Hawa ndio wanaokula mema ya Rais Magufuli

Hawa ndio wanaokula mema ya Rais Magufuli

Mimi najiuliza saana zamani watumishi wa umma walikuwa wanapata fedha mbali ya mshahara ni kutokana na Semina pamoja na masurufu ya safari za ndani na nje kwa kada zote.

Sasa hivi naona wanaoathirika ni kada ya kati na chini maana kwao semina zimefutwa pamoja na safari lkn viongozi wa ngazi za juu muda wote wako safarini wakipishana mikoa toka mkoa mmoja na mwingine.

Hivi mafuta ,vipuri vya magari masurufu ya safari si ndo kikundi Fulani kinachofaidika pia viongozi nao wazuiwe kusafiri wakae maofisini watendaji ndo wasafiri na kuwaletea viongozi mrejesho.

Hivi sasa kila waziri yuko kwenye kona ya mkoa Fulani tofauti ya JK ili kuwa nje ya nchi na watawala wake, JPM ndani ya nchi na watawala wake.

Mhhhhhhhhh watulie ofisini vipuri,mafuta na masurufu yetu wanayateketeza peke yao.
 
Mkuu,soko la mbaazi liko wapi nikauze zangu? Mwaka huu tumepata pigo kubwa wakulima wa mbaazi. Ni maumivu makali ya hasara kubwa. Mbaazi zimetubwaga na kutupoteza. Maumivu!
Yaani upo tayari kuibiwa tanzanite mradi upate pa kuuzia mbaazi?
 
Mkuuu akili huna....!!! Hujawahi kufanya biashara yoyote hata kilimo hujui...kaaa kimya..!!
Mmachinga atamuuzia nani kama wateja wake hawana pesa hata wakimruhusu apange bidhaa zake hadi ikulu...!! Mkulima amenufaika hivi...pembejeo ziko wapi??...bajeti ya mbolea imeongezwa sh.ngapi?? Wapi kuna soko la uhakika hasa mazao ya biashara..!! Mazao ya chakula kila siku yanaporomoka bei!!!?? Unafikiri production cost ikiwa kubwa mkulima ananufahika vipi???
Viazi mbeya wanauza kwa bei ya hasara kila siku wanalalamika kukosa wateja na hii inasababishwa na kudorora kwa uchumi...!!!
Nenda ufipa
 
Wenye kazi na shughuli zao halali wamerihika na wanafurahia utendaji mzuri wa serikali. Wanaopiga kelele ni wale mafisadi, wezi, wakwepa kodi na majipu waliokuwa wanalipwa mishahara hewa. Wengine ni waliofoji vyeti vya taaluma.

Serikali ya JPM haihitaji wanyonyaji na wapiga dili. Ni Kazi Tu.
Naona umeamua kujipa kazi ya cocochannel.....hongera mkuu
 
Wenye kazi na shughuli zao halali wamerihika na wanafurahia utendaji mzuri wa serikali. Wanaopiga kelele ni wale mafisadi, wezi, wakwepa kodi na majipu waliokuwa wanalipwa mishahara hewa. Wengine ni waliofoji vyeti vya taaluma.

Serikali ya JPM haihitaji wanyonyaji na wapiga dili. Ni Kazi Tu.
Hiyo biashara wanaifanyia marekani hivi umeongea kwa kutafiti au umeongea kuongeza idadi ya comments
 
Kuacha wamachinga kutandaza vitu barabarani leo ni sifa ya kujivunia?Mkulima anayelipishwa road licence wakati wilaya nzima haina barabara hata moja ya lami?
 
Mi nilidhani kuna soko la mazao ya kilimo na mifugo la uhakika limepatikana kumbe maneno,bora kodi ingebaki lakin tutafutiwe soko la uhakika la mazao yetu.
 
Mkuu,soko la mbaazi liko wapi nikauze zangu? Mwaka huu tumepata pigo kubwa wakulima wa mbaazi. Ni maumivumakali ya hasara kubwa. Mbaazi zimetubwaga na kutupoteza. Maumivu!
Poleni naskia mbaazi mnapiga nazo picha tu ...
Any way labda serikali watanunua toka Kwa wakulima

Ova
Polw
 
Back
Top Bottom