DUBULIHASA
JF-Expert Member
- Nov 26, 2016
- 3,563
- 5,957
Wakuu habari za week end. Natumaini wote ni wazima na mnaendelea na majukumu ya kila siku. Leo ningependa Ku share kidogo mawazo yangu kwenye mchezo wetu Wa soka tuupendao sana. Huu mchezo unatufanya tufurahie huu ulimwengu wetu japo tuna changamoto nyingi zinazotukabili kila siku.
Leo ningependa niwazungumzie kidogo wanakabumbu ambao kiukweli kabisa mimi kama shabiki wa soka nawapenda sana kutokana na uwezo wao LAKINI kiukweli kabisa mi naona wanapewa sifa sana kuzidi uwezo wao. Naomba nieleweke vizuri hapa; ni kwamba sio kwamba hawana uwezo Ila ukweli nionavyo Mimi ni dhahiri sifa zao zimezidi mno uwezo na ufundi Wa kulicheza gozi. Ifuatayo ni orodha ya wanakandanda watano(5) wanaosifiwa zaidi au kwa kizungu tunaita "OVERRATED" kuliko uwezo Wa ukweli walionao
1.Neymar Jr, huyu ni mwanasoka ambae wachambuzi, mashabiki na wadau wengi wa soka wanamchukulia kama mchezaji Wa tatu kwa ubora duniani baada ya Lionel Messi na Christiano Ronaldo. Ukweli ni kwamba huyu Barobaro Wa kibrazili ni mchezaji nzuri Ila not to that extent. Kwa Mimi naona huyu mtoto kikubwa alichojaliwa na Mungu ni kwamba anajua kuuchezea mpira, kutengeneza mashambulizi na uwezo Wa kuweza kutoa assists za kufunga na pia yeye mwenyewe kufunga. Kikubwa kinachowadanganya watu kumuona ni mchezaji bora ni ile kucheza mpira Wa "swagger" au Mpira unaovutia a.k a Samba. Kwa kweli hana kitu kigeni cha kumfanya aonekane bora kuliko Alexis Sanchez pamoja na Eden Hazard. Huyu dogo pia ameonekana bora zaidi baada ya kucheza pamoja na mafundi akina Lionel Messi pamoja na Suarez pale Barcelona. Asipocheza timu moja pamoja na wakali huishia kuzurura tu uwanjani mfano mkubwa game ile ya majuzi dhidi ya Real Madrid. Wengi wanadai eti anajua kunyumbulika, kwani kunyumbulika ni kila kitu katika soka? Mbona Coutinho ananyumbulika pia. Kama kunyumbulika mbona hata huyu Shiza kichuya Wa hapa kwetu Tanzania pia ananyumbulika. Nimekuwa nikishangaa sana Neymar alivyowekwa kama mchezaji Wa Tatu kwa ubora nyuma ya Messi na Ronaldo kwenye Ballo'n dor 2015 na 2017.
2.Paul Pogba, huyu jamaa huwa pia anapaishwa sana. Inashangaza Manchester united walimsajili kwa pesa nyingi sana kutoka Juventus wakati huyu charii ni Wa kawaida kabisa. Zaidi ya fashion za nywele na kutembea kwa madaha sijaona mapya na mageni kutoka kwake. Wanaita eti box to box midfielder ambae anaweza akaipush timu hatimaye kupata magoli. Midfielder gani huyu anapata sifa za bure, hivi watu wamekaa wakafuatilia shughuli aliyokua akiifanya fundi Zinedine Zidane Zizzou, hivi nani hakumheshimu Steven Gerrard? Nani hakumvulia kofia Frank Lampard? Kama haitoshi sidhani kama kuna mtu ashawahi kuwa na Mashaka na Paul Scholes. Kuna viungo wengi Wa miaka ya hivi katibuni sijawahi kuwatilia shaka iwe defensive au holding midfielder. Sina Mashaka na attacking au sijui kuna wengine wanaitwa all round midfielders. Sina Mashaka na Pirlo, sina Mashaka na Iniesta na wala sina Mashaka na Xavi Hernandez. Sijawahi kuwa na Mashaka na Ngolo Kante na isitoshe sina Mashaka kabisa na mbishi Wa Juventus ambae Mimi nampenda kuliko kiungo yoyote duniani, si mwinginr Bali ni mwamba Alex Vidal. Kwa nini niwe na Mashaka na Pogba peke yake?
3.Mesut Ozil, huyu ni moja ya mijitu milegevu na mivivu sana kwenye Soka. Wengine watakuambia the man is so "creative", creativity without hard working is non sense. Huyu jamaa huwa anasubiri wamletee Mpira mguuni ili yeye aweze ku create. Huyu ni kama mwanamke, yeye asipowezeshwa basi yeye hawezi. Ozil kila mda yupo bored, assipokuwa disappointed basi ujue amewezeshwa.
4.Zlatan Ibramovic, huyu jamaa anapaishwa mno kuliko uwezo wake binafsi. Mwili wake mkubwa uliojengeka kikakamavu kutokana na mazoezi kumemfanya watu wampende sana. Kwa miaka mingi amekuwa akifanywa mchezaji bora sana duniani na kufikia kipindi kuwekwa kundi moja na Messi na Rinaldo. Dunia ya soka inamuona mtu special sana wakati uwezo wake hauwazidi wanasoka kama Didier Drogba, Samuel Etoo, Thiery Henry pamoja na Radamel Falcao japo amecheza soka kipindi kimoja na hao jamaa pia kwa uwezo sawa. Nadhani huyu jamaa anapaishwa sana kwa sababu amecheza timu nyingi bora na kubeba nazo vikombe vingi.
5. Karim Benzema, huyu striker wakati mwingine mi huwa nashangaa kwa nini anaendelea kuchezea Real Madrid. Uwezo wake ni mdogo sana sijapata kuona, Mara nyingine mashabiki Wa Madrid wanapomzomea naona ni sawa japo sio vizuri. Huyu jamaa inashangaza, inakuwaje striker namba 9 unamaliza msimu Wa ligi na magoli kumi, Mara Tisa, nane, saba. Akijitahidi sana basi atafunga kumi na tano. Hili lichezaji huwa linanishangaza sana, yaani muda wote yeye ni kumu accommodate Ronaldo ili afunge. Sasa inafikia kipindi mi huwa najiuliza HIVI HUYU JAMAA NI STRIKER, MIDFILDER AU PLAYMAKER? Anataka avunje historia kwa striker namba 9 kuwa KING OF ASSISTS. Nilikuwa nashangaa sana kipindi forward line partnership ya MSN(Messi, Suarez, Naymar) kuilinganisha na forward line ya BBC(Bale, Benzema, Cristiano Ronaldo). Kwenye BBC ni yeye ndio alikuwa anawaangusha na kushindwa dhidi ya MSN kwa sababu yeye hawezi kufunga magoli. Huyu Benzema Wa Madrid na yule Wa kipindi cha ligi ya ufaransa ni Benzema wawili tofauti. Tukitaja strikers bora zaidi duniani huwezi liona jina lake. Haya twende Luis Suarez, Pierre Aubameyang, Harry Kane, Robert Lewandowski, Gonzalo Higuain, Sergio Aguero, Edson Cavanni. Ona sasa jina lake halipo japokuwa ndio striker namba 9 Wa Real Madrid.
NI HAYO TU WAKUU KAMA UNABISHA BASI BISHA KWA HOJA KWA KUWA HAYO NI MAWAZO YANGU NA SIO LAZIMA TUFANANE.
Leo ningependa niwazungumzie kidogo wanakabumbu ambao kiukweli kabisa mimi kama shabiki wa soka nawapenda sana kutokana na uwezo wao LAKINI kiukweli kabisa mi naona wanapewa sifa sana kuzidi uwezo wao. Naomba nieleweke vizuri hapa; ni kwamba sio kwamba hawana uwezo Ila ukweli nionavyo Mimi ni dhahiri sifa zao zimezidi mno uwezo na ufundi Wa kulicheza gozi. Ifuatayo ni orodha ya wanakandanda watano(5) wanaosifiwa zaidi au kwa kizungu tunaita "OVERRATED" kuliko uwezo Wa ukweli walionao
1.Neymar Jr, huyu ni mwanasoka ambae wachambuzi, mashabiki na wadau wengi wa soka wanamchukulia kama mchezaji Wa tatu kwa ubora duniani baada ya Lionel Messi na Christiano Ronaldo. Ukweli ni kwamba huyu Barobaro Wa kibrazili ni mchezaji nzuri Ila not to that extent. Kwa Mimi naona huyu mtoto kikubwa alichojaliwa na Mungu ni kwamba anajua kuuchezea mpira, kutengeneza mashambulizi na uwezo Wa kuweza kutoa assists za kufunga na pia yeye mwenyewe kufunga. Kikubwa kinachowadanganya watu kumuona ni mchezaji bora ni ile kucheza mpira Wa "swagger" au Mpira unaovutia a.k a Samba. Kwa kweli hana kitu kigeni cha kumfanya aonekane bora kuliko Alexis Sanchez pamoja na Eden Hazard. Huyu dogo pia ameonekana bora zaidi baada ya kucheza pamoja na mafundi akina Lionel Messi pamoja na Suarez pale Barcelona. Asipocheza timu moja pamoja na wakali huishia kuzurura tu uwanjani mfano mkubwa game ile ya majuzi dhidi ya Real Madrid. Wengi wanadai eti anajua kunyumbulika, kwani kunyumbulika ni kila kitu katika soka? Mbona Coutinho ananyumbulika pia. Kama kunyumbulika mbona hata huyu Shiza kichuya Wa hapa kwetu Tanzania pia ananyumbulika. Nimekuwa nikishangaa sana Neymar alivyowekwa kama mchezaji Wa Tatu kwa ubora nyuma ya Messi na Ronaldo kwenye Ballo'n dor 2015 na 2017.
2.Paul Pogba, huyu jamaa huwa pia anapaishwa sana. Inashangaza Manchester united walimsajili kwa pesa nyingi sana kutoka Juventus wakati huyu charii ni Wa kawaida kabisa. Zaidi ya fashion za nywele na kutembea kwa madaha sijaona mapya na mageni kutoka kwake. Wanaita eti box to box midfielder ambae anaweza akaipush timu hatimaye kupata magoli. Midfielder gani huyu anapata sifa za bure, hivi watu wamekaa wakafuatilia shughuli aliyokua akiifanya fundi Zinedine Zidane Zizzou, hivi nani hakumheshimu Steven Gerrard? Nani hakumvulia kofia Frank Lampard? Kama haitoshi sidhani kama kuna mtu ashawahi kuwa na Mashaka na Paul Scholes. Kuna viungo wengi Wa miaka ya hivi katibuni sijawahi kuwatilia shaka iwe defensive au holding midfielder. Sina Mashaka na attacking au sijui kuna wengine wanaitwa all round midfielders. Sina Mashaka na Pirlo, sina Mashaka na Iniesta na wala sina Mashaka na Xavi Hernandez. Sijawahi kuwa na Mashaka na Ngolo Kante na isitoshe sina Mashaka kabisa na mbishi Wa Juventus ambae Mimi nampenda kuliko kiungo yoyote duniani, si mwinginr Bali ni mwamba Alex Vidal. Kwa nini niwe na Mashaka na Pogba peke yake?
3.Mesut Ozil, huyu ni moja ya mijitu milegevu na mivivu sana kwenye Soka. Wengine watakuambia the man is so "creative", creativity without hard working is non sense. Huyu jamaa huwa anasubiri wamletee Mpira mguuni ili yeye aweze ku create. Huyu ni kama mwanamke, yeye asipowezeshwa basi yeye hawezi. Ozil kila mda yupo bored, assipokuwa disappointed basi ujue amewezeshwa.
4.Zlatan Ibramovic, huyu jamaa anapaishwa mno kuliko uwezo wake binafsi. Mwili wake mkubwa uliojengeka kikakamavu kutokana na mazoezi kumemfanya watu wampende sana. Kwa miaka mingi amekuwa akifanywa mchezaji bora sana duniani na kufikia kipindi kuwekwa kundi moja na Messi na Rinaldo. Dunia ya soka inamuona mtu special sana wakati uwezo wake hauwazidi wanasoka kama Didier Drogba, Samuel Etoo, Thiery Henry pamoja na Radamel Falcao japo amecheza soka kipindi kimoja na hao jamaa pia kwa uwezo sawa. Nadhani huyu jamaa anapaishwa sana kwa sababu amecheza timu nyingi bora na kubeba nazo vikombe vingi.
5. Karim Benzema, huyu striker wakati mwingine mi huwa nashangaa kwa nini anaendelea kuchezea Real Madrid. Uwezo wake ni mdogo sana sijapata kuona, Mara nyingine mashabiki Wa Madrid wanapomzomea naona ni sawa japo sio vizuri. Huyu jamaa inashangaza, inakuwaje striker namba 9 unamaliza msimu Wa ligi na magoli kumi, Mara Tisa, nane, saba. Akijitahidi sana basi atafunga kumi na tano. Hili lichezaji huwa linanishangaza sana, yaani muda wote yeye ni kumu accommodate Ronaldo ili afunge. Sasa inafikia kipindi mi huwa najiuliza HIVI HUYU JAMAA NI STRIKER, MIDFILDER AU PLAYMAKER? Anataka avunje historia kwa striker namba 9 kuwa KING OF ASSISTS. Nilikuwa nashangaa sana kipindi forward line partnership ya MSN(Messi, Suarez, Naymar) kuilinganisha na forward line ya BBC(Bale, Benzema, Cristiano Ronaldo). Kwenye BBC ni yeye ndio alikuwa anawaangusha na kushindwa dhidi ya MSN kwa sababu yeye hawezi kufunga magoli. Huyu Benzema Wa Madrid na yule Wa kipindi cha ligi ya ufaransa ni Benzema wawili tofauti. Tukitaja strikers bora zaidi duniani huwezi liona jina lake. Haya twende Luis Suarez, Pierre Aubameyang, Harry Kane, Robert Lewandowski, Gonzalo Higuain, Sergio Aguero, Edson Cavanni. Ona sasa jina lake halipo japokuwa ndio striker namba 9 Wa Real Madrid.
NI HAYO TU WAKUU KAMA UNABISHA BASI BISHA KWA HOJA KWA KUWA HAYO NI MAWAZO YANGU NA SIO LAZIMA TUFANANE.