Huyu Mzee sabodo lazima kuna jambo nyuma ya pazia,aidha anajua chadema wanakuja kutwala na yeye ana madudu mengi anajificha au anatafuta huruma,au anatumiwa na mafisadi wenzake kuwanunua viongozi wetu wa baadaye,sijawahi kusikia hata ulaya mtu mmoja akachangia harusi milion 60,tujiulize kuna nini ndani ya box?
kazi ya kujenga visima, barabara, hospital na mashule ni kazi ya serikali, ni makosa sana yaliyofanywa na serikali kututwishwa wananchi mzigo wa kujenga shule, au hopital, Sabodo hana haki yoyote ya kulazimishwa kufanya jambo ambalo ni jukumu la serikali, anavyofanya hivyo ni kwa kujitoa kweke tu, Hizo ni pesa zake na yeye ndio mwenye uamuzi wa kuzigawaChenge, EL, Rostam na wengineo wana Mabilioni na wala hujawahi kuweka uzi humu wa kuwalalamikia watu hawana visima,
Tusijifanye hatujui taratibu za uchangiaji kwenye maarusi!
Mchangiaji kawaida anapeleka fedha kwenye kamati ya maandalizi, wala hamkabidhi mwenye shughuli.
Unless kama mna uhakika kuwa alikabidhiwa mkononi, ndipo na mimi nitawaunga mkono kulaumu, kwasasa noway!
Watanzania kinacho tusumbua ni njaa tu na wivu, huyo mtu anapesa za kutosha tusipende kujaji vitu ambavyo hatuna uwezo navyo acha watu wamchangie Dr slaa.