PendoLyimo
JF-Expert Member
- Sep 30, 2014
- 1,059
- 1,133
Umoja wa wasomi wa vyuo vikuu wanaotokea wilayani Ngorongoro wamezungumza masuala mbalimbali kuhusiana na wilaya yao.
wameeleza sababu za wao kujaza mifugo hifadhini humo walipozungumzia habari iliyochapishwa na Gazeti la JAMVILAHABARI kuhusu changamoto ya muingiliano baina ya watu, uhifadhi na mifugo katika hifadhi ya Ngorongoro inayopelekea kuhatarisha kwa uhai na uwepo wa hifadhi hiyo.
Katika utetezi wake mmoja wa wasomi hao anayeonekana katika video hii, amekiri kuwepo kwa makundi makubwa ya mifugo hifadhini humo tofauti na hali ya uwezo wa hifadhi na hivyo kusema uwingi wa makundi ya mifugo hifadhini humo kwao upande wao ni jambo la kawaida kwani ndio chanzo chao pekee cha kujikimu na maisha na kwamba isingetarajiwa isingekuwepo mifugo hiyo.
Hivi karibuni gazeti la JAMVILAHABARI liliandika kuhusiana na Hatari inayoikumba hifadhi hiyo ya kipekee Nchini baada ya kujionea hali ilivyokuwa mbaya kwa muingiliano kuwa mkubwa baina hifadhi, watu, wanyamapori na mifugo.
waratibu wa wa Kituo cha wanahabari watetezi wa Rasilimali na Taarifa (Media Centre for Information and Resources Advocacy - MECIRA), wamesisitiza kuwa Hali ni mbaya Hifadhini Ngorongoro na jitihada za makusudi kunusuru tatizo hili zinahitajika ili pande zote zinazoihusu hifadhi hiyo ambazo ni watu, mifugo, mimea Maliasili zilindwe.