Hatimaye FRELIMO iko matatani, mwisho wake umefika!

Hatimaye FRELIMO iko matatani, mwisho wake umefika!

H

Hapa ndo mjue siasa za ki Frica ni upuuzi sentence ina sema hivi kiongozi wa upinzani anaamulu maandamano huku akuwa mafichoni alikokimbilia baada ya kuuawa kwa aliyekuwa mqasheria wake maana yake yeye anapenda kuishi ataki kufa au kuumizwa kulemazwa lkn anaotaka kuwatawala ana waamulu waandamane ili??alafu wakifanikisha hayo maandamano kwa kuumizwa na kulemazwa atakuja kumtawala Nani? Na kwanini nayeye asije kuandamana Kama watu wengine Kama akiumizwa ionekane kaumizwa au kafa kwa kutetea haki za watu wake?
Mapinduzi yeyote au mabadiliko yeyote lazima yawe na gharama. Miongoni mwa gharama hizo ni watu baadhi kufa na wengine kuwa walemavu katika mtifuano sababu wenye madaraka hawatataka kuachia kirahisi.

Kinachotokea Tanzania ni kwamba wote hatutaki kuingia hio gharama ila tunategemea matokeo na watawala washajua udhaifu wetu. Sisi tunataka kwamba wakabidhi madaraka kwa maombi ya mitandaoni na kutia huruma mithili ya ngamia anavyokaa kibla kwa dua ili achinjwe. Yani wa Lumumba fc wakae kibla kwa blaah blaah zenu mitandaoni? Mtakunywa sana supaletta bar.
 
Sio mwa fisiem vs sisi manyumbu.. Unadhani bongo nyoso kiongozi akae ufichoni atoe maelekezo kuna mtu ataingia road, sisi ni maiti zinazotembea, labda vizazi vijavyo, wakikuta population tushagota kwenye milioni 100 huko, badari ishauzwa kwa mwarabu, gesi ya mchina.. Miradi yote imebinafsishwa, mfagizi wa ofisi ni muhindi, mbuga zote za wanyama zimepigwa bei, madini wameachiwa wachache, asilimia 10 tu ndio wanafaidika the rest kula ugali maharage ni anasa huenda hawa wakawa wamefufuliwa na ujio wa nabii issa.
Bongo kila mtu anataka aishi haijalishi anaishije ila hataki tabu na mtu. Unategemea kuna maandamano humo! Mnategemea CCM iondoke madarakani kwa dua?🤣
 
Bongo kila mtu anataka aishi haijalishi anaishije ila hataki tabu na mtu. Unategemea kuna maandamano humo! Mnategemea CCM iondoke madarakani kwa dua?🤣
Utajiri wa CCM ni uwoga na ujinga wa mtanzania.

Hii haiwezi kubadilika kwa kizazi chetu sisi.
 
Ni swala la muda tu, hata hawa majangili wa kijani nao watafurumushwa. Maana kama kuchokwa, tushawachoka. Imebaki kutolewa kwa mateke tu.
We ngedere pambana na chagadema yenu, CCM watanzania bado wanaipenda na kuiamini, our country cannot be lead by dogs. CCM mpaka miaka 100 ijayo itakuwepo
 
Yatatoka tu. Unajua ccm wana-survive kwa sababu hatuna chama imara cha upinzani. Ukitaka kuona cdm kinaimarika mtoe Mbowe pale juu muweke Lema au yule jamaa wa Mkoa wa Mara
Lema ? Kwl nyie ni wehu. Yule mvuta bangi mwizi wa magari awe
M/kiti? Hilo litakuwa genge la wahuni.
 
Hapa kwetu yametuweza. Tumezamishwa kwenye dini kama mambumbumbu. Akishika mkristo anatetewa na Wakristo na waislamu hivyo hivyo. Hata kama ni ujinga unafanyika.
Wala dini siyo ishu. Changamoto ni jeshi la polisi kufungamana na watawala. Hapo ndio utata maana watu kupigwa kuumizwa hawataki ila wanataka mabadiliko.
 
Kwa wanaofuatilia siasa za Mozambique, hali ni mbaya kwa chama tawala cha Frelimo pamoja na serikali iliyoko madarakani. Baada ya uchaguzi kuisha na serikali kujitangaza kushinda kwa wastani wa asilimia sabini, wananchi wameikata, wakiongozwa na kiongozi wa upinzani Venancio Mondlane.

Kinachotokea sasa hivi ni kwamba huyu kiongozi wa upinzani ndiye mwenye nguvu na sauti kuliko serikali; yeye ndiye anayeamuru nini kifanyike. Anaratibu maandamano akiwa mafichoni, baada ya kukimbia nchi kufuatia mauaji ya wakili wake.

Hali si shwali. Mfano jana, ameamrisha kufanyika maandamano kwa siku tatu bila kupumzika, akilenga bandari kufungwa pamoja na mipaka. Kumeitikiwa kwa muitikio mkubwa katika miji yote mikubwa ya Maputo, Beira, na Nampula pamoja na miji mingine midogo, huku karibu watu 40 wakiwa wameuwawa na polisi.

Inchi inaongozwa na mtu aliyeko mafichoni, huku Rais Nyusi akiwa hana sauti. Ukiona mwenzako ananyolewa.

Soma, Pia: Yanayojiri kwenye Uchaguzi Mkuu wa Msumbiji: FRELIMO (Chama rafiki ya CCM) kushinda Uchaguzi 09 Oktoba?
Tatizo lenu CHADEMA Mboe akitangaza maandamano hamufiki pale Boma na badala yake munaandamana humu JF.
 
15 November 2024

Uchafuzi wa Uchaguzi Msumbiji 2024: Ghasia za baada ya uchaguzi na ukandamizaji lazima zikome, wanasema wataalam wa Umoja wa Mataifa​

9:34 | 15 Nov 2024

Haki zisizo za kibinadamu.un_

Picha: OHCHR
  • 15 Novemba 2024
Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa* leo wamezitaka mamlaka nchini Msumbiji kuzuia na kukomesha mara moja unyanyasaji na ukandamizaji wa waandishi wa habari, wanasheria, watetezi wa haki za binadamu na waandamanaji na kuhakikisha waliohusika wanachunguzwa na kufunguliwa mashtaka.


Kufuatia uchaguzi wa tarehe 9 Oktoba 2024 nchini humo, ripoti thabiti zinaonyesha ghasia na hatua za ukandamizaji zilizotumiwa dhidi ya waandamanaji katika maandamano ya amani, ambayo yaliendelea na kutolewa ripoti hadi tarehe 7 Novemba 2024, yalisababisha vifo vya watu 30, kujeruhi watu 200 na kupelekea kukamatwa kwa angalau 300.


"Ukiukwaji wa haki ya kuishi, ikiwa ni pamoja ya watoto, mauaji ya makusudi ya waandamanaji wasio na silaha na utumiaji nguvu kupita kiasi wa polisi waliotumwa kutawanya maandamano ya amani kote Msumbiji ni jambo la kustusha sana," wataalam walisema.

"Tunatoa wito kwa mamlaka za Msumbiji kuchunguza kwa haraka na bila upendeleo mauaji yote kinyume cha sheria."

Maandamano kadhaa katika wiki za hivi karibuni kupinga kukosekana uadilifu katika mchakato wa uchaguzi.

"Mamlaka zinahitaji kuchukua hatua kukomesha ghasia na kuhakikisha mazingira ambayo wananchi wote wa Msumbiji, ikiwa ni pamoja na wanawake na wasichana, wanaweza kushiriki kikamilifu na kwa usawa katika michakato ya kisiasa na kujieleza bila woga," wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa walisema.


"Wasimamizi wa sheria wana jukumu la kuheshimu na kulinda wale wanaotumia haki yao ya kukusanyika kwa amani, na maafisa lazima wawe na msimamo na kutopendelea wakati wa maandamano yoyote, kuzuia madhara na kulinda haki ya kuishi, uhuru na usalama wa watu wanaohusika katika maandanano."

Wataalamu hao walisema kutoweka kwa usalama atika muktadha wa ghasia za uchaguzi kuna athari ya kudumu kwa mfumo wa kidemokrasia wa Mataifa.


Vikwazo kwa uhuru wa vyombo vya habari pia vimeripotiwa sana, ikiwa ni pamoja na mashambulizi, vitisho na unyanyasaji wa wanahabari, na mtandao wa intaneti kuzimwazimwa na vizuizi vya mara kwa mara kwa huduma za mtandao wa simu za viganjani.

Watetezi wa haki za binadamu wanaoripoti kuhusu ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi, uchafuzi wa chaguzi au ripoti za kushiriki maandamano wametishwa na hivyo kuingia hofu.

"Tunaziomba mamlaka za Msumbiji kuwezesha upatikanaji wa taarifa kwa wote na tunalaani usumbufu mkubwa wa huduma za mtandao, ambao umeripotiwa sanjari na maandamano na maandamano yaliyotangazwa," wataalam hao walisema.

Wataalamu wa Kimataifa wa Umoja wa Mataifa wapo katika mazungumzo na mamlaka ya Msumbiji kuhusu masuala haya na wanafuatilia kwa karibu hali hiyo.

*Wataalamu hao: Gabriella Citroni (Mwenyekiti-Rapporteur), Grażyna Baranowska (Makamu Mwenyekiti), Aua Baldé, Ana Lorena Delgadillo Pérez na Mohammed Al-Obaidi, Kikundi Kazi cha Kutoweka kwa Kutekelezwa au Kutoweka kwa Hiari; Irene Khan , Ripota Maalum kuhusu ukuzaji na ulinzi wa haki ya uhuru wa maoni na kujieleza; Gina Romero , Ripota Maalum kuhusu haki za uhuru wa kukusanyika kwa amani na kujumuika; George Katrougalos, Mtaalamu wa Kujitegemea juu ya kukuza utaratibu wa kimataifa wa kidemokrasia na usawa; Mary Lawlor , Mwandishi Maalum wa watetezi wa haki za binadamu; Reem Alsalem , Ripota Maalum kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na wasichana; Margaret Satterthwaite , Mwandishi Maalum kuhusu uhuru wa majaji na mawakili; Morris Tidball-Minz , Ripota Maalum juu ya utekelezaji usio wa kisheria, muhtasari au unyongaji kiholela; na Alice Jill Edwards , Ripota Maalum wa Mateso na Adhabu au Adhabu nyingine za Kikatili, Kinyama au za Kushusha hadhi.


Wanahabari Maalum ni sehemu ya kile kinachojulikana kama Taratibu Maalum za Baraza la Haki za Kibinadamu. Taratibu Maalum, chombo kikubwa zaidi cha wataalam huru katika mfumo wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, ni jina la jumla la mifumo huru ya Baraza la kutafuta ukweli na ufuatiliaji ambayo inashughulikia ama hali maalum za nchi au masuala ya mada katika sehemu zote za dunia.


Wataalam wa Taratibu Maalum hufanya kazi kwa hiari; wao si wafanyakazi wa UN na hawapati mshahara kwa kazi zao. Wako huru dhidi ya serikali au shirika lolote na wanahudumu kwa nafasi zao binafsi.


Chanzo: Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu (OHCHR) / Taarifa kwa Vyombo vya Habari. Geneva.
 
15 November 2024

Msumbiji: Rais atoa wito wa umoja katika "nyakati zenye changamoto"​

3:05 | 15 Nov 2024

Filipe-Nyusi-2

Picha: O País. Mheshimiwa rais Felipe Nyusi wa Mozambique

Rais wa Msumbiji leo ametoa wito wa umoja kati ya wananchi wa Msumbiji katika "nyakati za taabu na changamoto", akisema kuwa serikali itasalia kuzingatia amani na maridhiano, maadili yaliyomo katika Mkataba wa Amani na Kitaifa wa Maridhiano.


"Thamani za amani na upatanisho, zilizojumuishwa katika Mkataba wa Maputo, zinaendelea kuwa msingi wa maslahi ya kitaifa ya Msumbiji na kwa mustakabali wenye mafanikio," Filipe Nyusi alitangaza wakati wa kufunga kozi ya 11 ya Wakuu wa Pamoja wa Wafanyakazi na Ukuzaji Rasmi wa 13. bila shaka.

"Mkataba wa Maputo" - rasmi Mkataba wa Amani na Upatanisho wa Kitaifa - ulitiwa saini na serikali na Upinzani wa Kitaifa wa Msumbiji (Renamo) mnamo 2019, na kukomesha mzunguko wa ukosefu wa utulivu nchini.


"Kama taifa, tumeweza kushinda changamoto na lazima tuendelee kwenye njia hii, lakini lazima tukumbuke kwamba, kila wakati dhamira yetu ya kuleta amani inapowekwa kwenye majaribu, uthabiti wetu unakua na tunaibuka na nguvu," alisema Rais. akibainisha kuwa Msumbiji ilishiriki hata uzoefu wake katika kujenga amani katika Umoja wa Mataifa.


"Katika nyakati ngumu na zenye changamoto, umoja unakuwa sio muhimu tu, lakini muhimu. Mustakabali wetu, taifa letu, familia zetu, watoto wetu wanatoa wito kwa kila mmoja wetu kupiga hatua nyingine mbele kwa ari na matumaini,” aliteta.

Pia katika hotuba yake, Filipe Nyusi alitangaza kuwa zaidi ya asilimia 73 ya wanufaika wa mchakato wa Upokonyaji Silaha, Uhamishaji na Maridhiano (DDR) kwa waliokuwa wanamgambo wa RENAMO tayari wameanza kupokea pensheni zao.


Kufuatia Maridhiano ya DDR, kesi 4,215 [za athari za pensheni] zilipokelewa na Wizara ya Wapiganaji, ambapo 3,930 (81%) walipokea kibali kutoka kwa Mahakama ya Utawala. Kati ya idadi hii, waasi 3,808 wa zamani waliohifadhiwa na DDR tayari wanaona pensheni zao zikilipwa katika akaunti zao za benki, rais alisema
Chanzo : LUSA,
 
Wala dini siyo ishu. Changamoto ni jeshi la polisi kufungamana na watawala. Hapo ndio utata maana watu kupigwa kuumizwa hawataki ila wanataka mabadiliko.
Hata Mozambique polisi walikuwa kalibu sana na watawala lakini sasa hivi pumzi inakata, nisema hawa kilichowasaidi ni ile vita ya wenyewe kwa wenyewe, sasa hivi wanamkumbuka Alfonso dhalakama kama alikuwa mtu sahihi kwao wanamlani Chissano ndiye alieasisi wizi, dhuluma na umaskini waliyokuwa nao
 
Back
Top Bottom