Hawa ndio wa watanzania

Hawa ndio wa watanzania

Danpol

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2013
Posts
5,747
Reaction score
9,012
Ukiwa Kijana

1. Ukiwa single watakuuliza, kwanini huna Girlfriend au Boyfriend?

2. Ukiwa na mchumba, watahoji mmekaa sana mtaoana lin?

3. Ukioa utasikia, mbona hamzai nyie?cc twataka wajomba,shangaz na wajukuu

4. Mkizaa watakuja na hii, mtoto kakua mtafutieni dada au kaka yake!

5. Ukimtafuta, utasikia mbona mnazaa haraka haraka hamuogopi maisha?maisha magumu cku izi Ukiwa na Hela

1. Ukinenepa, we unanenepa tu hivi huogopi magonjwa (presha na kisukari)

2. Ukikonda, acha ubahili, pesa zote hizo unakuwa mbahili? wengine watasema mara alitembeaga na dada/ kaka fulani mwenye ngoma ndio imekolea sasa. Hamalizi mwaka huyu, lazima tumzike tu.

3. Ukinunua gari, unanunuaje gari wakati hujajenga? huna kiwanja? Vijana wa siku hizi bure kabisa.

4. Ukijenga huna gari, yaani na usumbufu wote huu wa madaladala huna gari? tunakushangaa sana. Nunua ata Toyo!! Ukifanya mazoezi

1. Kama ni mwembamba, wee kimbau mbau unapunguza nini kwenye ako kamwili ako, (wanajua mazoezi ni kupunguza mwili tu!)

2. Ukiwa Mnene, yaani Mungu hakupi vyote. Ona sasa amekula mikuku yake sasa ndio anateseka nayo kupungua.

3. Ukiwa na mwili wa wastani, huyu ni bishoo tu, hana lolote yeye ni kupita na vikaptula tu mitaani! Jamani! sasa lipi jema kwenu??
 
ubinanamu kaaazi ingawa hatulipwi mshahara
 
Back
Top Bottom