TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Nyote mtakubaliana nami kuwa washabiki wa kisiasa (political commentators) ni watu muhimu katika taifa lolote lile katika kufanyia uchambuzi mambo mbalimbali ya kisiasa na wakati mwingine kijamii katika nchi au bara husika.Katika hawa wako waandishi wa habari (waliofuzu taaluma hiyo na hata wale ambao hawajafuzu kimsingi),viongozi wa dini (hasa zile dini zisizo na wafuasi wengi) ,viongozi wa asasi za kiraia na wengineo wafanyao kazi hiyo.Leo hii ukiamka na kwenda kununua gazeti,kwenda uwanjani kupata burudani na kwingineko watu hawa ndo tunakutana nao.Wapo wanaozungumza mambo ya msingi na wapo ambao ukitafakari wanachosema unapata ugumu kuelewa kama kweli wanatumia vizuri akili zao katika kutafakari mambo.Wapo wengine huenda mbele zaidi na kujiita watafiti wa mambo huku kile wanachokiongea kikiwa hakiendani kabisa na taaluma hiyo ya utafiti.Tanzania ya leo imegubikwa na chuki katika makundi ya watu wa kipato cha juu ambao nao hawa wametafuta support toka kundi la watu wa kipato cha kati (vijana,wasomi na wafanyabiashara).Hawa nao wametafuta pia support kwa kuwarubuni watanzania wa kipato cha chini walio wengi kujiunga nao kupitia kila aina ya propaganda.Wengine wanawanyonya kwa kujiita manabii na wachungaji huku wakianzisha makanisa na madhehebu lukuki,wakijineemesha wao na kujiita wajasiriamali.Wengine wameingia katika kundi la wanasiasa,hawa wanajiita wakombozi (inawezekana wapo wenye nia),hawa wanatumia kila aina ya unyonge na matatizo waliyo nayo wananchi kama ngazi ya kupandia kwenye mafanikio yao binafsi na vikundi vyao(muda utasema).Watu hawa kama nilivyosema awali,wana lengo la kuona yale wanayotaka yanatimia.Kama mwanafunzi anapodhamiria kufaulu mtihani kwa gharama yoyote ile.Wapo watakaosema uongo,watakaolia na hata wapo watakaosema wameshushwa na Mungu wakikomboe kizazi.Yote katika yote napenda kuwaasa Watanzania wenzangu wenye nia njema na taifa kutafakari yale ambayo tunayapitia leo,kesho na siku zijazo.Kujua nafasi ya kila mmoja wetu na kujua kwamba siasa na uongozi ni zaidi ya kile ambacho tunakisikia.Umoja wetu na mshikamano wetu si kitu cha msimu.
Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Tanzania