Hawa ndio wakeraji barabarani...!

sijui nini

JF-Expert Member
Sep 29, 2010
2,553
1,285
Nimeamini siku hizi barabarani wenye magari ni wengi kuliko madereva....Hizi tabia zina kera sana barabarani..kama na wewe huwa unafanya haya barabarani basi jua unakera wenzako:

1. Unakuta barabara ya njia(lanes) mbili halafu mtu anaendesha gari katikati ya hizo lane mbili afu unaenda taratibu..hueleweki upo kushoto au kulia...kagari kenyewe kadogo sasa si ukae lane moja uwapishe wengine...?

2. upo njia kuu unakuja yeye anataka kuingia na anakuona kabisa lakini na yeye anaingia tu afu anaanza kutembea taratibu wakati mtu unaharaka zako...sasa si ungenisubiri nipite..si ndo sheria..kama uliona utawahi basi tembea mwendo wa kueleweka au mpishe mwenzako aendelee za safari zake na wewe uendelee na mwendo wako mdogo..au unaona raha kufuatwafatwa matakoni...??

3.haya nimeamua kuvumilia mwendo wako mdogoo wee nimepata nafasi nataka niku overtake..naanza kukupita na wewe unaongeza mwendo...iiish!! unaakili wewe..??nikipunguza nikuache utangulie unaenda kidogo unarudia mwendo wako ule ule..kwani nashindana na wewe jamaa..

4. saa kumi na mbili jioni hata giza halijaingia vizuri tena unapita katikati ya mji mtu ameshawasha taa FULL LIGHTs??? hivi unajua maana ya hizo taa? unawamulika wenzako..wanakuonyeshea na ishara kwamba unawamulika wewe walaaa..kwani unapita porini?? kuwa mstaarabu..au ndo hata hizo taa hujui kwanini zinawaka tofauti tofauti unavyowasha??

5. barabara nyembamba..mbele yako kuna msukuma mkokoteni tena anajitahidi kweli kusukuma kwa nguvu ili asiweke foleni ila wewe bado tu na mahoni yako..piii piii piii..sasa we unataka apae?? ustaarbu kitu cha bure..au unaona kuna foleni labda mbele kabisa kuna lori linakwenda taratibu na kwa kulipita hamna wewe unakuja tu huko unaanza kupiga mihoni yako..sasa unataka kitokee nini...

6.kisa wewe una gari basi waendesha pikipiki,(kumbuka si kila mwendesha pikipiki ni bodaboda), baiskeli na wapita kwa miguu kwako hawana haki ..kila sehemu wewe ndo unajifanya una haki..unakuta round about kuna mtu wa pikipiki au baiskeli anakatisha na wewe unaingia tu ...kisa wewe una gari..?? au wewe ndo unaingia njia kuu na kuna baiskeli inakuja au pikipiki na umeiona kabisa ila wewe unaingia tu... sheria huijui..hata ustaarabu pia??

7. barabara inapita katikati ya mtaa..kuna watoto kibao wanakatiza na kibao cha spidi kipo ila mtu unakimbia spidi 100...??bure kabisa...


8. ongezea na wakwako wanaokukera...
 
Last edited:
Kukereka na gari ya mwenzio hujui alipolipata hilo ni jipu
 
Kukereka na gari ya mwenzio hujui alipolipata hilo ni jipu
kukera wenzako kisa wewe una gari ni zaidi ya jipu... afu mimi nna gari na wewe unagari...kila mtu akiamua kujionyesha humo barabarani kutapitika?? zamani ndo ilikuwa dili sio skuizi mkuu..
 
kuna madereva na wasogeza magari

mabraza men, masister du, wakishua ndio zao hizo cha kuchekesha sasa mbwembwe zote ni kwenye automatic cars mpe manual utamuonea huruma masikini
 
Namba 3 imenigusa sana hasa kwa barabara ya Kongowe hadi Kigamboni. Kuna jamaa ana altezza jirekebishe kama humu wapita. Jifunze kuachia wenzio wapita iwapo huna haraka badala ya kung'ang'ania mbele, ukiovertake anaanza ligi hataki upite. Basi shiida tu. Angalia gari nyingine sio size yako utaja pasua block engine
 
Nimeamini siku hizi barabarani wenye magari ni wengi kuliko madereva....Hizi tabia zina kera sana barabarani..kama na wewe huwa unafanya haya barabarani basi jua unakera wenzako:

1. Unakuta barabara ya njia(lanes) mbili halafu mtu anaendesha gari katikati ya hizo lane mbili afu unaenda taratibu..hueleweki upo kushoto au kulia...kagari kenyewe kadogo sasa si ukae lane moja uwapishe wengine...?

2. upo njia kuu unakuja yeye anataka kuingia na anakuona kabisa lakini na yeye anaingia tu afu anaanza kutembea taratibu wakati mtu unaharaka zako...sasa si ungenisubiri nipite..si ndo sheria..kama uliona utawahi basi tembea mwendo wa kueleweka au mpishe mwenzako aendelee za safari zake na wewe uendelee na mwendo wako mdogo..au unaona raha kufuatwafatwa matakoni...??

3.haya nimeamua kuvumilia mwendo wako mdogoo wee nimepata nafasi nataka niku overtake..naanza kukupita na wewe unaongeza mwendo...iiish!! unaakili wewe..??nikipunguza nikuache utangulie unaenda kidogo unarudia mwendo wako ule ule..kwani nashindana na wewe jamaa..

4. saa kumi na mbili jioni hata giza halijaingia vizuri tena unapita katikati ya mji mtu ameshawasha taa FULL LIGHTs??? hivi unajua maana ya hizo taa? unawamulika wenzako..wanakuonyeshea na ishara kwamba unawamulika wewe walaaa..kwani unapita porini?? kuwa mstaarabu..au ndo hata hizo taa hujui kwanini zinawaka tofauti tofauti unavyowasha??

5. barabara nyembamba..mbele yako kuna msukuma mkokoteni tena anajitahidi kweli kusukuma kwa nguvu ili asiweke foleni ila wewe bado tu na mahoni yako..piii piii piii..sasa we unataka apae?? ustaarbu kitu cha bure..au unaona kuna foleni labda mbele kabisa kuna lori linakwenda taratibu na kwa kulipita hamna wewe unakuja tu huko unaanza kupiga mihoni yako..sasa unataka kitokee nini...

6.kisa wewe una gari basi waendesha pikipiki,(kumbuka si kila mwendesha pikipiki ni bodaboda), baiskeli na wapita kwa miguu kwako hawana haki ..kila sehemu wewe ndo unajifanya una haki..unakuta round about kuna mtu wa pikipiki au baiskeli anakatisha na wewe unaingia tu ...kisa wewe una gari..?? au wewe ndo unaingia njia kuu na kuna baiskeli inakuja au pikipiki na umeiona kabisa ila wewe unaingia tu... sheria huijui..hata ustaarabu pia??

7. barabara inapita katikati ya mtaa..kuna watoto kibao wanakatiza na kibao cha spidi kipo ila mtu unakimbia spidi 100...??bure kabisa...


8. ongezea na wakwako wanaokukera...
Hiyo ya 6 mkuu ndo penyewe kabisa(ewe dereva usidhani kila pikipiki ni bodaboda) dereva usidhani wote wanaoendesha pikipiki hawana magari,wengine magari wanayo ila ni vile foleni tu za mjini zinafanya gari kuwa mzigo!
 
Uko mbele kwenye gari..... kuna mwendesha mkokoteni au tukio lolote hivyo inakulazimu kwenda mwendo mdogo..... sasa dereva gari la nyuma bila kujua mbele kuna nini na haraka zaje za kidwanzi mihoni kibaaaaaooooo...mwache...siku nyingine utapewa ishara upite ukavagae lori
 
Hiyo ya 6 mkuu ndo penyewe kabisa(ewe dereva usidhani kila pikipiki ni bodaboda) dereva usidhani wote wanaoendesha pikipiki hawana magari,wengine magari wanayo ila ni vile foleni tu za mjini zinafanya gari kuwa mzigo!
Unakuta mtu anakuja na gari mbio huko mbele kuna pikipiki na mbele ya pikipiki kuna gari lingine ile yeye anakuja tu na kumbana mwenye pikipiki mtaroni.. Shida nini??
 
Unakuta mwingine amepaki gari usiku labda mjini ila bado kawasha mitaa full.. Sasa wewe umesimama na umepaki gari pembeni basi zima taa washa za parking au hata flashers tu walau lakini wewe unawasha full lights kweli.. Afu bora hata ingekuwa mtu unasimama labda sec10 au dk moja hivi.. Nusu sasa nzima?
 
matumizi sahihi ya hizi lane mbili watu wengi bado ni shida inakera sana inatakiwa kama uko taratibu kaa kushoto waendaonkasi wapite kulia lakini unakuta jamaa kakazana kuendesha upande wa kulia ilhali mwendo wake mdogo sana na ukimpa ishara akupishe haelewi. nadhani kwenye hili tanroads watuwekee mabango yaseme
KAA KUSHOTO / KEEP LEFT
PITA KULIA / PASS RIGHT
 
matumizi sahihi ya hizi lane mbili watu wengi bado ni shida inakera sana inatakiwa kama uko taratibu kaa kushoto waendaonkasi wapite kulia lakini unakuta jamaa kakazana kuendesha upande wa kulia ilhali mwendo wake mdogo sana na ukimpa ishara akupishe haelewi. nadhani kwenye hili tanroads watuwekee mabango yaseme
KAA KUSHOTO / KEEP LEFT
PITA KULIA / PASS RIGHT
Uko sahihi kabisa.. Matumiz ya lane wengi wanabahatisha tu.. Unakuta mtu yupo lane ya kushoto anataka kukata kulia badala ya kuingia kwanza/mapema lane ya kulia then ndo akatishe yeye anataka atoke kushoto moja kwa moja na kuvuka lane inayofata na kukata kona hapo hapo.. Na anaona kabisa nyuma yake kuna magari matokeo yake anaweka foleni zisizo nalazima
 
Unakuta mwingine kupiga u turn tu barabarani utadhani anaendesha roli kumbe gari ndogo tu tena auto.. Yaani mtu anaenda mbele anarudi nyuma mara tano?! U turn tu...tena barabara pana ya kutosha.. Watu wanasubiri mpaka wanachoka... Duh..
 
Mkuu pole sana hiyo inatukera wengi ila binadamu tunatofautiana, nadhani wenye tabia hiyo watajirekebisha baada ya kusoma Uzi huu.
 
Kukereka na gari ya mwenzio hujui alipolipata hilo ni jipu
soma mada uelewe kabla ya ku comment, mleta mada anakereka na madereva kutofuata sheria za barabarani na kutokuwa na ustaarabu, jaribu kuwa serious sometimes sio kutwa kutema Pumba tu humu kama Bata.
 
me kuna mmoja leo asubuh maeneo yq kwa nyerere kanichomekea alaf atembei ukitaka kumpita anaongezq mwendo na nilikua naalaka kwell bas tukaendq ad mataa ya moroco nikampita kumbe alikua na dem alaf dem kaladha kiti kajiladha chali jamaa linashika mapaja
 
Back
Top Bottom