Jing chu
JF-Expert Member
- May 9, 2019
- 385
- 592
Habari za wakati huu wakuu. Rejea hapa kwanza


Wakuu picha zima liko hapa Nafikiria kufanya maamuzi haya magumu japo naumia sana
Ikumbukwe bado nampenda kama hiki kipindi ambacho niko mbali nae atajirekebisha sitamuacha lakini asipojirekebisha nitaachana nae mazima.
Hakika sasa naiona amani ya moyo baada ya kukaa takribani siku tatu bila kuonana na mke wangu (nimetoka home na kwenda kuishi asipopajuwa)
Siku natoka sikumuaga alinisubili ilipofika saa 6 usiku akapiga simu nikamwambia nipo mitaa ya karibu hivyo ningerudi nyumbani muda mfupi, akauliza mbona haoni baadhi ya vitu vyangu nikamjibu navojuwa alielewa lakini kwa mashaka.
Nikazima simu nikaja kuwasha asubuhi ya kesho yake, kumbe wasiwasi umemjaa hajalala usiku mzima asubuhi kaenda kuripoti police kwamba hajui nilipo duuh.
Nimekuja kupata simu ya mama mmoja akijitambulisha kuwa yeye yuko kwenye kitengo cha ustawi wa jamii na kuwa amepewa taarifa na mke wangu kuwa sionekani.
Nikamjibu ,,,huyo kakurupuka mimi nipo sijapotea na anajuwa nilipo na mimi ni mzimawa afya wala msijali kabisa nikaongezea kwamba nitamtaarifu tena kama kasahau yaliyotokea na aliyokuwa anayafanya akitegemea mimi sina akili timamu. Ofisa akakata simu.
Kiufupi kwa sasa niko na amani nimempigia mara kadhaa kumsalimia na kuongea na mtoto japo mtoto bado hajajuwa kunyoosha maneno, nakula nashiba na nahisi moyo mtulivu zile kelele za kero sisikii tena hadi najiona nitafanikiwa mapema sana kwenye issue zangu.
Hakika nimeelewa kwa nini wengi walinambia ondoka,ondoka, ondoka ikiwezekana usigeuke nyuma bali hudumia mtoto tuu.
Nimepigiwa simu na rafiki yake anadai mke wangu hana amani kabisa. Nikamwambia anakudanganya nadhani now anafurahi kwamba nimeondoka.
Ahsanteni.



Wakuu picha zima liko hapa Nafikiria kufanya maamuzi haya magumu japo naumia sana
Ikumbukwe bado nampenda kama hiki kipindi ambacho niko mbali nae atajirekebisha sitamuacha lakini asipojirekebisha nitaachana nae mazima.
Hakika sasa naiona amani ya moyo baada ya kukaa takribani siku tatu bila kuonana na mke wangu (nimetoka home na kwenda kuishi asipopajuwa)
Siku natoka sikumuaga alinisubili ilipofika saa 6 usiku akapiga simu nikamwambia nipo mitaa ya karibu hivyo ningerudi nyumbani muda mfupi, akauliza mbona haoni baadhi ya vitu vyangu nikamjibu navojuwa alielewa lakini kwa mashaka.
Nikazima simu nikaja kuwasha asubuhi ya kesho yake, kumbe wasiwasi umemjaa hajalala usiku mzima asubuhi kaenda kuripoti police kwamba hajui nilipo duuh.
Nimekuja kupata simu ya mama mmoja akijitambulisha kuwa yeye yuko kwenye kitengo cha ustawi wa jamii na kuwa amepewa taarifa na mke wangu kuwa sionekani.
Nikamjibu ,,,huyo kakurupuka mimi nipo sijapotea na anajuwa nilipo na mimi ni mzimawa afya wala msijali kabisa nikaongezea kwamba nitamtaarifu tena kama kasahau yaliyotokea na aliyokuwa anayafanya akitegemea mimi sina akili timamu. Ofisa akakata simu.
Kiufupi kwa sasa niko na amani nimempigia mara kadhaa kumsalimia na kuongea na mtoto japo mtoto bado hajajuwa kunyoosha maneno, nakula nashiba na nahisi moyo mtulivu zile kelele za kero sisikii tena hadi najiona nitafanikiwa mapema sana kwenye issue zangu.
Hakika nimeelewa kwa nini wengi walinambia ondoka,ondoka, ondoka ikiwezekana usigeuke nyuma bali hudumia mtoto tuu.
Nimepigiwa simu na rafiki yake anadai mke wangu hana amani kabisa. Nikamwambia anakudanganya nadhani now anafurahi kwamba nimeondoka.
Ahsanteni.
