Bujibuji Simba Nyamaume
Platinum Member
- Feb 4, 2009
- 78,157
- 166,102
Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, amekubali kumaliza sakata hilo ambalo liliibuka mwishoni mwa mwaka jana baada ya Tanesco kutaka kupitisha nyaya za umeme juu ya mabango ya kanisa hilo.
Hata hivyo, lengo hilo la Tanesco liligonga mwamba baada ya waumini wa Kanisa hilo kutanda na kuweka ulinzi kwa saa 24 kanisani hapo.
Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam, Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Zakaria Kakobe, alisema mazungumzo ya kutaka kusitisha mpango huo wa Tanesco yanakwenda vizuri na kwamba wiki hii ukweli utajulikana.
Kakobe alisema amefanya mazungumzo na Waziri wa Nishati na Madini ambaye ana dhamana na masuala ya umeme na anaamini kuwa yatazaa matunda.
Mwishoni mwa mwaka jana Tanesco ilitangaza kupitisha nyaya zake juu ya mabango ya Kanisa hilo kitendo ambacho kilipingwa na waumini wake.
Kutokana na kitendo hicho cha Tanesco, waumini wa Kanisa hilo waliamua kujipangia zamu za kulinda Kanisa lao usiku na mchana.
Askofu Kakobe alisema ulinzi unaofanywa na waumini wake ni wa uhakika na kwamba Tanesco hawawezi kupenya.
Walinzi hao wa Kanisa wanafanya kazi hiyo huku wakiwa wamevalia tisheti zilizoandikwa maneno "Tanesco muogopeni Mungu mmeshindwa Richmond mmegeukia Kanisa"
Baadhi ya waumini wa Kanisa hilo waliliambia Nipashe kuwa ulinzi huo unajulikana kama "ulinzi wa kumdhibiti adui."
Ngeleja aliingilia kati sakata hilo baada ya waumini wa Kanisa hilo kujitokeza hadharani na kutangaza vita na Tanesco ambapo waliapa kufa kuliko kuruhusu nyaya zipite juu ya mabango yao.
CHANZO: NIPASHE
Hata hivyo, lengo hilo la Tanesco liligonga mwamba baada ya waumini wa Kanisa hilo kutanda na kuweka ulinzi kwa saa 24 kanisani hapo.
Akizungumza na Nipashe jana jijini Dar es Salaam, Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Zakaria Kakobe, alisema mazungumzo ya kutaka kusitisha mpango huo wa Tanesco yanakwenda vizuri na kwamba wiki hii ukweli utajulikana.
Kakobe alisema amefanya mazungumzo na Waziri wa Nishati na Madini ambaye ana dhamana na masuala ya umeme na anaamini kuwa yatazaa matunda.
Mwishoni mwa mwaka jana Tanesco ilitangaza kupitisha nyaya zake juu ya mabango ya Kanisa hilo kitendo ambacho kilipingwa na waumini wake.
Kutokana na kitendo hicho cha Tanesco, waumini wa Kanisa hilo waliamua kujipangia zamu za kulinda Kanisa lao usiku na mchana.
Askofu Kakobe alisema ulinzi unaofanywa na waumini wake ni wa uhakika na kwamba Tanesco hawawezi kupenya.
Walinzi hao wa Kanisa wanafanya kazi hiyo huku wakiwa wamevalia tisheti zilizoandikwa maneno "Tanesco muogopeni Mungu mmeshindwa Richmond mmegeukia Kanisa"
Baadhi ya waumini wa Kanisa hilo waliliambia Nipashe kuwa ulinzi huo unajulikana kama "ulinzi wa kumdhibiti adui."
Ngeleja aliingilia kati sakata hilo baada ya waumini wa Kanisa hilo kujitokeza hadharani na kutangaza vita na Tanesco ambapo waliapa kufa kuliko kuruhusu nyaya zipite juu ya mabango yao.
CHANZO: NIPASHE