Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,320
Kama alivyoimba Mwana dada na nguli wa muziki wa bongo fleva Judith Wambura,"Siku hazigandi ". Ule mpambano wa kukata na shoka kati ya CCM na Mh Lowasa umewadia. Kila upande kwa nafasi yake umekuwa ama ukikwepa au ukisita kuingia katika mpambano. Mara ya kwanza ilikuwa ni kwenye bunge la jamhuri pale" caucus "ya chama ilipokubali ripoti ya Richmond kujadili bungeni. Mh Lowasa alipopewa nafasi ya kujitetea bungeni aliahilisha mpambano kwa kuamua kujiuzuru Uwaziri mkuu. Wengi turidhani kwa kuwa wao walimwaga mboga basi yeye angemwaga ugali. Mara ya pili ni pale ripoti ya ndg Mkama ambae alikuja kuwa katibu mkuu wa CCM iliposema chama kimepoteza mvuto kwa kuwakumbatia mafisadi. Ili kujisafisha ilibidi kujivua gamba na mmoja wa waliotakiwa kujivua alikuwa Mh Lowasa. Hata hivyo kujivua gamba kulimalizika huku CCM na Mh Lowasa kila mmoja akionekana kumkwepa mwenzake. Mara ya Tatu ilikuwa ni hatua ya chama kuwasimamisha makada wake kujihusisha na siasa kwa miezi 12 (Mh Lowasa alikuwa miongoni mwa waliosimamishwa)). Miezi 12 iliisha na mpambano ukawa umeahirishwa. Safari hii Mh Lowasa akiwa anajipambanua (kwa kauli na matendo yake) kama mgombea bora na mwenye mvuto kuwazidi wenzake ndani ya CCM, Chama kinasisitiza hakiwezi kusimamisha "mgombea mwenye kumwosha kwa dodoki". Mpambano huu umekuwa ukiahirishwa lakini safari hii lazima ufanyike. Huku Chama kule Mh Lowasa (na team yake). Sijui nani atashinda.