Chacha Wangwe alikufa kifo cha ajali. Utamlinganisha na Kolimba?Waangalie yasije kuwatokea ya Chacha Wangwe!!
Chacha Wangwe alikufa kifo cha ajali. Utamlinganisha na Kolimba?Waangalie yasije kuwatokea ya Chacha Wangwe!!
Shibuda na Zitto wapo kimaslahi binafsi zaidi, shibuda kaona akina Sumaye na wanaharakati wengine wanaiponda CCM na kuisifia CDM wanataka kujiweka kama na yeye Mwana-Ukombozi. KWA TAARIFA YENU HAKUNA MWANA UKOMBOZI LEGE LEGE KAMA HAWA WAWILI AMBAYE ANAANGALIA NA KUSEMA LAKINI CCM WANAFANYA VIZURI, kama ni hivyo kwa nini usijiunge nao. Woote hawa kwenye historia ya ukombozi hawatakuwepo, Zitto alianza vizuri saana sasa tatizo ni umaskini na msimamo ni ngumu kama ngamia kuingia katika tundu la sindano, wakampa pesa akanyamaza.
Hata usipomfahamu JK kama Rais halali wa Tz bado JK anabaki kuwa Rais wa Tz.
Halali maana yake ni kwamba "Alitangazwa na NEC" kuwa mshindi.
Sasa tofauti inakuja kwamba Je, NEC walimtangaza mshindi halali??
Baadhi yetu tunaamini mshindi hakuwa JK, lakini chombo halali (NEC) kikampa urais.
Kwa habari ya Shibuda Magalle nawashauri CDM wamkubali kama alivyo, sasa mnataka wabunge wote wa CDM wawe kama Dada Regia au Mnyika hiyo diversity itatoka wapi?? Ruhusuni wenye kuthubutu kuongea wawepo ndani ya chama ili siku Dr. Slaa au Mbowe wakitoka bila nguo awepo wa kusema "mkuu leo umesahau kuvaa".
La muhimu wasimwingize kwenye nafasi nyeti za chama.
John Shibuda, ameibuka na kutetea maandamano yanayofanywa na chama chake, huku akionya CCM kuacha kufanya kile alichokiita mchezo wa kugeuza polisi kuwa ICU ya kutibu maradhi yake ya siasa za ufisadi.
Kukosekana kwa Shibuda katika maandamano na mikutano ya Chadema hata yalipotua mkoani kwake Shinyanga, kuliibua mguno wa chini chini miongoni mwa wapenzi na washabiki wa chama hicho.
Source : Gazeti la Mwananchi la leo
Wakuu, huyu " Chibuda" tunaweza kweli kumwamini au ni kauli "danganya toto" ???:A S 13:
Na wewe ni nani anayekuamini! Tuache tabia za kitoto. Kama wewe humwamini kaa kimya siyo unaanza kumobilize wengine!