Mjenda Chilo
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 1,467
- 513
Nichukue fursa hii kumpongeza Mh. makala, baada ya Sugu kukomaa na hii studio iliyotolewa na Rais kwa kikundi cha fleva unit kupelekwa baraza la sanaa ili kuwanufaisha wanamuziki wote serikali kupitia kwa naibu waziri huyu imekiri kuwa itabidi wamshauri rais airudishe basata. Kuonyesha hiki kikundi kuomba studio hiyo pia waliomba walipiwe kodi ya pango ya studio, Rais akatoa mil 9, jamaa wakaomba hela ya ukarabati na ya mtaalam. kodi imeisha wanaomba tena walipiwe du? kwahiyo yale majibu mepesi waliyokuwa wakimjibu sugu kuwa walioomba ndo waliopewa ina maana hawakujua haya? mbona ilikuwa wazi? Mi sikumwamini kabisa Mh alipoteuliwa ila kwa hili nakuona umethubutu. Hongera