Hatma ya walimu wa sanaa Tanzania

Hatma ya walimu wa sanaa Tanzania

geraldincredible

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2017
Posts
2,035
Reaction score
7,227
Samahani wakuu,

Naomba kujua hatma ya walimu wa sanaa (ARTS) waliopo vyuoni na wale waliomaliza chuo toka 2015. Naona kama washatupwa, zikiongelewa ajira mpya wanajisifu na zile ajira elfu tatu za sayansi ila kuna lundo la vijana wetu zaidi ya elfu ishirini waliomaliza chuo mwaka juzi hawajui nini mwisho wao.

Najua hapa ni google rapa chochote utakachouliza kitapatikana jawabu lake.

ASANTENI
 
Walimu wa art ndio ishatoka hivo, serikali haina pakuwaweka,

Hivo msiwashauri wajao wasome ualimu wa art , kuna koz nyingi tu ukisoma art utajiajir au kuajiriwa
 
Waende wakalime maana sasa tunajenga uchumi wa viwanda
 
vyama vya wafanyakazi leo ndio ilikuwa siku ya kujua au kutaka maelezo kutoka kwa mkuu hilo suala, ila tatizo nao wanarukaruka tu.
Kwa mifumo hii ambayo haiangalii uhitaji miaka 10/20/50 ijayo sitashangaa siku ikifika hakuna graduate anaehitajika popote pale maana nafasi hazipo...
 
Walimu wa Arts Serikali imeshasema wamezidi maitaji zaid ya 7000 ambao Waziri alisema watawapeleka ktk shule za Msingi kwaiyo Ajira mpya kwa walimu wa Arts Serikalini Hamna Labda sijui baada ya Rais uyu kuondoka Madarakani!!! Poleni Sana
 
daaaah Mimi Nina mdogo wangu kamaliza udom pale nimekaa nae hapa nikaona isiwe kesi nikachukua mkopo nikamnunulia bajaj ajiajiri na leseni akakata....ile bachelor ya history imefanya miez miwili imepata ajali Sasa hivi Niko hapa namuuguza...Nimeona nije hapa kuuliza hatma yao hawa madogo
 
Samahani wakuu Naomba kujua hatma ya walimu wa sanaa (ARTS) waliopo vyuoni na wale waliomaliza chuo toka 2015.Naona kama washatupwa zikiongelewa ajira mpya wanajisifu na zile ajira elfu tatu za sayansi ila kuna lundo la vijana wetu zaidi ya elfu ishirini waliomaliza chuo mwaka juzi hawajui nini mwisho wao...



Najua hapa ni google rapa chochote utakachouliza kitapatikana jawabu lake...ASANTENI
Kwani unamkataba na serikali kwamba ukasome kishaserikali itakuajiri?
 
Walimu wa art ndio ishatoka hivo, serikali haina pakuwaweka,

Hivo msiwashauri wajao wasome ualimu wa art , kuna koz nyingi tu ukisoma art utajiajir au kuajiriwa
Mwalimu wa sayansi anaweza kufundisha art lakini mwalimu wa art hawezi fundisha sayansi haya ndio majibu ya wzi mimi sipendi kufariji mtu
 
Pole mkuu kwa mdogo wako kupata ajari. Nakushauri usikome kumhudumia na kumsaidia msaada wa mawazo na mali
daaaah Mimi Nina mdogo wangu kamaliza udom pale nimekaa nae hapa nikaona isiwe kesi nikachukua mkopo nikamnunulia bajaj ajiajiri na leseni akakata....ile bachelor ya history imefanya miez miwili imepata ajali Sasa hivi Niko hapa namuuguza...Nimeona nije hapa kuuliza hatma yao hawa madogo
 
Mwajiri mkuu ni serikali na miaka ya nyuma ualimu ndio uliongoza kwa ajira hapa tatizo ni kukoma kwa ajira za walimu wa sanaa ghafla. BTW tunasoma kuongeza maalifa na wahitimu wote wa shahada walisoma "DEVELOPMENT STUDY, DS" itawasaidia
Kwani unamkataba na serikali kwamba ukasome kishaserikali itakuajiri?
 
Serikali ya viwanda imesema inataka walimu wa sayansi tu..hawa wa arts sijui hatma yao vipi
 
Nini hatma ya wahitimu nchini (waalimu) na hii Inatoa picha gn kwa vijana wanaotarajia kujiunga na vyuo mbal mbali?

Sent using Jamii Forums mobile app

walimu mbona wamejariwa ( sayansi) ? Labda ungesema hatima ya wahitimu wote wanaosubiri Ajira kama madaktari, mifugo, kilimo n.k ambao hata hawajaguswa
 
Back
Top Bottom