mitindo huru
JF-Expert Member
- Apr 26, 2016
- 1,607
- 1,596
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na dada Esther ambaye anasimama kama facilitator wa kiwanda cha Dangote kabla hata akijaanza na Mr Gabriel ambaye ni transporter mkuu wa makaa ya mawe wakihojiwa na Masoud Kipanya katika kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na Redio Clouds Fm siku ya leo walisema.
Wahujumu wakubwa wa kiwanda cha Dangote ni
1.Management ya kiwanda chenyewe kwa kuwa wanatoa taarifa zinazokinzana na makubaliano ya serikali hasa kwenye bei ya mauziano ya gasi pili bei inayokinzana kuhusu hali halisi ya soko hulia kwamba haiwezekani mwekezaji mmoja akauziwa gesi bei tofauti na wawekezaji wengine. Na ifahamike kwamba management ya kiwanda imejumuisha watu wengi wenye asili ya india na wachache kutoka nigeria.
2. Wahujumu wa pili ni wamiliki wa mgodi wa makaa ya mawe kule songea, kwa mujibu wa Mr Gabriel ambaye ni tramsporter anasema zoezi la kutoa makaa ya mawe kutoka mgodini hadi kupakia kwa gari moja inachukua siku nne hivyo ikapelekea tatizo la upatikanaji wa makaa ya mawe kwa kuwa uhitaji ya makaa ya mawe ni mkubwa kwa kiwanda cha Dangote ukilinganisha na upatikanaji nchini Tanzania. Na ijulikane wamiliki wakubwa wa mgodi wa makaa ya mawe kule songea ni watu toka india
3. Wahujumu wengine ni viwanda vya ndani na nje ya nchi vinavyozalisha Cement, hivyo wamekuwa wanatoa shinikizo kwa watu wengine wanaohusika na uzalishaji wa kiwanda cha Dangote kwa namna mbalimbali ili kuhujumu utendaji wa kiwanda mfano ni uharibifu wa mitambo, uwizi wa vitu mbalimbali kama mafuta, mashine mbalimbali n.k na management ya kiwanda cha Dangote wanajua hili tatizo.
Baada ya hayo maelezo machache yafuatayo yanaweza kufanyika ili kutatua hili tatizo
1. Dada Esther kwa maelezo yake amesema anawafahamu kwa majina watu wote wanaoshirikiana na watu mbalimbali ili kuhujumu kiwanda ila anaogopa kwa usalama wake, hivyo tunaomba Rais JPM ampe ulinzi dada Esther ili ataje hao watu kwa manufaa ya taifa.
2. Tunaomba mkataba uliosainiwa mara ya kwanza awamu ya Rais JK uwekwe wazi baina ya Dangote na Serikali ili ijulikane tatizo liko wapi kwa kuwa mara ya kwanza tatizo lilionekana ni makaa ya mawe lakini siku zinavyokwenda inaonekana kuna matatizo mengine kati ya serikali na kiwanda cha Dangote.
Nimeelezea kwa ufupi ila kadiri mjadala utakavyokuwa tutaendelea kuuchambua ukweli uliojificha.
NB: watanzania kama tunahitaji maendeleo inatakiwa tuvae uzalendo wa nchi. Tukitegemea mataifa mengine hasa hawa wahindi wawe wasemaji na waamuzi wa mambo yanayohusu maendeleo ya Tanzania hatutaweza kufika popote..
Hii ishu inatishia uchumi wa nchi na uwekezaji mana kama Dangote mwenyewe amefikia kuiongelea kwenye majarida na vyombo vya habari vya kimataifa kama Forbes na BBC.
Na kama kiwanda kimoja kikubwa kama cha Dangote kinatusumbua, je vikija viwanda 10 kama hivi itakuwaje kama serikali haina sera zinazoeleweka kwenye uwekezaji
Wahujumu wakubwa wa kiwanda cha Dangote ni
1.Management ya kiwanda chenyewe kwa kuwa wanatoa taarifa zinazokinzana na makubaliano ya serikali hasa kwenye bei ya mauziano ya gasi pili bei inayokinzana kuhusu hali halisi ya soko hulia kwamba haiwezekani mwekezaji mmoja akauziwa gesi bei tofauti na wawekezaji wengine. Na ifahamike kwamba management ya kiwanda imejumuisha watu wengi wenye asili ya india na wachache kutoka nigeria.
2. Wahujumu wa pili ni wamiliki wa mgodi wa makaa ya mawe kule songea, kwa mujibu wa Mr Gabriel ambaye ni tramsporter anasema zoezi la kutoa makaa ya mawe kutoka mgodini hadi kupakia kwa gari moja inachukua siku nne hivyo ikapelekea tatizo la upatikanaji wa makaa ya mawe kwa kuwa uhitaji ya makaa ya mawe ni mkubwa kwa kiwanda cha Dangote ukilinganisha na upatikanaji nchini Tanzania. Na ijulikane wamiliki wakubwa wa mgodi wa makaa ya mawe kule songea ni watu toka india
3. Wahujumu wengine ni viwanda vya ndani na nje ya nchi vinavyozalisha Cement, hivyo wamekuwa wanatoa shinikizo kwa watu wengine wanaohusika na uzalishaji wa kiwanda cha Dangote kwa namna mbalimbali ili kuhujumu utendaji wa kiwanda mfano ni uharibifu wa mitambo, uwizi wa vitu mbalimbali kama mafuta, mashine mbalimbali n.k na management ya kiwanda cha Dangote wanajua hili tatizo.
Baada ya hayo maelezo machache yafuatayo yanaweza kufanyika ili kutatua hili tatizo
1. Dada Esther kwa maelezo yake amesema anawafahamu kwa majina watu wote wanaoshirikiana na watu mbalimbali ili kuhujumu kiwanda ila anaogopa kwa usalama wake, hivyo tunaomba Rais JPM ampe ulinzi dada Esther ili ataje hao watu kwa manufaa ya taifa.
2. Tunaomba mkataba uliosainiwa mara ya kwanza awamu ya Rais JK uwekwe wazi baina ya Dangote na Serikali ili ijulikane tatizo liko wapi kwa kuwa mara ya kwanza tatizo lilionekana ni makaa ya mawe lakini siku zinavyokwenda inaonekana kuna matatizo mengine kati ya serikali na kiwanda cha Dangote.
Nimeelezea kwa ufupi ila kadiri mjadala utakavyokuwa tutaendelea kuuchambua ukweli uliojificha.
NB: watanzania kama tunahitaji maendeleo inatakiwa tuvae uzalendo wa nchi. Tukitegemea mataifa mengine hasa hawa wahindi wawe wasemaji na waamuzi wa mambo yanayohusu maendeleo ya Tanzania hatutaweza kufika popote..
Hii ishu inatishia uchumi wa nchi na uwekezaji mana kama Dangote mwenyewe amefikia kuiongelea kwenye majarida na vyombo vya habari vya kimataifa kama Forbes na BBC.
Na kama kiwanda kimoja kikubwa kama cha Dangote kinatusumbua, je vikija viwanda 10 kama hivi itakuwaje kama serikali haina sera zinazoeleweka kwenye uwekezaji