Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
RAIS Jakaya Kikwete amesema baada ya maridhiano kati ya Chama cha Wananchi (CUF) na Serikali ya Mapinduzı ya Zanzibar, hali ya kisiasa, itazidi kuwa nzuri visiwani humo.
Mbali na hilo, amesema watu wasitarajie sasa kusikia amri za wanasiasa za kuchochea vurugu visiwani humo.
Akizungumza na wanafunzi wanaosoma nchini Uturuki juzi, Rais Kikwete alisema ''baada ya mazungumzo hali ya Zanzibar itazidi kuwa nzuri zaidi. Matumaini yetu amri za wanasiasa kupiga mawe hazitakuwapo tena.
Kawaida wanasiasa ndiyo wanaogombana na si wananchi, aliongeza Rais Kikwete. Rais Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad walikutana Ikulu Zanzibar, Novemba 5, mwaka jana na kuzaa maridhiano ya kisiasa visiwani humo na sasa kunaandaliwa kura ya maoni kwa ajili ya kuundwa kwa mfumo wa Serikali ya Mseto.(Habari Leo)
My take
Kumbe alikuwa anajua wanaoanzisha vurugu ni viongozi alikuwa wapi sasa kukemea hizo amri hadi baadhi ya wananchi wasio na hatia kupoteza maisha yao au alikuwa hawajui kwa majina si viongozi tu bali hata ukimya wake pia ulisababisha kuchochea vurugu
Mbali na hilo, amesema watu wasitarajie sasa kusikia amri za wanasiasa za kuchochea vurugu visiwani humo.
Akizungumza na wanafunzi wanaosoma nchini Uturuki juzi, Rais Kikwete alisema ''baada ya mazungumzo hali ya Zanzibar itazidi kuwa nzuri zaidi. Matumaini yetu amri za wanasiasa kupiga mawe hazitakuwapo tena.
Kawaida wanasiasa ndiyo wanaogombana na si wananchi, aliongeza Rais Kikwete. Rais Amani Abeid Karume na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad walikutana Ikulu Zanzibar, Novemba 5, mwaka jana na kuzaa maridhiano ya kisiasa visiwani humo na sasa kunaandaliwa kura ya maoni kwa ajili ya kuundwa kwa mfumo wa Serikali ya Mseto.(Habari Leo)
My take
Kumbe alikuwa anajua wanaoanzisha vurugu ni viongozi alikuwa wapi sasa kukemea hizo amri hadi baadhi ya wananchi wasio na hatia kupoteza maisha yao au alikuwa hawajui kwa majina si viongozi tu bali hata ukimya wake pia ulisababisha kuchochea vurugu