Watumishi wengi wa (hw) hatujalipwa mishahara yetu hadi leo. Na inasemekana hela zetu zimetafunwa pale hal'shauri. Ukiuliza hawatoi majibu ya kueleweka. Inasikitisha sana mtu umefanya kazi ila kupewa chako inakuwa tatizo. Na hii wilaya inaongoza kwa kunyanyasa watumishi hasa kwenye malipo (malimbikizo). Wanasingizia mtandao ndio uliondoa majina kwenye payrol, je, wenzetu huko vp mmepata tatizo km hilo kwa baadhi ya watumishi?