukiisha,
Maana nimesikia wanapanga mikakati Fulani kwenye hoteli moja hivi.

Poleni Ukerewe
Poleni Mwanza
Pole Tanzania.
 
Back
Top Bottom