Hawa nao ni watanzania?

Lukansola

JF-Expert Member
Sep 5, 2010
5,435
1,597
Ilikuwa majira ya saa saba mchana pale maeneo ya PPF Towers jijini Dar es Salaam leo tarehe 2 march 2011, nikiwa katika harakati za kusababisha mikono yangu na ya wale wanaonitegemea iende kinywani, ghafla nikawaona hawa, nikashawishika kuwapiga picha ili ku-share na wanajamii wenzangu The Great Thinkers.

Wanasema uchungu wa mwana aujuae ni mzazi, mimi ninao watoto, ninaujua uchungu wa mwana, nina amini hata watoto hao wana wazazi wao pia, najaribu ku imagine uchungu walio nao wazazi wa watoto hao, endapo wapo hai au wanawajua watoto wao hao. Maana kuna uwezekano hata baba zao hawajui kama watoto hao ni wao (si nasikia kuna watoto wengine huzaliwa bila mama zao kuwa na uhakika baba zao ni kina nani au kutowajua kabisa) anyway mwisho wa siku ni watoto wa Watanzania ni watoto wetu wote, ndio tunaowategemea waijenge Tanzania ya kesho.

CCM imeahidi maisha bora kwa kila mtanzania, ndio kauli mbiu ya chama hicho, na juzi katika hotuba ya rais wetu moja kati ya zile za kila mwezi alisema mafanikio mengi yamepatikana katika utawala wa CCM na yanaonekana ingawa mimi binafsi sijayaona kihivyo, najiuliza hivi itachukua muda gani kabla hatujaacha kukutana na taswira kama hizi katika Tanzania yetu.

Na hawa ni baadhi tu ya watoto wanao ishi kwenye mazingira kama haya kote Tanzania, achilia mbali wale wanaosafisha vioo vya magari pale kwenye mataa ya moroko na kwingineko huku wakitarajia ujira mdogo kutoka kwa wenye magari hayo.

Wapo wale wanaofanya biashara ya ngono wakiwa na umri mdogo, kwa ajili ya kuepuka kifo cha njaa, hakika siwezi kuwakilisha matatizo yote ya kijamii hapa.

Hebu na sisi tuchangie mawazo yetu hapa hivi kuna kitu tunaweza kufanya kuepusha aibu hii kwa taifa letu, nina amini hata wageni wanaona kama tunavyoona sisi, si wanapita humuhumu tunamopita sisi? unless mnaniambia hali hii hata kwenye nchi zilizoendelea ipo, mnaoishi majuu tuambieni.
 

Attachments

  • taswira ya nchi.jpg
    taswira ya nchi.jpg
    57.7 KB · Views: 105
Kweli inatia huruma sana, hawana uhakika na chochote waTZ hawa....
 
Inasikitisha sana, natamani kama ningalikuwa na uwezo angalau wa kuhoji wahusika wa wizara ya wanawake na watoto, bila shaka na wao ni binadamu na wazazi kama mtoa mada....
 
Kwa kuwa ni saa saba mchana wamelala hivyo means hawapata chakula wala hawana matumaini yoyote ya maisha hii ni mbaya sana kama serikali ilipaswa kuwa na cha kufanya kuhusu hili.

Tuna wizara kibao na taasisi nyingi tu zisizo za kiserikali zinazojishughulisha na watoto, je hawayaoni haya? Usanii mtupu.

Pengine kwa tafsiri ya watawala wetu haya ndio maisha bora kwa kila mtanzania, ki kweli inasikitisha sana. Mali za kumfanya kila mtanzania aishi salama zipo, tatizo ni kukosa vipa umbele kama taifa.

Inahuzunisha sana. Hili ndio lili linaloitwa taifa la kesho, sipati picha!!
 
Inasikitisha sana, natamani kama ningalikuwa na uwezo angalau wa kuhoji wahusika wa wizara ya wanawake na watoto, bila shaka na wao ni binadamu na wazazi kama mtoa mada....

Waziri wao yuko bize na mambo mengine MAMBO YA SI HASA
 
Kwa kuwa ni saa saba mchana wamelala hivyo means hawapata chakula wala hawana matumaini yoyote ya maisha hii ni mbaya sana kama serikali ilipaswa kuwa na cha kufanya kuhusu hili.

Tuna wizara kibao na taasisi nyingi tu zisizo za kiserikali zinazojishughulisha na watoto, je hawayaoni haya? Usanii mtupu.

Pengine kwa tafsiri ya watawala wetu haya ndio maisha bora kwa kila mtanzania, ki kweli inasikitisha sana. Mali za kumfanya kila mtanzania aishi salama zipo, tatizo ni kukosa vipa umbele kama taifa.

Inahuzunisha sana. Hili ndio lili linaloitwa taifa la kesho, sipati picha!!

Jayfour_King,
Uko sawa, hawawezi wakawa wamelala baada ya chakula cha mchana, kwamba wanajimpumzisha kidogo chakula kiyeyuke tumboni, la hasha halafu fikiria picha unayoiona ni ya siku moja tu! lakini kwao ni maisha ya kila siku tena bila matumaini ya kujikwamua.

nadhani da sofia angeachana na malumbano akafanya kazi na sisi tumkubali walau kidogo sasa yeye kila siku kutupiana madongo tu duuuuh!
 
Ukweli ni kwamba No 1 cares, wachache wanaojali mchango wao huishia kwenye maneno na maandishi kama haya.
Wengine ambapo ndio wengi wanaona fulsa za kiuchumi kwenye matatizo ya hawa watoto.
Mbaya ni kwamba hawa watoto kwa maisha magumu wanayo pitia ni bomu kali zaidi ya Nyuklia bomu. Hawa watoto nivigumu kuwa na purpose in life, hivyo ni rahisi kutumiwa kwa namna yoyote.
In another perspective nani anatakwimu za hawa watoto!? Tumesikia huko india na Rusia kumeanzishwa maduka ya viungo vya binadamu, nani anahakikisha usalama wa hawa watoto?

My take, badala ya kupiga blaablaa nyingi kila mmoja achukue atua. Charity bigins at home.
1. Anza kwa kuhakikisha kila mtoto katika familia, ukooo na kuendelea anapata elimu sahihi.
2. Saidia kila inapohitajika, tuwaonapo mtaani tuone ni watoto wetu, wadogozetu, wajombazetu. Kalibia kila kona ya mji kuna vituo vya watoto yatima, hata mala moja kwa mwaka ama miezi 6 watembelee na kuwasaidia kwa lolote. Hata kwa nguo ilizojaza ndani kwako na huzitumii wewe wala watoto wako hawatumiii. nenda na familia yako yote ikajifunze kitu.

3. Kwa NGO'S nawaomba muache kutake advantage ya matatizo ya wengine, fanyeni hiyo kazi kwa moyo na mtapata tuzo ilyo bora kutokana na kazi hiyo.

4. Serikali kwa ujumla inatakiwa kutambua kila sekta inaumuhimu sawa na bila kulitambua hili hatuwezi endelea. Serikali naweza ifananisha na mfumo wa gari, ambapo kila sub system inaumuhimu mkubwa na inahitaji uzito wake wa uangalizi ili gari liende salama.
 
hao ni watanzania tena halisi ila wametengwa na serikali yao na wapo zaidi kuisuta kauli mbiu zao za maisha bora
 
Back
Top Bottom