GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,554
- 108,895
Nikichukua maelezo ya mwenye PhD yake aliyoyatoa hivi majuzi tu halafu nilivyomsikia jana Halima Mdee akichambua Kiutaalam na Kiumakini kabisa masuala ya Kiuchumi kwa Tanzania naona au nadhani inabidi Yule Mtu wa juzi ambaye kiuhalisia ni mmiliki wa Shahada ya Uzamivu ( PhD ) basi angempa tu hiyo PhD yake Halima Mdee halafu na Yeye akabaki na Elimu ya Mdee.
Mbunge wa Kawe Halima Mdee sitaki kuwa mnafiki na bila kupepesa macho wala kumung'unya maneno na kutikisa masikio kwa ule ufafanuzi wako wa jana nakupa pongezi / kongole nyingi mno kwani umeonyesha kuwa hukuenda Shule kupata tu sijui Degree au Masters au PhD bali ulienda kuongeza maarifa yako ambayo kiukweli Mimi binafsi nimeyapenda.
Mwisho nitoe tu RAI kwa Mteuzi Mkuu wa Vyeo nchini Tanzania kuwa siku zingine akiwa anateua Watu wake wa kumsaidia Kazi basi si lazima awe tu anatumia Kigezo cha kuwa na PhD bali aamini kuwa kuna wengine kama akina GENTAMYCINE mwenye Elimu tu ya darasa la Saba na akina Halima Mdee wenye sijui Degree kama siyo Masters tunaweza kumsaidia hadi akashangaa kutokana na kwamba tumebarikiwa mno akili za kuzaliwa kuliko tu za kujibia na kupigia Chabo Mitihani Shuleni na Vyuoni.
Hongereni sana wale Watanzania ambao hivi sasa mnachukua PhD's zenu huko katika Vyuo Vikuu mbalimbali duniani ila ukweli tu ni kwamba na mfahamu kuwa hadi hivi sasa kwa PhD's tulizonazo nchini Tanzania hakuna ambazo zimeweza kuleta Tija yoyote kwa Taifa letu hili hivyo mnaposoma huko tambueni tu kwamba Watangulizi wenu wameshatuonyesha huko mlipo mnapoteza tu muda.
Tanzania inahitaji Watu wenye akili za Halima Mdee kama 100 tu ili nchi iende kuliko wenye PhD's 100,000 kama za Yule wa juzi ( ambaye aliropoka pasipo kuwa na data zozote ) ambazo hazina Tija yoyote ile kwa nchi yetu zaidi tu ya kutishiana tu humu mitaani.
Naamini kwamba message sent and delivered.
Nawasilisha.
Mbunge wa Kawe Halima Mdee sitaki kuwa mnafiki na bila kupepesa macho wala kumung'unya maneno na kutikisa masikio kwa ule ufafanuzi wako wa jana nakupa pongezi / kongole nyingi mno kwani umeonyesha kuwa hukuenda Shule kupata tu sijui Degree au Masters au PhD bali ulienda kuongeza maarifa yako ambayo kiukweli Mimi binafsi nimeyapenda.
Mwisho nitoe tu RAI kwa Mteuzi Mkuu wa Vyeo nchini Tanzania kuwa siku zingine akiwa anateua Watu wake wa kumsaidia Kazi basi si lazima awe tu anatumia Kigezo cha kuwa na PhD bali aamini kuwa kuna wengine kama akina GENTAMYCINE mwenye Elimu tu ya darasa la Saba na akina Halima Mdee wenye sijui Degree kama siyo Masters tunaweza kumsaidia hadi akashangaa kutokana na kwamba tumebarikiwa mno akili za kuzaliwa kuliko tu za kujibia na kupigia Chabo Mitihani Shuleni na Vyuoni.
Hongereni sana wale Watanzania ambao hivi sasa mnachukua PhD's zenu huko katika Vyuo Vikuu mbalimbali duniani ila ukweli tu ni kwamba na mfahamu kuwa hadi hivi sasa kwa PhD's tulizonazo nchini Tanzania hakuna ambazo zimeweza kuleta Tija yoyote kwa Taifa letu hili hivyo mnaposoma huko tambueni tu kwamba Watangulizi wenu wameshatuonyesha huko mlipo mnapoteza tu muda.
Tanzania inahitaji Watu wenye akili za Halima Mdee kama 100 tu ili nchi iende kuliko wenye PhD's 100,000 kama za Yule wa juzi ( ambaye aliropoka pasipo kuwa na data zozote ) ambazo hazina Tija yoyote ile kwa nchi yetu zaidi tu ya kutishiana tu humu mitaani.
Naamini kwamba message sent and delivered.
Nawasilisha.