Hatma ya wasomi wetu Tanzania

Clark boots

JF-Expert Member
Jun 5, 2017
6,401
5,525
Habari za pilikapilika za kutwa nzima wanaJF!

Ni wakati/muda tu umenilazima kuyaandika haya kuhusiana na hatma ya wasomi wetu nchini hasa kwenye suala la ukosefu wa ajira ndani ya miaka hii minne toka serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani na miaka ijayo mbeleni.

Ni ukweli usiopingika kuwa sasa ajira zimekuwa adimu Serikalini hata mashirika/taasisi binafsi, licha ya wafanyakazi hewa wote wale waliondolewa, ufisadi au utakatishaji fedha za umma uliokomaa na pesa zetu nyingi zinazorudishwa serikalini kutoka kwa mafisadi Ila bado suala la ajira ni kizungumkuti.

Ni dhahiri kabisa kuwa suala/sekta ya ajira ni sekta nyeti kwa kila taifa, nadhani serikali yenyewe inahimiza watu kuhusu elimu ili ije kuwakomboa watu katika maisha yao na tegemeo kuu ni ajira.

Vijana mamia kwa mamia wanahitimu elimu za juu kila mwaka na wanajazana mitaani tu, Ajira Hamna. Ni muda sasa serikali ikaliona hili japo si wote na tunaamini hakuna serikali yoyote inayoweza kuajiri wasomi wote katika taifa husika basi hata kwa kiwango fulani/nusu yao si haba.

Inasikitisha sana nyakati hizi kuona msomi wa shahada anamaanika, elimu imekuwa haina thamani tena na watu kujenga dhana kuwa elimu ni upotevu wa muda/wakati.

Leo nilikuwa nafuatilia hizi ajira kada ya kilimo kutoka sekretariet ya ajira. Vijana wengi wameitwa kwenye usaili halafu nafasi ni 10 tu. Kiukweli haiingii akilini unahitaji watumishi 10 halafu unaita interview watu 1300 sawa na 0.7% ya watu wote. Inasikitisha sana.

Ni muda muafaka sasa wa Serikali kuliona hili kwani hali ni tete na elimu yetu bado sana wala haiwezi kumjenga kijana kuweza kujiajiri mwenyewe baada ya kuhitimu masomo yake. Ni muda mrefu sana Graduates wanaozeana huku mitaani.
Sasa umekuwa ni muda wa kutengeneza, vibaka, majambazi, machangudoa, wezi, matapeli.

Naomba serikali iliangalie hili kwa jicho la tatu.

Nawasilisha.
 
Cha kushangaza ni kwamba kunahitajika watumishi wengi wakazibe magap yaliyopo ila ajira hazitolewi.

.....Hii ndio maana halisi ya kusomeshwa namba.....!!
 
Cha kushangaza ni kwamba kunahitajika watumishi wengi wakazibe magap yaliyopo ila ajira hazitolewi.

.....Hii ndio maana halisi ya kusomeshwa namba.....!!
Kweli kabisa, hakika "Namba inasomeshwa"
 
Kitu kinacho changia ukosefu wa ajira Ni mifumo yetu ya elimu kuwa mibovu na dhaifu
Yani haimfanyi mwanafunzi kuwa mbunifu wa kitu chake kutokana na fani (profession) yake aliyosomea
Badala yake wanafunzi wanasoma ili tu kufaulu mitihani na hawafundishwi uvumbuzi Yani mwanafunzi abuni kitu chake
 
Kitu kinacho changia ukosefu wa ajira Ni mifumo yetu ya elimu kuwa mibovu na dhaifu
Yani haimfanyi mwanafunzi kuwa mbunifu wa kitu chake kutokana na fani (profession) yake aliyosomea
Badala yake wanafunzi wanasoma ili tu kufaulu mitihani na hawafundishwi uvumbuzi Yani mwanafunzi abuni kitu chake
motivational Speaker huyu
 
Nawakumbusha tu kuwa ile midoli na vikatuni tunavyowanunulia watoto wetu Kariakoo vimetengenezwa na form four leaver wa China huku maprofesa wetu ujuzi wao unaishia kwenye project na ma proposal tu.

Kuna jamaa yangu 2016 nilimwambia kuwa huyu mzee sio akabisha. Leo mwaka 3 tangu apate shahada yake anauza duka la uncle wake tu. Kanyooka.

Mwingine mwaka 2015 nilimwambia huyu mzee sio poa akabisha na kila siku alikuwa akiedit profile picture fb kwa picha ya mzee, sasa mwaka 4 tangu apate shahada hajui ajira, kaenda jkt kamaliza 2 yrs bila ya usaili hata mmoja. Tuliokwenda jkt enzi za Jakaya tunajua, ndani ya miaka 2 unafanya usaili hata mara 4 au zaidi.

Magu kaza zaidi
 
Ule wimbo wa acha waisome namba, unadhani ulikiwa una maanisha nin?


Ukiiona ccm ikimbie kabisa, ni zaidi ya mashetan, wanafanya watu wanaishi kama mashetan kama ilani yao inavosema..
 
Sasa umekuwa ni mda wa kutengeneza, vibaka, majambzi, machangudoa, wezi, matapeli..
Yaani hapa ndipo ulipaharibu kabisa hoja yako nzuri. Hivi ina maana ukikosa ajira serikalini unakuwa kibaka au changudoa? Kwa nini unawafunga fikra wahitimu wetu, Je serikali hata ikitengeneza fursa za ajira nyingi iwezekanavyo, inaweza kuajiri wote katika kada zote? Je wakibaki hata 500 tu nchi nzima, ina maana watakuwa majambazi?
 
Kitu kinacho changia ukosefu wa ajira Ni mifumo yetu ya elimu kuwa mibovu na dhaifu
Yani haimfanyi mwanafunzi kuwa mbunifu wa kitu chake kutokana na fani (profession) yake aliyosomea
Badala yake wanafunzi wanasoma ili tu kufaulu mitihani na hawafundishwi uvumbuzi Yani mwanafunzi abuni kitu chake
Mfumo mbovu wa uchumi ndiyo unaochangia
 
Hakika, mfumo mbovu wa uchumi ndiyo unaochangia ukosefu wa ajira. Hauzalishi ajira nyingi mbona nchi kama Germany inawasomi wengi kuliko Tanzania lakini unemployment rate siyo ya kutisha kama Tz?

Mkwere aliruhusu private sector kukua ndiyo maana ajira zilianza kuongezeka taratibu huyu hata serikali anyoiongoza imefeli kuajiri huku sekta binafsi inajifia taratibu.
 
Bado kuna uhitaji mkubwa wa wataalam serikalini, sio kweli kwamba imefika muda eti wataalam wametosha..

Pamoja na nchi kuwa maskini sera mbovu na kukosa ubunifu kwa serikali ya CCM ndio sababu..

Hakuna aliyepo huko juu anafikiria kuondokana na umaskini katika hii nchi, wamebaki kupiga kelele za watu wajiajiri, kuajiajiri sawa ila mwisho wa siku mteja ni nani? Nani utampa hizo huduma hiari watu wapo katika tope la umaskini?
 
Back
Top Bottom