KERO Mpimbwe: Watumishi tulioajiriwa JUNI 2022 hatujapandishwa madaraja wala kulipwa Malimbikizo ya Mishahara

KERO Mpimbwe: Watumishi tulioajiriwa JUNI 2022 hatujapandishwa madaraja wala kulipwa Malimbikizo ya Mishahara

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Watumishi walioajiriwa mwezi Juni 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe tunaomba haki yetu ya msingi itendeke. Pamoja na kutimiza wajibu wetu wa kazi kwa uaminifu, hadi sasa wengi wetu hatujafanyiwa utaratibu wa kupandishwa madaraja kama sheria na taratibu za utumishi wa umma zinavyoelekeza.

Aidha, watumishi wengi bado hawajalipwa malimbikizo ya mishahara ya kipindi cha mwanzo wa ajira zetu. Madai yaliwasilishwa tangu mwezi Disemba mwaka 2022 lakini mpaka leo hayajaingizwa kwenye mifumo husika ili yapitiwe na kufanyiwa malipo.

Hali hii imesababisha usumbufu mkubwa kwa watumishi, huku tukikosa majibu ya kueleweka licha ya kufuatilia kwa muda mrefu.

Tunaiomba serikali, viongozi wa utumishi na mamlaka husika kuingilia kati suala hili ili watumishi wote walioathirika wapatiwe haki zao kwa wakati. Tunahitaji haki, usawa na uthamini wa kazi tunayoifanya kwa wananchi.
 
Mkuu unaweza nikosoa umeajiriwa 2022 leo 2026 unataka upande Daraja!? Au unataka ufanyiwe utaratibu wa kupanda Daraja sahv!??
 
Watumishi walioajiriwa mwezi Juni 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe tunaomba haki yetu ya msingi itendeke. Pamoja na kutimiza wajibu wetu wa kazi kwa uaminifu, hadi sasa wengi wetu hatujafanyiwa utaratibu wa kupandishwa madaraja kama sheria na taratibu za utumishi wa umma zinavyoelekeza.

Aidha, watumishi wengi bado hawajalipwa malimbikizo ya mishahara ya kipindi cha mwanzo wa ajira zetu. Madai yaliwasilishwa tangu mwezi Disemba mwaka 2022 lakini mpaka leo hayajaingizwa kwenye mifumo husika ili yapitiwe na kufanyiwa malipo.

Hali hii imesababisha usumbufu mkubwa kwa watumishi, huku tukikosa majibu ya kueleweka licha ya kufuatilia kwa muda mrefu.

Tunaiomba serikali, viongozi wa utumishi na mamlaka husika kuingilia kati suala hili ili watumishi wote walioathirika wapatiwe haki zao kwa wakati. Tunahitaji haki, usawa na uthamini wa kazi tunayoifanya kwa wananchi.
Kiongozi unazifahamu taratibu au unajiandikia tu. Juni 2022 unataka upande daraja leo? Upo serious??? June 2022 - May 2023 Probation, June 23 - May 24 Year 1, June 24 - May 25 Year 2, June 25 - June 26 Year 3. Unapandaje sasa wakati mwaka wa 3 ndo kwanza umeingia??
 
Tunahitaji haki, usawa na uthamini wa kazi tunayoifanya kwa wananchi.
Kabla ya kutuandikia hapa sisi km wakuu wa panel ya JF mlichukua hatua gani yaani hili lalamiko lenu la tangu 2022 mpaka leo hii June 2026 lilifika wapi na wapi mpaka sasa limefikia wapi?
 
Kiongozi unazifahamu taratibu au unajiandikia tu. Juni 2022 unataka upande daraja leo? Upo serious??? June 2022 - May 2023 Probation, June 23 - May 24 Year 1, June 24 - May 25 Year 2, June 25 - June 26 Year 3. Unapandaje sasa wakati mwaka wa 3 ndo kwanza umeingia??
Binafsi nimeshangaa kidogo anacho Lalamika taratibu za kiutumishi kwa Ajira mpya Pengine hazijui
 
Kiongozi unazifahamu taratibu au unajiandikia tu. Juni 2022 unataka upande daraja leo? Upo serious??? June 2022 - May 2023 Probation, June 23 - May 24 Year 1, June 24 - May 25 Year 2, June 25 - June 26 Year 3. Unapandaje sasa wakati mwaka wa 3 ndo kwanza umeingia??
Vizuri umemfafanulia mkuu sasa atakua ameelewa naona hio probation period hakuifanyia mahesabu na hapo bado mpaka aidhinishwe kazini unaweza kuta aliidhinishwa 2024 kwa hio kupandishwa itakua bado mpaka asubirie 3 years km sijakosea
 
Kiongozi unazifahamu taratibu au unajiandikia tu. Juni 2022 unataka upande daraja leo? Upo serious??? June 2022 - May 2023 Probation, June 23 - May 24 Year 1, June 24 - May 25 Year 2, June 25 - June 26 Year 3. Unapandaje sasa wakati mwaka wa 3 ndo kwanza umeingia??
Kwa hio aliyeajiriwa let's say Feb,2023 anapanda daraja lini?
 
Nnachojua Ajira ya 2021 ndio wengi hawajapanda, baadhi ya mikoa wameanza kupanda mwaka huu.
 
Watumishi walioajiriwa mwezi Juni 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe tunaomba haki yetu ya msingi itendeke. Pamoja na kutimiza wajibu wetu wa kazi kwa uaminifu, hadi sasa wengi wetu hatujafanyiwa utaratibu wa kupandishwa madaraja kama sheria na taratibu za utumishi wa umma zinavyoelekeza.

Aidha, watumishi wengi bado hawajalipwa malimbikizo ya mishahara ya kipindi cha mwanzo wa ajira zetu. Madai yaliwasilishwa tangu mwezi Disemba mwaka 2022 lakini mpaka leo hayajaingizwa kwenye mifumo husika ili yapitiwe na kufanyiwa malipo.

Hali hii imesababisha usumbufu mkubwa kwa watumishi, huku tukikosa majibu ya kueleweka licha ya kufuatilia kwa muda mrefu.

Tunaiomba serikali, viongozi wa utumishi na mamlaka husika kuingilia kati suala hili ili watumishi wote walioathirika wapatiwe haki zao kwa wakati. Tunahitaji haki, usawa na uthamini wa kazi tunayoifanya kwa wananchi.
Nyie wa ajira mpya ya mwaka huo bado hamjafiikia umri wa kupandishwa madaraja. Na hakuna malimbikizo ya mshahara hapa. Labda kama hukupata mishahara ya mwanzo wakati umepata ajira. Kupandishwa kwenu ni kuanzia mwaka ujao yaani Julai hii au kikao cha Safari hii. Acheni kulalamika fanyeni kazi
 
Kiongozi unazifahamu taratibu au unajiandikia tu. Juni 2022 unataka upande daraja leo? Upo serious??? June 2022 - May 2023 Probation, June 23 - May 24 Year 1, June 24 - May 25 Year 2, June 25 - June 26 Year 3. Unapandaje sasa wakati mwaka wa 3 ndo kwanza umeingia??
Pamoja na hizi hesabu huyu mtu July inabidi aanze huku kapanda. Aliandika mapema lakini ni sahihi kabisa kwamba anatakiwa kupanda, sehemu zingine wameshapanda.
 
Watumishi walioajiriwa mwezi Juni 2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe tunaomba haki yetu ya msingi itendeke. Pamoja na kutimiza wajibu wetu wa kazi kwa uaminifu, hadi sasa wengi wetu hatujafanyiwa utaratibu wa kupandishwa madaraja kama sheria na taratibu za utumishi wa umma zinavyoelekeza.

Aidha, watumishi wengi bado hawajalipwa malimbikizo ya mishahara ya kipindi cha mwanzo wa ajira zetu. Madai yaliwasilishwa tangu mwezi Disemba mwaka 2022 lakini mpaka leo hayajaingizwa kwenye mifumo husika ili yapitiwe na kufanyiwa malipo.

Hali hii imesababisha usumbufu mkubwa kwa watumishi, huku tukikosa majibu ya kueleweka licha ya kufuatilia kwa muda mrefu.

Tunaiomba serikali, viongozi wa utumishi na mamlaka husika kuingilia kati suala hili ili watumishi wote walioathirika wapatiwe haki zao kwa wakati. Tunahitaji haki, usawa na uthamini wa kazi tunayoifanya kwa wananchi.
Hivi hii Wilaya yenu ya Mpimbwe iko Mkoa gani! Mpimbwe!!!
 
Back
Top Bottom